Ndoa ni makubaliano ya watu wawili ya kuishi pamoja kama mke na mume ili kujenga familia. . . . Kinachofanya ndoa idumu ni mambo mengi sana ila lililo la msingi ni kama wanandoa wanamalengo yanayofanana kwenye uhitaji wao kwenye ndoa!
...Ndoa ni muungano kati ya mwanamke na
mwanamume kuishi pamoja kama mume na mke
muda wote wa maisha yao. (Sheria ya ndoa
mwaka 1971 kifungu cha 9).
i) Wanaooana wawe wamekubaliana pasipo
kulazimishwa na mtu.
ii) Ndoa ni ya mwanamke na mwanamume.
iii) Ni ndoa ya kudumu maishani.
...hapo kwenye KUDUMU naomba niparuke...L.O.L...juhudi binafsi zinahitajika...kama ni kwa MUNGU sana,piga goti...kama ni kwa WAGANGA wa kienyeji...wewe tu na imani yako!
NDOA NI KUTOA 1. Ndio sio mkataba wa kijamii bali agano la kiroho. Waefeso 5:31-33 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Siri hiyo ni kubwa, ila mimi nanena habari ya KRISTO na Kanisa.
Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe, wala mke asikose kumstahi mumewe.Hapa tunajifunzai) Ndoa ni fumbo la ajabu la kiroho linalowaunganisha watu wawili, mwanamume na mwanamke (mst.31)ii)
Ndoa ya kikristo inaliganishwa na uhusiano uliopo kati ya KRISTO na Kanisa (mst.32)iii) Mpango wa MUNGU katika ndoa unahitaji upendo wa kujitoa sadaka kama KRISTO anavyofanya kwa Kanisa (mst.33)2. Ndoa ya Kikristo ni kujitoa sio kupokea.
Wafilipi 2:3-4 Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno, bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenzie kuwa bora kuliko nafsi yake mwenyewe. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. Hapa tunajifunza i) Kutokuwa wabinafsi ii) Unyenyekevu
iii) Roho ya kutoa na kujitoa.
Ndoa ni mwanaume kusaini mkataba,
1:Ndiye atakeye mtunza mwanamke na familia yake,hata kama mwanamke ana mshahara kuliko mwanaume.
2:Ni mwisho kwa mwanaume kusaidia familia yake,na ndugu wa mwanume mwisho kumtembelea mwanaume.
3:Hela ikipungua,penzi litapelekwa kwa mtu mwingine na kila ukifika nyumbani tegemea kununiwa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.