mamii90
JF-Expert Member
- Oct 5, 2014
- 380
- 265
Habari,
Hili jambo limenitesa miaka nenda miaka rudi, natamani lifike mwisho.
Wakati naingia kwenye mahusiano na huyu ambae ni mume wangu sasa, alikuja binti mmoja ambaye alikuwa ndo kamaliza form 4 (mdogo wake) akaanza kusoma cozi kwenye chuo flani.
Nikapata ujauzito so ikabidi nilete binti wa kazi. Na mimi katika maisha yetu nimelelewa na mabinti wa kazi, sipendi wateseke kabisa maana niliona walivyomsaidia mama enzi tunakua, so shida ikaanza anamuachia yule binti kila kitu afanye, hadi ampikie amuamshe chumbani, yale mambo yalikua yananikera nikaanza kumsema kwa nguvu sana, hakubadilika. Ikabidi nimwambie kaka yake. Kaka yake akasema kama unamuona msichana wako anapata shida basi nitamuekea msichana wake yeye
Ile hali ikaendelea sana kwa muda na yule binti alikua mdogo kwa hiyo ikabidi niwe napika mwenyewe, siku zikaenda akaja tena mdogo wake wa kiume, wote kazi ikawa ile ile, huyu wa kiume hadi anamwambia dada amfulie nguo. Nilikua naongea napiga mzigo nadeki mpaka mimba ina miezi nane ndo mama angu akaja.
Kiukweli niliteseka mimba ya huyu mtoto, ugomvi ndani ya nyumba hautuliii kabisaa; wakaungana wote na mama zake kwamba niachike. Na kweli mume wangu akasema natamani kukuacha ni vile tu tumefunga ndoa.
Hapo nimeskip kipindi cha ndoa maana tulifunga ndoa tayari huyu binti tunaishi nae kuna mengi yalitokea lakini nitaeleza tu tukio moja.
Usiku wa kesho yake ndio ndoa akaniambia kwa hiyo kwenye hiyo saluni uliyofanya booking na mimi nitasuka? Nikamwambia ni maids tu wewe hautaenda pale, aliangua kilio imagne na kuna wageni, mume wangu haya maswala ya maids hajui anasema kwanini unaenda kuremba watu baki unamuacha huyu? Akaninuia tumeenda kusameshana wakati wakuvalishana pete ya ndoa.
Unaweza ukahisi movie ila sio movie ni maisha watu tunapitia.
Wakati wa sherehe huyu binti na wenzake kwenye ile meza ya wazazi wangu hawakupeleka vinywaji kabisa maana wao ndo walikua kwenye hiyo kamati ya vinywaji na mama zake wadogo.
Sasa huyu binti alikuja baadae kwenda hostel mimi mimba ikiwa kubwa kama miezi 8 ambapo na mama ndo akaja. Sasa wakati wa X-mass maana ilikuwa hata bado sijajifungua kaka yake akampigia simu aje kula sikukuu nyumbani, hakuja kabisa akaenda kwa dada mmoja ambae alikuja baadae kuwa mtu wa karibu na mimi. Huyo dada akamwambia mbona hujaenda kwa kaka kula sikukuu? Akasema, KAJAZA NDUGU ZAKE SIWEZI KWENDA PALE.
Kiukweli alikua kaja mama yangu na mjukuu wake na mdogo wangu, alikuja kusalimia, nikihesabu muda kwa ujumla waliokaa pale ni kama wiki tatu, dogo akaondoka na mimi nikawa nimejifungua nikakaa wiki2 nikaondoka na mama kurudi nyumbani.
Sasa imagne watu hawajakaa hata mwezi yeye kaona kero ila wenyewe miaka nenda rudi wapo.
Alikuja kumaliza chuo ila hakupata kazi, akaenda kwao akarudi tena akasoma tena akamaliza hakupata kazi. Na hii ya mara ya pili, wembe ukawa ule ule, hafanyi chochote analala tu dada amfanyie kila kitu.
