kluger
JF-Expert Member
- Jun 16, 2016
- 2,093
- 1,894
Salamu kwenu waungwana,
Nimewahi kusikia huku nchi za watu kuna ndoa au mahusiano ya mkataba.
Kama wewe ni mume au mke unakubaliana na mwenzako kuwa katika mahusiano ya kimapenzi au ndoa kwa muda fulani na kwa malengo kadhaa.
Wapo wanaokubaliana kuishi pamoja kama wapenzi tu bila kufanya mambo yoyote ya maendeleo kwa pamoja.
Wengine ni kwa ajili ya kupata mtoto tu baada ya hapo kila mtu na njia yake.
Ndoa nyingi Tanzania zina matatizo mengi kutokana na tamaduni zetu, ambapo mahusiano na ndugu wengine kama mawifi na wakwe yamekuwa yakileta kila aina ya zahama mbali mbali.
Mfano unaonikera sana ni uhusiano mbovu kati ya mke na ndugu zako wa dhati kama Mama au Dada zako, kwa kweli hali hii inaleta maumivu makubwa sana kwetu sisi wanaume.
Mama ndiye kakulea na kukufundisha taabia njema hadi ukamvutia mkeo, kadhalika Dada zako waliishi na wewe kwa kila aina ya upendo na hata kukupa moyo hadi umeonekana mwanaume bora na kumvutia mkeo.
Lakini mara baada ya ndoa, mke anaanzisha chuki na ndugu zako ambao, mmekuwa toka utoto wenu iwe shida ama njaa, wakija kukusalimu mke anavimba mashavu. Tabia moja ya ajabu sana.
Najua hali hii inawakuta wengi katika mahusiano yenu, nafikiri ifike mahali watu tuanze kuoa au kuwa na mahusiano ya mikataba kwa lengo la kuzaa watoto, thena kila mtu awe na njia yake.
Au hata kuzalisha wanawake ambao hutokutana naye wala kumjua huko mahosipitalini.
Mtoto anapozaliwa kabla hajamtambua Mama yake, unamchukua na kumlea kama wewe mpka anapokuwa mkubwa.
Hili kwa mnaolifahamu, je wapo warembo kwa Tanzania ambao wapo tayari kwa mahusiano haya?
Mfano mzuri ni mchezaji mpira maarufu duniani, Christian Ronaldo, CR7.
Nimewahi kusikia huku nchi za watu kuna ndoa au mahusiano ya mkataba.
Kama wewe ni mume au mke unakubaliana na mwenzako kuwa katika mahusiano ya kimapenzi au ndoa kwa muda fulani na kwa malengo kadhaa.
Wapo wanaokubaliana kuishi pamoja kama wapenzi tu bila kufanya mambo yoyote ya maendeleo kwa pamoja.
Wengine ni kwa ajili ya kupata mtoto tu baada ya hapo kila mtu na njia yake.
Ndoa nyingi Tanzania zina matatizo mengi kutokana na tamaduni zetu, ambapo mahusiano na ndugu wengine kama mawifi na wakwe yamekuwa yakileta kila aina ya zahama mbali mbali.
Mfano unaonikera sana ni uhusiano mbovu kati ya mke na ndugu zako wa dhati kama Mama au Dada zako, kwa kweli hali hii inaleta maumivu makubwa sana kwetu sisi wanaume.
Mama ndiye kakulea na kukufundisha taabia njema hadi ukamvutia mkeo, kadhalika Dada zako waliishi na wewe kwa kila aina ya upendo na hata kukupa moyo hadi umeonekana mwanaume bora na kumvutia mkeo.
Lakini mara baada ya ndoa, mke anaanzisha chuki na ndugu zako ambao, mmekuwa toka utoto wenu iwe shida ama njaa, wakija kukusalimu mke anavimba mashavu. Tabia moja ya ajabu sana.
Najua hali hii inawakuta wengi katika mahusiano yenu, nafikiri ifike mahali watu tuanze kuoa au kuwa na mahusiano ya mikataba kwa lengo la kuzaa watoto, thena kila mtu awe na njia yake.
Au hata kuzalisha wanawake ambao hutokutana naye wala kumjua huko mahosipitalini.
Mtoto anapozaliwa kabla hajamtambua Mama yake, unamchukua na kumlea kama wewe mpka anapokuwa mkubwa.
Hili kwa mnaolifahamu, je wapo warembo kwa Tanzania ambao wapo tayari kwa mahusiano haya?
Mfano mzuri ni mchezaji mpira maarufu duniani, Christian Ronaldo, CR7.