Ndio mapenzi ya kisasa au ananipotezea muda?

Ndio mapenzi ya kisasa au ananipotezea muda?

KATOTY

Member
Joined
Oct 31, 2013
Posts
24
Reaction score
11
Salamu kwa wana jf wote!!

Leo nimekuja na hili,

Nina mpenzi wagu ambaye tumepanga kuoana ndani ya mwaka huu, jamani tunaishi kama kaka na dada, yaan hatufanyi mapenz, mpenz wangu yupo bize sana na kazi na biashara, kwa mtazamo wangu naona kama hanijali kama ninavyomjali mimi, hanisaidii kwa chochote yaani toka tumejuana hata sent tano yake siijui, hana time ya kusema hata aninunulie zawadi even ch..u..p ya elfu moja! Ana gari lakini ila mimi sina cha ajabu nikienda kwake nikishuka kituoni ananiambia chukua tax afu kwa hela yangu sio kwamba atalipia.

Simuelewi maana kama ni hela analipwa mara mbili yangu na biashara anapata laki 6 kwa siku. Zaidi yupo makini sana na simu yake hakubali hata niishike, hata akiingia kuoga sijui anaificha wapi, mara nyingi anachat tukiwa wote nikimuuliza anasema ni watu wa biashara.

Hebu nisaidieni wandugu wenye wapenzi ndivyo mnavyoishi? Naombeni ushauri wenu nin cha kufanya,


Angalizo; yeye sio mchaga.

asanteni,
 
Shake(wa) before use labda jamaa ni ....kibamia!!hiyo condition ni ajabu sana kwa mwanaume u know..
 
Salamu kwa wana jf wote!!

Leo nimekuja na hili,

Nina mpenzi wagu ambaye tumepanga kuoana ndani ya mwaka huu, jamani tunaishi kama kaka na dada, yaan hatufanyi mapenz, mpenz wangu yupo bize sana na kazi na biashara,
Hebu weka mambo wazi kwanza, ina maana hamjawahi kufanya tokea muwe pamoja? au mlikuwa mkifanya, kisha mwenzio akaanza kubadilika.
Weka mambo hadharani kwanza kisha nije na jibu
 
Labda maadili yake hayaruhusu mpaka ndoa. halafu we si unakipato sasa ye anaona alipie tax yanini wakati nawe una mshahara. Mipango ya ndoa inaendeleaje lakini?
 
caring ni kipaji cha mtu kwa jinsi alivyolelewa, huyo sidhani hata kama ana afair nje bali caring hana wala hajui,anajali nafsi yake na mali zake zaidi. ukiweza kuyavumilia hayo go ahead, kwa lugha rahisi ni bahili pia
 
Mmmmmh! Hapo pa kuingia had kwa baf na simu ndo pameanza kuntia mashaka, anyway endelea kumchunguza taratibu na ujarbu kuongea nae kwa upole umwelezee vile unajiskia anapokuwa hivyo
 
bado hujwa wazi sana maana unasema mnaishi kama..... then hukwambia upande taxi ....jiangalie yawezekana kakuona una tatizo na hana hisia nawe. Kwa kawaida wanaume hisia huwa juu sana kwa wapenzi hasa mwanzoni.
huyo jiangalie mlianzaje labda ulianza kuringa akapata mwingine na wewe ukaja baadaye kwa kuchelewa
 
SHABASHI,MULIKA MWIZI,KAA CHONJO,kusoma hujui ata pichaaa heeeee,!!mwaka ndo huu mgusie ile mipango ya ndoa vp usikie atajibu vp,polee!
 
kufanya mapenzi kabla ya ndoa now days is very important, Mungu anisamehe
 
Kama moyo wako bado unamuitaji vumilia tu uone mwisho wake
 
Akhuu huyo simtaki,si ajabu hata mkija kua na familia gharama zote ziwe juu yako,
....hata outing akupelekagi?
 
kufanya mapenzi kabla ya ndoa now days is very important, Mungu anisamehe

Tatizo hapo wengine wanawapa hata ambao hawana mpango wowote wa kuwa nao in the future.
Mwishowe ni mimba na kuzitoa maana we unajua ndie na mwenzio still scanning.
 
Hili swala la mwanaume kuwa bize na simu zake na kuenda nayo kila sehemu hata bafuni liliwahi kunitokea, nikimuuliza nikawa najibiwa eti simu ina confidential information, siku nilipokuja kuibamba na kusoma vilivyomo ndani nilitamani kufa nikajuta kuwafahamu hawa viumbe wanaoitwa wanaume
 
Hiyo trela sinema yenyewe bado. kachunguze S4 yake ina password. Kuna mipicha kapiga na wenzako. na mtu wa aina yake anakutumia tu kwa faida yake. imagine anaongiza midola kibao na hakusaidii unasubiri nini. chapa lapaaaaaa
 
sasa kama mwanaume hakusaidii kwa lolote na wewe unahitaji msaada hata hela ya tax hakupi kwake unafuata nini?
 
Back
Top Bottom