Sasa hii mara ya tatu anasoma tena ila anawahi kuondoka asubuhi jion kuna siku anachelewa kuna siku anawahi kurudi, ila ndo hivyo hasaidii chochote, yaani dada ndo afanye kila kitu.
Namuuliza anasema naoshaga sahani yangu pekee. Namuuliza na hivyo vingine anasema nawahi kuamka kwa hiyo siwezi.
Leo mpaka naandika niko bize napika yeye amekaa anachat, nikamwambia mimi siwez kukupikia wewe unachat hapo jipe shuhuli wala hajanisikia kitu. Kaenda kununua chips.
Mbaya zaidi nyuma ya pazia kuna rafiki yake mume wangu wametafutana wanapanga yao huko (na huyo kaka alihusika sana kwa yule baby mama wa mr kumuondoa)
Na kingine kikubwa ni kwamba mama yake anaona kawaida tu hata ukimwambia.
Ashawahi iba nguo zangu akaenda kugawa, aliyempa akapiga picha akaweka Insta nikaiona ile nguo nikambana akasema alimpa, nikamwambia akaifate akampigia mama ake na mama ake akasema muulize (yaani aniulize mimi) hiyo nguo ni bei gani atume ela.
Nimeruka mambo mengi ila kuna dada wa saluni pia alishawahi kuniita akaniambia kuwa makini na huyu binti anaweza akakuua.
Sasa ndugu zangu nifanyaje hapa, wako wawili yeye na huyo shemeji wote wanataka tuwahudumie kama ambavyo namuhudumia kaka yao yaani mimi na dada ndo tuwafanyie kila kitu.
Na kingine kikubwa ana mawasiliano ya karibu mno na yule dada aliyezaa na mume wangu pamoja na yule aliyehusika kupika figisu.
Nifanyaje kuimaliza hii nightmare wandugu maana kila nikimuona anapita nakumbuka machungu hasa enzi za mimba maana ilikua niachwe kwa sababu yake.
Roho inaniuma, nina uchungu sana
=======
Michango ya wadau
Hili jambo limenitesa miaka nenda miaka rudi, natamani lifike mwisho.
Wakati naingia kwenye mahusiano na huyu ambae ni mume wangu sasa, alikuja binti mmoja ambaye alikuwa ndo kamaliza form 4 (mdogo wake) akaanza kusoma cozi kwenye chuo flani.
Nikapata ujauzito so ikabidi nilete binti wa kazi. Na mimi katika maisha yetu nimelelewa na mabinti wa kazi, sipendi wateseke kabisa maana niliona walivyomsaidia mama enzi tunakua, so shida ikaanza anamuachia yule binti kila kitu afanye, hadi ampikie amuamshe chumbani, yale mambo yalikua yananikera nikaanza kumsema kwa nguvu sana, hakubadilika. Ikabidi nimwambie kaka yake. Kaka yake akasema kama unamuona msichana wako anapata shida basi nitamuekea msichana wake yeye
Ile hali ikaendelea sana kwa muda na yule binti alikua mdogo kwa hiyo ikabidi niwe napika mwenyewe, siku zikaenda akaja tena mdogo wake wa kiume, wote kazi ikawa ile ile, huyu wa kiume hadi anamwambia dada amfulie nguo. Nilikua naongea napiga mzigo nadeki mpaka mimba ina miezi nane ndo mama angu akaja.
Kiukweli niliteseka mimba ya huyu mtoto, ugomvi ndani ya nyumba hautuliii kabisaa; wakaungana wote na mama zake kwamba niachike. Na kweli mume wangu akasema natamani kukuacha ni vile tu tumefunga ndoa.
Hapo nimeskip kipindi cha ndoa maana tulifunga ndoa tayari huyu binti tunaishi nae kuna mengi yalitokea lakini nitaeleza tu tukio moja.
