Ndoto hii imenifikirisha siku nzima

kabon14

JF-Expert Member
Jun 14, 2016
1,233
867
Wakuu naombeni msaada wa tafsiri ya ndoto hii, jana nimeota kuwa nipo maeneo fulani nimevaa gwanda za FFU ghafla nkakutana na askari kibao wametanda barabaran njiapanda hivi wakiwa kama wanasaka kitu fulani (kwa walioko Dodoma ni pale ilipo Airtel shop)

Kutokana na hofu nilishtukiwa na afande mmoja akaniuliza kitu ambacho sikumbuki ni nini, nikamuita pembeni nikamwambia bro naomba unisamehe na usiwaambie wenzako please, naomba unitoe eneo hili akakubali.

Tukiwa njiani kuelekea kusikojulikana tukakutana na askari wengine wengi sana wakiwa kwenye paredi, jamaa yaonekana alikuwa mkubwa alipokaribia akawaamulisha wakafungua mguu (mguu pande), nikiwa katika hofu sana nilitembea kwa kutetemeka hadi nikasikia minong'ono miongoni mwa askari waliokuwa pale.

Tulifika sehemu inayoonekana kuwa ni nje ya mji kwenye mashamba ya watu, niliwaona jamaa fulani wanalima tuliwasemesha (sikumbiki tuliwasemesha nini) tukakatiza katikati ya mashamba kutafta njia, mbele kulikuwa kama na korongo fulani lililotuzuia kupita, tukapinda kulia hivi, kulikuwa na nyumba fulani ndogo hivi inayoonekana ubavuni, kwa mbele kulionekana barabara ya lami na magari yalionekana kupita.

Yule Askali akaniambia sasa tafuta barabara inayoelekea Babati au Arusha urudi, nilishangaa sana kwanini jamaa kanifikisha mbali hvo na sijui narudi vipi Dodoma maana sikuwa hata na mia mfukoni.

Wakati na tafakari jamaa sikuona alipopotelea ghafla wakaja mabinti wawili ninaowafahamu, ambao sikuwa na wazo la kujiuliza wametokea wapi kwa sababu tulikuwa pembeni ya nyumba ile.

Basi wakanisemesha (sikumbiki tuliwasemeshana nini), dada mmoja akaniambia kuwa anapenda shati langu huku akilishikashika, ghafla nikagundua sijavaa gwanda za FFU tena bali ni nguo fulani kama rangi ya maziwa hivi.

Wakati akishika shati langu nikagundua kuna maandishi mengi sana kwenye suruali yangu mguu wa kulia yaliyoandikwa kwa kalamu ya wino.

Nilishangaa sana na kujiuliza yametoka wapi, baada ya kuchunguza vizuri nikagundua sio maandishi bali ni namba nyingi sana zimeandikwa na kutengeneza kama umbo la mraba hivi.

Niliangalia kwa umakini nikaona kuna namba tatu zimeandikwa kwa wino mwekundu ambazo ni 1, 3, na 7 halafu kuna moja ya mwsho iliandikwa kwa wino wa blue kama zingine ila naikumbuka kwa sababu ilikuwa ni ya mwsho upande wa chini kulia mwa umbo lile la mraba na ilikuwa haijaandikwa kikamilifu na ilikuwa kubwa kuliko zote, nayo ni namba 8 (iliandikwa as if mwandishi alikuwa na speed kubwa hivyo haikufungwa vizuri upande wa juu kulia).

Baada ya hapo nilishtuka toka usingizini.

Naombeni mchongo wa mawazo yenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndoto ni kumbukumbu tu za ubongo unapokuwa umepumzika juu ya mambo uliyowahi kutenda, kuyafikiria ama imaginations tu.
 
Ulikula nini kabla ya kulala..?
Usije kutusumbua hapa kumbe ulikula chakula kigumu lzm uote ndoto za ajabu!!

Halafu mnaotaje ndoto za namna hiyo wkt Mimi huwa naota ndoto za aina mbili tu,nipo nazini au napigana na huwa sipigwi hata ngumi moja😂 ningekuwa mimi ndo wewe kwenye hiyo ndoto ningepiga hao ffu vibaya mno hlf mwishoni hao binti uliowaona mmoja wapo ningeimalizia ndoto kwa kuzini.. ndoto zangu huwa zina happy ending ya namna hiyo!... Wewe ulikwama wapi mkuu..?
 
Kipande cha kwanza, utakuwa na boss wako atakuamini na kukutetea hata pale utakapokosea. Atakuongoza lakini mwishoni utaondoka sehem uliopo kwa misukosuko na baadae utaenda sehem nyingine usiyofaham. Hutakuwa maarufu tena eneo la shughuli yako. Tafsiri itaendelea....
 
Mbona haina maajabu.maana ina kachumbali za ajabu ajabu kama ndoto nyingine tu.

Ndoto yenye ujumbe spesheli huwa imenyooka,na hueleweka pia.
 
Ndoto ni kumbukumbu tu za ubongo unapokuwa umepumzika juu ya mambo uliyowahi kutenda, kuyafikiria ama imaginations tu.

Zipo ndoto ambazo hutokana na mawazo ambayo mtu alikuwa nayo nyakati fulani. Ndoto za namna hii hazina maana yoyote kwa maisha ya mwanadamu. Lakini kuna ndoto ambazo sio mawazo ya siku za nyuma, ni kitu kipya kabisa, ndoto za namna hii sio za kupuuzia, kiulimwengu wa roho, haya ni maono. Wapo watu wenye vipaji vya kutafsiri ndoto za aina hii. Farao (mtawala wa Misri), aliota ndoto mbili usiku mmoja na kwa nyakati tofauti (kila ndoto na wakati wake ndani ya usiku mmoja), alipoletwa Yosefu kutafsiri, siku za usoni mambo yalitokea kama ilivyotafsiriwa. Na ndoto zote mbili za Farao zilimaanisha kitu kimoja; miaka saba ya neema na miaka saba ya njaa. Hivyo tuwe makini na baadhi ya ndoto tunazoota.
 
hahahaha unazingua mkuu
Ulikula nini kabla ya kulala..?
Usije kutusumbua hapa kumbe ulikula chakula kigumu lzm uote ndoto za ajabu!!

Halafu mnaotaje ndoto za namna hiyo wkt Mimi huwa naota ndoto za aina mbili tu,nipo nazini au napigana na huwa sipigwi hata ngumi moja ningekuwa mimi ndo wewe kwenye hiyo ndoto ningepiga hao ffu vibaya mno hlf mwishoni hao binti uliowaona mmoja wapo ningeimalizia ndoto kwa kuzini.. ndoto zangu huwa zina happy ending ya namna hiyo!... Wewe ulikwama wapi mkuu..?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ndoto ilikuwa ndefu kweli lkn ktk uhalisia unaweza kukuta ulitumia sekunde 10 tu kuota😅
 
Kipande cha kwanza, utakuwa na boss wako atakuamini na kukutetea hata pale utakapokosea. Atakuongoza lakini mwishoni utaondoka sehem uliopo kwa misukosuko na baadae utaenda sehem nyingine usiyofaham. Hutakuwa maarufu tena eneo la shughuli yako. Tafsiri itaendelea....
Aje pm na elfu hamsini kwa msaafa zaidi ha ha ha.... Acha kumtisha dogo, NDOTO ICHUKULIWE KAMA NDOTO TU!.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom