Pole sana kijana, kwanza inakupasa kuamini kwamba kuna ulimwengu usioonekana kwa macho ya damu ya nyama (Ulimwengu wa roho) ulimwengu huu unatumiwa na falme mbili za Shetani Na Mungu na kupambana katika ulimwengu wa roho kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na ndoto. Mara nyingi Mungu anatumia njia hii kuongea na wanadamu kwa kuwajulisha kufanya jambo fln kwa jinsi atavyoona pia shetani anatumia ndoto kudhuru wanadamu,,,,,kwa mfano unaweza kuota unalishwa au kula nyama Na kweli ukiamka unajikuta umeshiba na huna hamu na chakula. Kwa ufupi niseme kwamba ndoto yako ina maanisha kwamba kuna nguvu isiyoonekana kwa macho inapambana na wewe aidha kukurudisha nyuma inaweza ni uchumi, afya, elimu nk. Naamini ni kweli kwamba kuna baadhi ya mambo ambayo unafany hayakamiliki kwa wkati unataka wewe, kwahiyo hiyo nguvu inajitahidu sana kukukwamisha mambo yako. Sasa basi acha kudharau ndoto inaonesha kitu halisi kilichotokea nyuma au kitatokea baadae.
Siku nyingine nikipata muda nitaeleza kwa kina kuhusu ndoto na madhara yake pamoja na siri ya ulimwengu wa roho!