Usiku wa kesho yake ndio ndoa akaniambia kwa hiyo kwenye hiyo saluni uliyofanya booking na mimi nitasuka? Nikamwambia ni maids tu wewe hautaenda pale, aliangua kilio imagne na kuna wageni, mume wangu haya maswala ya maids hajui anasema kwanini unaenda kuremba watu baki unamuacha huyu? Akaninuia tumeenda kusameshana wakati wakuvalishana pete ya ndoa.
Unaweza ukahisi movie ila sio movie ni maisha watu tunapitia.
Wakati wa sherehe huyu binti na wenzake kwenye ile meza ya wazazi wangu hawakupeleka vinywaji kabisa maana wao ndo walikua kwenye hiyo kamati ya vinywaji na mama zake wadogo.
Sasa huyu binti alikuja baadae kwenda hostel mimi mimba ikiwa kubwa kama miezi 8 ambapo na mama ndo akaja. Sasa wakati wa X-mass maana ilikuwa hata bado sijajifungua kaka yake akampigia simu aje kula sikukuu nyumbani, hakuja kabisa akaenda kwa dada mmoja ambae alikuja baadae kuwa mtu wa karibu na mimi. Huyo dada akamwambia mbona hujaenda kwa kaka kula sikukuu? Akasema, KAJAZA NDUGU ZAKE SIWEZI KWENDA PALE.
Kiukweli alikua kaja mama yangu na mjukuu wake na mdogo wangu, alikuja kusalimia, nikihesabu muda kwa ujumla waliokaa pale ni kama wiki tatu, dogo akaondoka na mimi nikawa nimejifungua nikakaa wiki2 nikaondoka na mama kurudi nyumbani.
Sasa imagne watu hawajakaa hata mwezi yeye kaona kero ila wenyewe miaka nenda rudi wapo.
Alikuja kumaliza chuo ila hakupata kazi, akaenda kwao akarudi tena akasoma tena akamaliza hakupata kazi. Na hii ya mara ya pili, wembe ukawa ule ule, hafanyi chochote analala tu dada amfanyie kila kitu.
Sasa hii mara ya tatu anasoma tena ila anawahi kuondoka asubuhi jion kuna siku anachelewa kuna siku anawahi kurudi, ila ndo hivyo hasaidii chochote, yaani dada ndo afanye kila kitu.
Namuuliza anasema naoshaga sahani yangu pekee. Namuuliza na hivyo vingine anasema nawahi kuamka kwa hiyo siwezi.
Leo mpaka naandika niko bize napika yeye amekaa anachat, nikamwambia mimi siwez kukupikia wewe unachat hapo jipe shuhuli wala hajanisikia kitu. Kaenda kununua chips.
Mbaya zaidi nyuma ya pazia kuna rafiki yake mume wangu wametafutana wanapanga yao huko (na huyo kaka alihusika sana kwa yule baby mama wa mr kumuondoa)
Na kingine kikubwa ni kwamba mama yake anaona kawaida tu hata ukimwambia.
Ashawahi iba nguo zangu akaenda kugawa, aliyempa akapiga picha akaweka Insta nikaiona ile nguo nikambana akasema alimpa, nikamwambia akaifate akampigia mama ake na mama ake akasema muulize (yaani aniulize mimi) hiyo nguo ni bei gani atume ela.
Nimeruka mambo mengi ila kuna dada wa saluni pia alishawahi kuniita akaniambia kuwa makini na huyu binti anaweza akakuua.
Sasa ndugu zangu nifanyaje hapa, wako wawili yeye na huyo shemeji wote wanataka tuwahudumie kama ambavyo namuhudumia kaka yao yaani mimi na dada ndo tuwafanyie kila kitu.
Na kingine kikubwa ana mawasiliano ya karibu mno na yule dada aliyezaa na mume wangu pamoja na yule aliyehusika kupika figisu.
Nifanyaje kuimaliza hii nightmare wandugu maana kila nikimuona anapita nakumbuka machungu hasa enzi za mimba maana ilikua niachwe kwa sababu yake.
