Ndoa nyingi zimevunjika.....inasikitisha!

Ndoa nyingi zimevunjika.....inasikitisha!

Von Mo

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2012
Posts
1,819
Reaction score
1,187
Mambo vipi watu wangu wa ukweli! Hope mko poa, kwanza nitoe shukrani kwa Best wishes za Birthday yangu, Mungu awabariki sana! Back to the topic: Ndoa nyingi zimevunjika, yaani wanawake wengi walio ktk ndoa hawapati haki zao kutoka kwa wenzi wao, unakuta anasema me miezi sita, mwingine miaka miwili, kimsingi mahusiano kati ya mume na mke hayapo kinachowaunganisha ni watoto tu kwa vile bado wanataka malezi, kinachosikitisha ni kuona mzazi moja hawajibiki anamwachia mwenzie mzigo hadi anaelemewa ndiyo mwanzo wa mwanaume suruali...n.k Na hizi ndiyo sababu kubwa za akina mama kuwa na Serengeti Boyz na akina Baba kutembea na Vibinti vidogo, ukiachana na zingine. ushauri wangu wewe uliye ktk ndoa Muombe sana Mungu ndoa yako iwe na amani, lakini tusipende walivyo navyo bali wao walivyo both men and women,
 
Mke mwenye busara mtu hupewa na Bwana" (Mithali 18:22; 19:14).
Mwanamke wa siku hizi (my opinion) hawana busara, unakuta kama umerudi home unakuta kanuna tu au ukimsemesha kama umechelewa toka kwenye mishemishe zako hata kama ulimpa taarifa ni kununa tu. Yaani kimsingi hawaeleweki kabisa.
Anaweza zua ugomvi tu na hausigeli na kutaka afukuzwe kisa kakua wala hawezi kutafakari kuwa ni kwa bahati mbaya tu huyo mtoto alikosa labda mtu wakumsomesha angekuwa shuleni wakati huo. wageni wa ukweni kwake anaweza kuwapa kipaumbele zaidi kuliko wako. Kama mmeshafunga ndoa (kwa wakristo) basi anakuwa na comfidence ya destruction yaani anaweza kukuambia chochote kwa maana mmeshafunga ndoa, ukiwa hali ya uchumi imeyumba kidogo basi maneno hayaishi,sijui anaweza kukuambia na wewe unaweza kujiita mwanaume? Sasa mambo kama haya ni mabaya na ni chanzo cha kuzalisha nyumba ndogo (my opinion). Sasa cha ajabu wale wanaume wababe na maplay boy wake zao heshima mbele na kama akiwa na mihela ndio usiseme. Logically ina maana ukiwa honest kwake analipa mabaya! Hivini kwanini? Maandiko yanasema umepata kilicho chema sasa kimegeuka kibaya why? Kaunga and Passion Lady like this.




Mambo vipi watu wangu wa ukweli! Hope mko poa, kwanza nitoe shukrani kwa Best wishes za Birthday yangu, Mungu awabariki sana! Back to the topic: Ndoa nyingi zimevunjika, yaani wanawake wengi walio ktk ndoa hawapati haki zao kutoka kwa wenzi wao, unakuta anasema me miezi sita, mwingine miaka miwili, kimsingi mahusiano kati ya mume na mke hayapo kinachowaunganisha ni watoto tu kwa vile bado wanataka malezi, kinachosikitisha ni kuona mzazi moja hawajibiki anamwachia mwenzie mzigo hadi anaelemewa ndiyo mwanzo wa mwanaume suruali...n.k Na hizi ndiyo sababu kubwa za akina mama kuwa na Serengeti Boyz na akina Baba kutembea na Vibinti vidogo, ukiachana na zingine. ushauri wangu wewe uliye ktk ndoa Muombe sana Mungu ndoa yako iwe na amani, lakini tusipende walivyo navyo bali wao walivyo both men and women,
 
37753image002_39768_37753_1.jpg
 
wanamaudhi sana wake zetu..hawatumiki,hawaambiliki..wamejisahau....wao ni iPad, TV ,Simu,....baaaasi....yaani hawajali kama kuna mme au nini ingawa mume ndio kila kitu pale nyumbani....hawaeleweki kabisa!!!! inabidi tuishi nao tu kwa mapenzi tu ya mungu !!!! mi nimeshasahau kupikiwa,kufuliwa, kuwekewa maji, kuwa cared for nk..ingawa najitahidi kufanya ninayopaswa kufanya!!!
 
suluhisho kuwa na ndoa za mikataba
kila mtu atawajibika kwa mwenzake ili baadae waweze kujiongezea mkataba
lakini hii ya hadi kifo kiwatenganishe na hii silika ya wanaume wa kibongo kujiona ni miungu watu
kila kitu afanye mwanamke ndio husababbisha mabishano,kutokuelewana,kusalitiana nk.
shtuka, chukua hatua.
 
