Ndugai fanya hivi kulinda heshima ya bunge

East African

JF-Expert Member
Nov 27, 2013
704
989
Habari za siku wadau wa jf
Bunge ni chombo huru na linapaswa kulindwa ili kiwe na nguvu ya kutetea maslahi ya wananchi na taifa bila kujali vyama vyao. Kiongozi Mkuu wa chombo hiki ni Spika akisaidiwa na Naibu Spika, ambapo kazi ya kiongozi wa Bunge ni kuwaongoza wabunge bila kujali vyama vyao.

Vyama ni kama njia tu ya kuwafikisha pale Bungeni hivyo ni vyema kuongoza chombo hiki kwa maslahi ya taifa lote. Kutokana na sintofahamu na mgongano unaoendelea kujitikeza ningemshauri ndugu Spika Ngugai akae chini na uongozi wa Bunge na kutafuta suluhu ili chombo hiki kiendelee kuaminiwa kama ilivyokuwa enzi ya Sita na Makinda ambao angalau wabunge walikuwa wanaongea na kutoa maelekezo kwa serikali kwa pamoja.

Kama Kiongozi wa Bunge unatakiwa uhakikishe unarekebisha tofauti hizo la sivyo hata wewe hutapenda kuona unaongoza chombo ambacho hakina maelewano. Najua kuna watu wengine wangependa kushabikia kuadhibiwa kwa wapinzani. Lakini wewe kama kiongozi hakikisha Bunge linakuwa moja wakati wote ili liweze kusimamia serikali.

Nimeona nilete ushauri huu moja kwa moja kwako kwa kuwa huyu msaidizi wako hataki na wala hatakubali kutafuta suluhu kwa kuwa yeye ndio katibua hali ya hewa.

Inawezekana CCM wakapenda hali hii iendelee ili kuwakomoa wapinzani ila mimi nakushauri itisha kikao cha uongozi wa Bunge au uunde kamati ya maridhiano kama ilivyokuwepo kwenye Bunge la katiba.

Mwisho, natambua kuwa sheria za Bunge zipo ila sio kila jambo utatumia sheria. Mambo mengine ni busara inaweza kuamua na maisha yakaenda. Nakumbuka enzi za kina Sita na Makinda sio kweli kuwa hawakuwa wanafuata sheria bali busara ilitumika na ndio maana masuala mazito yaliweza kujadiliwa kwa mapana.

Lakini kwa kufuata sheria bila busara sifikirii kama masuala mazito yanaweza kupewa nafasi na kujadiliwa Bungeni hasa yale machungu kwa serikali. Maana ili mbunge alete hoja atatakiwa alete ushahidi kamili kitu ambacho hata huo ushahidi utaambiwa umeiba nyaraka za serikali.
 
Habari za siku wadau wa jf
Bunge ni chombo huru na linapaswa kulindwa ili kiwe na nguvu ya kutetea maslahi ya wananchi na taifa bila kujali vyama vyao. Kiongozi Mkuu wa chombo hiki ni Spika akisaidiwa na Naibu Spika, ambapo kazi ya kiongozi wa Bunge ni kuwaongoza wabunge bila kujali vyama vyao.

Vyama ni kama njia tu ya kuwafikisha pale Bungeni hivyo ni vyema kuongoza chombo hiki kwa maslahi ya taifa lote. Kutokana na sintofahamu na mgongano unaoendelea kujitikeza ningemshauri ndugu Spika Ngugai akae chini na uongozi wa Bunge na kutafuta suluhu ili chombo hiki kiendelee kuaminiwa kama ilivyokuwa enzi ya Sita na Makinda ambao angalau wabunge walikuwa wanaongea na kutoa maelekezo kwa serikali kwa pamoja.

Kama Kiongozi wa Bunge unatakiwa uhakikishe unarekebisha tofauti hizo la sivyo hata wewe hutapenda kuona unaongoza chombo ambacho hakina maelewano. Najua kuna watu wengine wangependa kushabikia kuadhibiwa kwa wapinzani. Lakini wewe kama kiongozi hakikisha Bunge linakuwa moja wakati wote ili liweze kusimamia serikali.

Nimeona nilete ushauri huu moja kwa moja kwako kwa kuwa huyu msaidizi wako hataki na wala hatakubali kutafuta suluhu kwa kuwa yeye ndio katibua hali ya hewa.

Inawezekana CCM wakapenda hali hii iendelee ili kuwakomoa wapinzani ila mimi nakushauri itisha kikao cha uongozi wa Bunge au uunde kamati ya maridhiano kama ilivyokuwepo kwenye Bunge la katiba.

Mwisho, natambua kuwa sheria za Bunge zipo ila sio kila jambo utatumia sheria. Mambo mengine ni busara inaweza kuamua na maisha yakaenda. Nakumbuka enzi za kina Sita na Makinda sio kweli kuwa hawakuwa wanafuata sheria bali busara ilitumika na ndio maana masuala mazito yaliweza kujadiliwa kwa mapana.

Lakini kwa kufuata sheria bila busara sifikirii kama masuala mazito yanaweza kupewa nafasi na kujadiliwa Bungeni hasa yale machungu kwa serikali. Maana ili mbunge alete hoja atatakiwa alete ushahidi kamili kitu ambacho hata huo ushahidi utaambiwa umeiba nyaraka za serikali.