Roho inaniuma, nina uchungu sana
=======
Michango ya wadau
Mpendwa
Pole kwa unayopitia,
Naomba kujua maswala mawili ambayo hujayaweka wazi sana
Je huyo mwana mke aliezaa na mumeo mahusiano yao yalidumu kwa muda gani na ilikua ni baada ya ndoa yenu au labla?
Na sababu ya kuachana nae ilikua nini?
Pili, wewe na mumeo mlikutana mkapendana wenyewe au mlilazimishwa na wazazi?
Cha kukushauri, kweli huwa tunaolewa kwenye familia za watu na tunakutana na ndugu wenyw tabia tofauti, cha msingi ni kutumia busara kuliko kutumia nguvu au hasira
Jaribu kutafuta better moment, ongea na mumeo, ikiwezekana hao ndugu muwatafutie shughuli ya kufanya ili waweze kujitegemea badala ya kuwategemea nyinyi
Msipofanya hivyo, hamuwezi kutatua mgogoro uliopo kati yenu na ndoa yenu haitapata amani
Usichukue hasira, enedelea na majukumu yako kama mke, wapikie wakaribishe chakula, ondoa vyombo, maana hapo ni kwako.
Jaribu kuepuka mambo ambayo yataleta ugomvi kati ya mumeo na nduguze
Ila tafuta muda uongee na mumeo hao ndugu wapate cha kufanya ila na nyinyi mpate nafasi ya kufanya maisha yenu
Mumeo ana makosa makubwa na inawezekana kuna mengi nyuma ya pazia yanaendelea kati ya mumeo na nduguze, pengine mumeo bado ana mahusianonna huyo mwanamke alise zaa nae na ndugu wapo upande wake, jaribu kuchunguza na uwe makini katika kila step
All in all mahusiano yakisha fika stage hiyo, mkiona mmeshindwa kuzungumza mkaelewana, watafute watu wa karibu yenu, ikiwezekana hata marafiki ambao wana hekima, wajaribu kuzungumza na mumeo kujua shida ipi wapi@mamii90,
Pole kwa yanayokusibu!
Kwa ridhaa yako naomba kusema nawe mambo machache yafuatayo.
Mosi: nilichokiona ni ushindani kati yako na upande wa mmeo kuonesha ni nani mwenye haki zaidi. Unapoingia kwenye ushindani huo unakuwa umejiondolea mamlaka yako ya umama wa familia.
Ulichopaswa kufanya ni kutoshindana nao, wachukulie ni wapitaji tu na hawataishi hapo milele, lakini pia kumbuka kuwa wewe huwezi kuwa mkamilifu tu na wao ndo wakosaji tu. Kuna pahala hata wewe unakosea na kuwakosea. Shida kubwa inakuja pale kila upande unapong'ang'ania mtazamo wake wa usahihi wake hata kama hauko sahihi.
Pili unaonekana kuwa mtu asiyesamehe na kusahau mambo, badala yake unaendelea kuorodhesha na kuongezea yale waliyokukosea. Hili linakufanya uone ubaya tu na pia unazidi kujijaza chuki na hasira. Mwisho wa siku utajifukuzisha mwenyewe.
Cha kufanya, samehe yote kwa dhati na sahau, jitahidi kuona uzuri na mazuri yao hata kama ni kidogo. Jenga mtazamo chanya na usiweke maneno akilini mwao. Acha kuongozwa na hisia hasi dhidi yao.
Kuhusu mmeo, huwezijua amefikaje pale alipo, kwa hiyo inawezekana amebebwa na familia kwa namna ambayo hawezi kuilipa. Mazingira ya hivyo yanaweza kumjengea upofu, na pengine ndiyo maana kila ukimshirikisha matatizo ya nduguze anaona kama unamtenganisha nao.
Kwa upande huu, ongea na mmeo kwamba umeamua kuondoa tofauti zenu ili muanze upya. Na baada ya hapo onesha upendo wa dhati siyo wa kuigiza dhidi ya mmeo na nduguze pasipo kujalisha matatizo na mapungufu yao.