Wengi sana hatujui....na hata kama tunajua...tunasahau! NINI hasa unachokitaka katika mahusiano? na je unakipata?
Ni kweli kuna mambo mengi lakini ukiacha hayo......kuna hili la "sexual satisfaction" je unaridhika??
Mfano: Unakuta mtu mke wake kibonge halafu katika kupiga stori anakwambia huwa anapenda sana "vimodo" kuna usalama hapo?
Kwa ninavyoona mimi tatizo ambalo linaweza kuwa kubwa sana ni mawasilino mabovu katika mahusiano....! mume au mke unashindwa kumwambia mwenzi wako unataka nini....lakini je, yuko tayari kukupa?
Wamama wanapenda serengeti boys pengine sababu ni wepesi na wanapunzi
Na wababa nao wanapenda vibinti pengine sababu ni wepesi wa kutoa "service"

Wanaume vitambi vinasumbua sana, kitambi karibia kilo kumi...kitandani patakuaje? halafu cha ajabu mke anapenda mme wake awe na kitambi then kitandani baada ya sekunde tu mtu hoi....zinaanza lawama! mwe...
 
Ndo maana unashauriwa usimuoe mtu eti kwa kua ni mrembo... uremno unaishaga tuu na mapenzi yanapungua...
Mi naona cha muhimu ni kuoa mtu sahihi na uevaluate thamani yake ata after 10 yrs..
 
Wa bahati mbaya swala la maisha ya ndoa hua hatulichukulii uzito hasa tunapokua vijana. Mara nyingi tunachanganya love na emotions. Na wakati mwingine hata huwa hatujiulizi je ni ndoa ya namna gani naitaka. Huwa tunabase sana kwenye maumbile na uwezo kifedha n.k. Tunasau kua ndoa ni lifetime commitment na ni sehemu utakayoishi muda mwingi kuliko nyumbani kwenu.
Pia huwa tunaharakisha sana kufanya maamuzi sijui ni kisasi au sijui nini hasa unapokua broken hearted hapa wengi huamua kuoa choice B, huku akiwa bado anampenda his/her first choice ambayo haikuworkout. Kwa makosa hayo ndio maana unakuta ndoa inakua chungu na wengine wamita ndoa ndoano which is not true kwanini uingie kwenye kitanzi ilhali tu uoe au uolewe. Ukimuomba Mungu na kuwa na imge ya ndoa yako unavyotaka iwe utafanikiwa sio mbo gumu.
 
wanamaudhi sana wake zetu..hawatumiki,hawaambiliki..wamejisahau....wao ni iPad, TV ,Simu,....baaaasi....yaani hawajali kama kuna mme au nini ingawa mume ndio kila kitu pale nyumbani....hawaeleweki kabisa!!!! inabidi tuishi nao tu kwa mapenzi tu ya mungu !!!! mi nimeshasahau kupikiwa,kufuliwa, kuwekewa maji, kuwa cared for nk..ingawa najitahidi kufanya ninayopaswa kufanya!!!

Tunaishi kwa mazoea zaidi si upendo kama ilivyokuwa awali.
 
wanamaudhi sana wake zetu..hawatumiki,hawaambiliki..wamejisahau....wao ni iPad, TV ,Simu,....baaaasi....yaani hawajali kama kuna mme au nini ingawa mume ndio kila kitu pale nyumbani....hawaeleweki kabisa!!!! inabidi tuishi nao tu kwa mapenzi tu ya mungu !!!! mi nimeshasahau kupikiwa,kufuliwa, kuwekewa maji, kuwa cared for nk..ingawa najitahidi kufanya ninayopaswa kufanya!!!

Kaka pole sana...............Tafadhali usizoee maudhi........vunja ukimya. Ongea na mwenzako kwa upole, mwuliza wapi mlipopoteza link kutoka mlivyokuwa wapenzi/ wachumba....mweleze kiu yako nini unatamani, na yeye akueleze nini anatamani. Tafuteni convegence point. Unawezakuta yeye anakufanyia hayo kwa kuwa nae anayo madai yake ambayo anaona hayatimizwi vema na wewe. Hiyo ya wewe kujitahidi kufanya unayopaswa kuyafanya kama mume.hakikisha kuwa mnayajadili na kudefine ni yepi unapaswa kuyafanya na mkubaliane, unawezakuta wewe unachokiona unajitahidi kufanya kama majukumu yako kama mume kwa tafsiri ya mkeni hayo ni majukumu ambayo yanapaswa kufanywa na mtu mwingine kabisa, wewe kama mumewe anahitaji mambo mengine kabisa. So inategemea hayo unayosema unahitajika kuyafanya ni nani anayadefine??

Mfano: Wewe unawezakudefine kuwa kama mumewe ili kuonyesha kuwa unamjali mkeo basi ni kwa wewe kwenda garage kila jumamosi kuliservice gari la mkeo na kulijaza mafuta ya wiki nzima....................but yeye kama yeye anatamani kuwa na mume ambaye kila jumamosi atakaa au kutoka nae kama mtu na mkewe na kujadili mapenzi yao. Wote mko right but ni nani na kwa jinsi gani anapaswa kudefine hizo priorities.

Mwingine anasema mimi kama mume ninahakikisha kuwa mezani kuna chakula kila siku, sawa ni vizuri na unaonyesha unajali, but mkeo hakutoka kwao kuja kula chakula nyumbani kwako kama humpi nafasi ya kukaa nae, kama wapenzi.
 
daah! pole sana wewe unayejuta kuwa ktk ndoa fanya Maombi juu ya ndoa yako, na wewe uliye single kama mimi mwambie Mungu haja ya moyo wako, na wewe uliye na mchumba Mwombe Mungu amtengeneze ili mfanane
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom