Mkuu ondoa shaka ya usaliti kwa mkeo,
Hali hiyo huwa inatokea kwa wanandoa na msipokuwa makini mnaweza kuivunja ndoa yenu takatifu,
Mkeo anamsongo wa mawazo, ni tatizo la kisaikolojia linalomfanya mwanandoa kukosa hamu ya tendo la ndoa,
Njia ya kubadili hali hiyo ni lazima uwe mbunifu mkuu,
Kwanza anza wewe kubadilika kwakubadili aina ya maisha unayoishi,
Unaweza siku ukaamua mtoke out jioni ambako mtakula chakula huko huko, mnaweza siku mkaamua mje beach kigamboni kwetu kama mpo dar,
Mnaweza kuamua mfano krismasi inakaribia muende mikumi nk,
Pia badili staili ya kuomba tendo la ndoa, usitumie kauli bali lugha ya mwili na vitendo tu,
Jaribu kubuni maeneo mapya ya kufanyia mapenzi kama vile jikoni, bustanini, bafuni, kwenye banda lakuku nk, lakini zingatia watoto wasione,
Na mwisho badika lugha yako ya kimahaba, mkeo keshaichoka, we umeng'ang'ania swaga zilezile za kipindi unamtongozo mpaka leo mna watoto wawili?
Ukipanga vizuri hayo nakuhakikishia utaona penzi jipya,
Zingatia lugha ya kumtoa nyoka pangoni kwamkeo ni kila sekunde itumike, sio lugha za mkato na za ukali