Kwa nini wao Wabunge wa ukawa wasimkubali NS? Kwa nini unataka mapendekezo ya ukawa ndiyo yasikilizwe na siyo ya CCM?
 
Tunakushukuru kwa kutambua kuwa kuna mtu amekosa hekima na busara
 
Habari za siku wadau wa jf
Bunge ni chombo huru na linapaswa kulindwa ili kiwe na nguvu ya kutetea maslahi ya wananchi na taifa bila kujali vyama vyao. Kiongozi Mkuu wa chombo hiki ni Spika akisaidiwa na Naibu Spika, ambapo kazi ya kiongozi wa Bunge ni kuwaongoza wabunge bila kujali vyama vyao.

Vyama ni kama njia tu ya kuwafikisha pale Bungeni hivyo ni vyema kuongoza chombo hiki kwa maslahi ya taifa lote. Kutokana na sintofahamu na mgongano unaoendelea kujitikeza ningemshauri ndugu Spika Ngugai akae chini na uongozi wa Bunge na kutafuta suluhu ili chombo hiki kiendelee kuaminiwa kama ilivyokuwa enzi ya Sita na Makinda ambao angalau wabunge walikuwa wanaongea na kutoa maelekezo kwa serikali kwa pamoja.

Kama Kiongozi wa Bunge unatakiwa uhakikishe unarekebisha tofauti hizo la sivyo hata wewe hutapenda kuona unaongoza chombo ambacho hakina maelewano. Najua kuna watu wengine wangependa kushabikia kuadhibiwa kwa wapinzani. Lakini wewe kama kiongozi hakikisha Bunge linakuwa moja wakati wote ili liweze kusimamia serikali.

Nimeona nilete ushauri huu moja kwa moja kwako kwa kuwa huyu msaidizi wako hataki na wala hatakubali kutafuta suluhu kwa kuwa yeye ndio katibua hali ya hewa.

Inawezekana CCM wakapenda hali hii iendelee ili kuwakomoa wapinzani ila mimi nakushauri itisha kikao cha uongozi wa Bunge au uunde kamati ya maridhiano kama ilivyokuwepo kwenye Bunge la katiba.

Mwisho, natambua kuwa sheria za Bunge zipo ila sio kila jambo utatumia sheria. Mambo mengine ni busara inaweza kuamua na maisha yakaenda. Nakumbuka enzi za kina Sita na Makinda sio kweli kuwa hawakuwa wanafuata sheria bali busara ilitumika na ndio maana masuala mazito yaliweza kujadiliwa kwa mapana.

Lakini kwa kufuata sheria bila busara sifikirii kama masuala mazito yanaweza kupewa nafasi na kujadiliwa Bungeni hasa yale machungu kwa serikali. Maana ili mbunge alete hoja atatakiwa alete ushahidi kamili kitu ambacho hata huo ushahidi utaambiwa umeiba nyaraka za serikali.
Busara aliitumia sana Lowassa lkn mwishowe akaambulia kuwa Garasa...Aliitumia sana tena sana Kikwete hata kumuwajibisha mtu alikuwa anamuomba/anambembeleza...lkn tulichoambulia muulize yeyote anajua..hata Mbowe..sugu...Mnyika...Msigwa wanajua....
KUMBE HUTAKIWI KUSAHAU KUWA BUSARA KUU PEKEE KATIKA NCHI SIKU ZOTE NA ITAENDELEA KUWA ZILE SHERIA MLIZOJIWEKEA...HIYO NDIYO BUSARA KUU NA PEKEE YA KUTUMIA KTK KUONGOZA...
Pole kijana..ni bahati mbaya kuwa enzi za Makinda za kumuita Lissu (Mwanangu Lissu hebu tusaidie hapa!!!!!!) ZIMEISHA....Kwa sasa yeye anapwaya..kumbe roho isikuume..muhimu
Tune yourself to the new move!!!!!!
 
Sawa huo ni ushauri mzuri. Lakini je bwana Job mwenyewe yuko wapi? Si tuliambiwa kwenda kupinga anya yake? Ni muda gani umekwenda? Nina u hakika atarudi? Unakumbuka lile bunge lililopita? Wskati wa ile kashifa ya ninihii. So alipotea mpk bunge likafungwa?
 
Ee Mwenyezi Mungu mjalie afya njema spika wetu. Ili arudi kuwatumikia watanzania bila kujali itikadi. Bado tunazihitaji busara na hekima zake za kuheshimu hata maoni ya upande Wa upinzani kwani woote sisi ndiyo tuliwachagua.
 
Naamini amekubali kufanya maridhiano, hicho ni kitu kizuri sana.
There is a reason behind...chui ni chui tu....mkururo kati yake na naibu wake ni faida ya upinzani(chadema)
Yeye kama binadamu mwingine yeyote ana roho anapenda kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake......
Yeyote anaweza kujisikia vibaya kwenye ofisi kama kapewa cheo lakini aliye chini yake awe na nguvu na ushawishi kwa boss wao kuliko yeye
 
Back
Top Bottom