Pia keti na ongea na wifi na shemeji uwaambie nia yako ya kuishi pamoja kwa upendo na amani. Onyesha kutambua hali iliyokuwepo ya nyote kutopendana na kwamba hujaona manufaa yake ndo maana umeamua muondoe tofauti zenu. Eleza kwa uwazi wapi walipokuwa wanakukwaza na pia wape nafasi ya kueleza ulipowakwaza pia.
Muhimu, hao ni wapitaji. wewe, wanao na mmeo ndo wa kudumu pale. Hata wasipofanya kazi sawa we fanya kwani hapo ni kwako na kazi ni zakwako, jua ni suala la muda tu wataondoka na kukupisha. Acha chuki, puuza yote hata kama wakifanya kituko cha makusudi usigadhabike, hilo ndo lengo lao kukuudhi ili ufanye makosa na hivyo ujifunge bao la ushindi kwao.
Usiwape hiyo nafasi. Nimeandika haya kuongea na wewe na haina maana kuwa sijayaona maumivu yako. Samehe bure tena hata kabla ya kukosewa kwa vile kukosewa kupo tu upende usipende.
Mungu na akujalie hekima, busara na ustahimilivu katika haya mazingira magumu unayopitia.
I.......
Kwakeli dada kazi unayo unayo. Isingekua kiapo cha ndoa ningesema utoke hapo kwa mme wako na mwanao ukajitegemee kama unajiweza kwa masharti kua kurudi ni mpak Awatoe hao ndugu zake.
Ila kingine kama utaweza mshauri mumeo awatafutie ndugu zake kazi au biashara halafu iwe mbali na hapi home kwenu itapunguza ujinga wanaoufany Na wataanza kua busy na maisha yao.
Kingine mwambie dada wa kazi afanye kazi zinazo mhusu tu, maswala ya kuwaulia nguo zao aache na ww ingilia kati, usikubali wafuliwe nguo na dada wa kazi. Majukumu yao wafanye wenyewe.
Kwa sababu Mume yupo upande wao usipeleke mashitaka kwa mme wako tena Waache tu, na kwa vile hawakuheshimu na wala hawaoni umuhimu wako na ww toa umuhimu wao kwako usiwategemee kwa chochote kile, pia punguza huduma unazojitole Kwao kama sio kuacha kuwahudumia kabisa, isipokua chakula tu ambacho anatoa kaka yao. Pia hakikisha mahitaji yao yanatoka kwa kaka yao tu. Usitumie pesa yako kwao, lazima wataanza kuona tofauti.
Usijishushie thamani kisa mume ambae anamwanamke mwingine ambae anampa furaha, maumivu ni yako hakuna cha kuhofia hapo, mume mwambie ukweli kua kuanzia sasa ahudumie mwenyewe ndugu zake kama hawatakubali kukusikiliza mama wa nyumba na kama hata kubali kukusikiliza basi awahudumie yeye.
Jukumu lako lipo kwa mume wako, hao ndugu zake ni huruma zako mwenyewe ambazo mwisho wa siku unaishia kuwalaumu kwa ujinga wako (am very sory kwa kusema ujinga wako) ila unaonekana mjinga kwa kua upo concerned kwao. Acha kua concerned sana kwao usijitolee hakikisha wanakula tu, inatosha hayo mengine usishughulike nayo. Nadisitiza mwambie dada wa kazi asiwafanyie chochote kile akatae kabisa na wala asiogope.
Nb: kitu ambacho hukijui ni kua sisi wanaume huwa tunapata wakati mgumu kuamua nani nimsikilize kati ya mke niliyekutana nae ujanani na ndugu zangu nilikua nao na mama yangu mzazi aliye nizaa. Nafsi zetu zinashikwa sana na mama zetu na ndugu zetu hasa wa kike. Hivyo unatakiwa kua na msimamo imara usiyumbe watakuelewa, au waamue kuondoka au kubaki.
Kama watabaki badi wakusikilize na wafanye yale unataka kana hawataki watoke tu.