Sir M.D.Andrew
JF-Expert Member
- Jul 30, 2012
- 201
- 37
Ndugu wana jf,nimefuatilia kwa makini vyombo vya habari siku ya leo ambapo masikio ya wengi yameelekea dodoma kikao cha bunge kuanza! Lakini kabla sijafika mbali naomba nieleweke kuwa katika nchi kuna mihimili mitatu yaani bunge,mahakama na serikali,lengo lake ni kila mhimili usimamie mhimili mwingine kwa maana ya checks and balance.Kazi ya bunge ni kuisimamia serikali,lakini tofauti na dhana hii leo naibu spika bwana ndugai kasema kuwa: Bajeti ya mwaka huu ni nzuri,imelenga kuwaletea maendeleo wananchi wote na kwamba wananchi waendelee kuiamini serikali yao ili itimize malengo yake,bajeti hii ni nzuri na haina sababu ya kutiliwa mashaka,na amekwenda mbali zaidi kwa kuwatoa wasiwasi wananchi kuwa vurugu bungeni hazitakuwepo sababu serikali imekuja na bajeti nzuri yenye kukidhi haja ya mtu mmoja mmoja,hakuishia hapo,pia akawaasa wabunge kufuata kanuni za bunge ili kuepusha mgongano bungeni utakaosababisha wananchi kudharau bunge lao: Hoja yangu ya msingi hapa ni kwanini ndugai kaisemea serikali? Maneno haya yangepaswa kusemwa na waziri mkuu ili bunge li prove,je spika na naibu spika ni sehemu ya serikali? Au bunge linaweza kukaa kama serikali hivyo kujijadili lenyewe na kujisahihisha lenyewe? Jamani kwa akili zangu nahisi bunge limeanza vikao vyake kukiwa na kasoro,ndugai si msemaji wa serikali,hakupaswa kusema hivyo! Nawasilisha.