Ndesamburo: CHADEMA ni sawa na Mti wenye Matunda...

Ndesamburo: CHADEMA ni sawa na Mti wenye Matunda...

mihadarati

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
268
Reaction score
74
*Ndesamburo "chadema ni sawa na Mti wenye Matunda"


Mbunge wa Moshi Mjini Philemoni Ndesamburo amesema matatizo yanayokikumba chama cha demokrasia na maendeleo Chadema yanatokana na kundi la watu wachache wenye uchu wa madaraka ambao pia wanatumia na chama cha mapinduzi CCM kukivurga Chama.


Ndesamburo alisema kuwa wanaosababisha hali yote ilivyo sasa ni vijana ambao hawana uchungu na Chadema ,hivyo lazima uongozi uchukue hatua stahiki ya kinidhamu kwa watu kama hao.


Ndesamburo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Kilimanjaro alikuwa akijibu maswali ya wananchi kwenye mikutano yake ndani ya jimbo la Moshi,ambapo wananchi walitaka kusikia kwa Mbunge wao nini hatima ya mzozo unaoendelea ndani ya Chama hicho.


Alisema kuwa Kiongozi yoyote wa chadema ambaye anakubali kuhongwa na kusaliti chama ni msaliti mkubwa,na anahujumu maisha ya watanzania million 45 ambao wanakitegemea chama.


Mwananchi aliyejitambulisha kwa jina moja la Mohamed alitaka kujua hatima ya matatizo anayoyasikia kwenye vyombo vya habari ikihusisha chama na Mbunge wa Kigoma Kaskazini wa Zito Kabwe,pamoja na wanachama wengine Dk Kitilla Mkumbo na Samson Mwigamba ambao tayari wamekwishavuliwa uonachama na kamati kuu ya chama (CC).


Aliwaambia wananchi kuwa lazima uongozi wa chama ufanye maamuzi magumu kwa wanachama na viongozi wengine ambao hawatakuwa hawana nidhamu ndani ya chama na bila kufanya hivyo watajiamulia kufanya kama wanavyotaka.


“Chadema lazima iwe tofauti na vyama vingine kwanza kwa kuwawajibisha wale wote ambao hawatakuwa wana nidhamu ndani ya chama,ili kuweza kuwepo tofauti na kwa sasabu ni chama cha upinzani hatuwezi kuwa kama CCM ambao wanakumbatia mafisadi”Alisema.


Ndesamburo alisema kuwa Chadema kwa sasa ni sawa na mti wenye matunda hivyo CCM haiwezi kuacha kuipiga mawe,lakini itaendelea kupigana na kuhakikisha inafanya vizuri kwa kuwa ni tegemeo la wananchi.
.............................................................................................................................................
 
Alichochungumza Mzee Ndesamburo na miongoni mwa waasisi wa chadema ni kwlei kwani ndani ya chama chochote wasaliti na mamluku hawawezi kukosekana hivyo kinachotakiwa kwa viongozi kuwa makini na kuwachukulia hatua ya hali ya juu maaana chama chochote cha upinzani ambacho kinanguvu kinakumbana na maswahiba mengi sana kutoka chama kilichopo madarakani..
 
CCM mjipange saana.. Mmebambikia kesi nyingi Viongozi na Wanachama wa CDM na kwa bahati mbaya mmechemka zooote..
Na mtambue ya Kwamba CDM iko ndani ya Mioyo ya Watanzania wapenda Mabadiliko na sio nyie wachache wapenda Rushwa na Ufisadi...
 
Chama ni Taasisi , hakiendeshwi kwa umaarufu wa mtu mmoja mmoja. Chama cha siasa sio klabu ya mpira ambayo nguvu yake kubwa ni mashabiki.
Siasa ni sera sio ushabiki. Ikifika pahali watu wakawa mashabiki tu inakuwa haileti maana yeyote.
Uongozi ni Dhamana . Lakini inapofika watu wakajiona Kiongozi ni Chama hapo pana mushkheri.
Mzee Ndesa yupo sahihi ni mtu wa busara.
 
huu upepo ukipoa salama CCM mtafute pa kutokea tuna imani huu upepo mbaya utatulia mda si mrefu NAPE na kufukuza maffisadi ndani ya siku 90,umeishia wapi?chama lazima kichukue maamuzi sahihii kwa mujibu wa taratibu zake walivyo jiwekea
 
Baada ya kuiba bot ndiyo anakuja kisema ufisadi rudisha pesa zetu kwanza

CHADEMA ni pango la wanyang'anyi
 
Baada ya kuiba bot ndiyo anakuja kisema ufisadi rudisha pesa zetu kwanza

CHADEMA ni pango la wanyang'anyi

Km aliiba bot serikali yako ya ccm ilichukua hatua gani acha kupotosha uma.
 
