Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,932
- 30,045
Wadau,
Leo tarehe 30/09/2015 jumatano mida fulani hivi ya saa mbili asubuhi niliona Ndege ndogo za kivita kama tatu hivi zikifukuzana kwa kasi kuelekea upande wa magharibi.
Tanzania ni nchi ya amani, na Watanzania tumezoea amani. Videge kama hivi navionaga tu kama kuna maadhimisho fulani, sio siku ya kawaida kama ya leo. Sidhani kama kulikua na matangazo kwa wananchi kua watarusha hizo ndege.
Sijaona kama kuna hatari yeyote ya Vita ijayokuja mpaka hivi videge vianze kupiga jaramba. Zaidi naona pengine viko kisiasa zaidi, labda tunatishana na kuogopeshana makusudi. Inawezekana navyo ni sehemu ya kampeni kwa namna moja ama ingine.
Binafsi nimewaza hivi, kama kuna wazo tofauti au la kuongezea basi karibu. Maana binafsi bado sijaelewa sawa sawa mantiki ya kurusha hizi ndege.
Leo tarehe 30/09/2015 jumatano mida fulani hivi ya saa mbili asubuhi niliona Ndege ndogo za kivita kama tatu hivi zikifukuzana kwa kasi kuelekea upande wa magharibi.
Tanzania ni nchi ya amani, na Watanzania tumezoea amani. Videge kama hivi navionaga tu kama kuna maadhimisho fulani, sio siku ya kawaida kama ya leo. Sidhani kama kulikua na matangazo kwa wananchi kua watarusha hizo ndege.
Sijaona kama kuna hatari yeyote ya Vita ijayokuja mpaka hivi videge vianze kupiga jaramba. Zaidi naona pengine viko kisiasa zaidi, labda tunatishana na kuogopeshana makusudi. Inawezekana navyo ni sehemu ya kampeni kwa namna moja ama ingine.
Binafsi nimewaza hivi, kama kuna wazo tofauti au la kuongezea basi karibu. Maana binafsi bado sijaelewa sawa sawa mantiki ya kurusha hizi ndege.