Wakuu,
najitokeza kusema mambo haya ambyo kimsingi naona kama wadau,wanachama na wapenz wa chadema.sijawah kuona tangu mfumo wa vyama vingi vya siasa chama cha upinzani kilichopo imara kama chadema.binafsi naona kuwa mkakat wa ccm kuibomoa chadema imeshindikana kutokana na uimara wa ajabu sana wa chama hiki,wako makini,na zaid sana wapo na Mungu.nikikumbuka mambo mengi ya uongo juu yao,wamepita.
Wasira,mwigulu,nchimbi na hata lukuvi walisema chadema kitakufa kabla ya 2014.lakin chadema chenye hofu na ulinzi wa Mungu kimeweza kupita na kuona mwaka mpya wa 2014,
hakika hakuna chama kingeweza kuhimili moto mkali kama chadema walivyoweza,yote haya ya kina zito kuisalit chama ni mpito ambao hakuna budi kuupitia..hata maandiko yanasema,hakuna mtu asiyepata majaribu na huwez kukomaa kiroho kama hujapitia ktk majarib makali..
Nafurah sana hiki chama kupitia katk moto kama huu,na hakika watakuwa imara kama chuma.
Naona kila dalili kuwa sasa mgogoro umeisha isipokuwa ccm bado wanahangaika kutafuta njia ya kuizma cdm lakin mwisho wa kukwama umekwisha.
Nilishangaa sana ccm kumpa zzk bili 3.8 kumsaidia kushinda vita yake na uongoz wa chadema,niliona watu wakipewa pesa,tshet kwenye kesi ya zito ili ionekane jamaa ana nguvu,zaid utakuta ni maccm na cuf ndo waliopo mbele ya mkakat huo.
Sitaki kuwaambia waache kwa kuwa yupo Mungu atakaepigana nao,atawawezesha wote wanaopingwa na ccm hasa viongoz wa chadema.
Hakika chadema mmekomaa na mzid kufanya kzi ya kuimarisha chama achaneni na kujibizana na kina zito waliopo ccm.
Tuna uchaguz wa madiwani kwa baadhi ya kata,serikali za mitaa,tujikite kwenye hilo,tuwaache maccm waliojivika mavaz na kad za cdm waonekane kuwa wanacdm waendelee kupiga kelele.
Pigen kelele sana lakin mwisho Mungu anajua nan atatawala nchi hii,teken watu,tunyang'anyeni haki zetu,tutalia machozi sana lakin machoz yetu yataenda bure,tutapambana kwa kuwa tunahtaj ukomboz wa nchi hii.
Ifike mahali chadema tuache kuzungumza au kujibizana na maccm.hiz ni njama za kututoa kwenye mjadala wa katba na uchaguz wa serkali za mitaa.
Mungu ibariki tanzania,ibariki chadema,wabariki viongoz wake,wape hekima na busara zaid,ee Mungu chadema hatulip kisasi,kisasi ni juu yako, wanatupinga sana lakin ww Mungu utuwezeshe,na kila anaesoma post hii ajitambue,mbarik kwa kuwa ni mtanzania mwenzetu,hata akipinga usimpige ww Jehova,mpe nguvu na uhai kwa kuwa atashiriki kupiga kura ya kuchagua kiongoz bora.
Na yule alietabir viongoz kufa na wapinzani kupigna,afe kwanza yeye..awe wa ccm au cdm hakuna mtu kufa..
Asanteni
 
Babu kasema, vipi wale wanae wawili wabunge wa viti maalumu! Chama cha familia
 
Watu wengne tunadhan mnaweza kuwa na busara na kuandika vitu vyenye maana, huwezi kuwa tofauti na mtu asiye na akili,unaushahid kuwa zzt kapewa pesa na ccm?
 
haya sasa wenye saccos yao wameanza kujitokeza. zitto njoo huku mama wa vifaranga wameanza kujitokeza.
 
ndesamburo.mtei.mbowe.lema ndio decision makers wa chadema. wana uchungu na saccos yao wako tayari kuua ukiyaingilia maslahi yao.wachagga oyeeee
 
ndesamburo.mtei.mbowe.lema ndio decision makers wa chadema. wana uchungu na saccos yao wako tayari kuua ukiyaingilia maslahi yao.wachagga oyeeee

Kama baba yako alitumia mbinu kama hizo kutaka kuikomoa Chadema akashindwa sembuse wewe mburula!!!
 
Back
Top Bottom