Ndege za 540 Zinaboa

Mwanaukweli

JF-Expert Member
May 18, 2007
4,786
1,710
Mimi nilisafiri kwa ndege ya 540 ambayo ilikuwa iondoke Mwanza tarehe 21/5/2011 siku ya Jumatatu saa 7 mchana. Abiria walianza ku check in tangu saa 5 na nusu na kusubiri. Muda wa kuondoka tukaambiwa ndege ina tatizo dogo la kiufundi ambalo linashughulikiwa na hivyo tutarajie kuondoka saa 9.

Ilipofika saa 9 msemaji wa shirika hilo la ndege alikuja na kutuambia kuwa tutarajie ndege itakuja saa 11, na akatupatia soda moja moja na maandazi mawili mawili. Baada ya hapo ikawa kimya mpaka saa 1 jioni tulipoambiwa kuwa ndege itakuja ila itabidi ipitie Zanzibar.

Ndege ilifika muda huo, na saa mbili na nusu tukaondoka kuelekea Zanzibar njiani tukapewa glas ya juice na korosho kidogo na biskuti kama 4 hivi. Tukatua zanzibar kama saa 3 na dak 40. Baadaye tukarudi kwenye runway kuondoka kwenda Dar, lakini rubani akagundua shida nyingine ndogo ya kiufundi. Akaahidi kuwa itashughulikiwa kwa muda mfupi. Baada ya dakika 40 ya kutengeneza, rubani akatuambia tushuke na kuwa ndege haitawezaa kuendelea na safari.

Hatimaye kwenye saa nane tukapelekwa hotelini na kulala bila kupata chakula. Kesho yake tukakodiwa ndege ya Costal Aviation na kufika Dar saa 5 asubuhi, karibu masaa 24 tangu tu check in.

Inaonekana wana ndege moja tu inayofanya kazi Tanzania, ambayo ni mbovu.

Huduma kwa wateja ni mbaya mnoooooooooooo.

Nauli iko juu zaidi ya Precision na Air Tanzania

Jihadhari kabla hujaamua kusafiri na 540
 
Asante kwa taarifa, mimi nitaendelea kupanda mabasi kati ya MZA na DAR.
 
Viwango vya ndege za mshirika mengi ni duni kabisaaa..... Hazifai kpakia binadamu, kwa kuzingatia madhara yatokanayo na ajali zake je Air Tanzania imefufuka????.
 
Ni feki sana service zao. Na rogwa useme unabidili ratiba wanakuchaji si chini ya dola 25. Rafiki yangu juzi alitaka kubadili toka Nairobi akaambiwa aongezee dola 145. Halafu wanatabia za kuchelewa chelewa bila taarifa. Jamani kama ni ndege precision kwa bongo ndoo the best
 
Dah,gharama plus fedheha,sipati picha una mkutano muhimu wa kuhudhuria...
Waafrika tumekuwa wavivu katika kupingana na vikwazo vidogovidogo vinavyoweza kuzuilika...
 
hv ndege kama daladala? Yaani kifo nje nje, na kwann ung'ang'anie tu kupanda? Wakurudishie nauli, peleka kesi mahakamani kwa kupotezewa muda...nyie ndo mnaendelea kuwalea mnavyoendelea kuwaacha na kuendelea kuvi2mia vdge vyao vibovu bovu..sa c bora ungepanda gari? Usirudie!
 
Nauli kwa sasa 540 ni 189,000/=Mza-Dar-Mza kwa mujibu wa tangazo lao lililobandikwa ofisini kwao Mwanza.na hii nadhani imetokana na ATCL kushusha mpaka 199,000/=. Nina tabia ya kutumia 540 mara nyingi sijawahi kukutana na tataizo alilokutana nalo mdau wetu,kwa kweli inasikitisha.

kwan nauli ya ndege kutoka dar kwenda mwnz ni sh ngap jaman
 
kwanza nauli zao ni za kihuni, wanadai mza-dar-mza lowest hadi laki na tisini ila hutakaa upate kwa kigezo iyo ni ya watu 10 wa kwanza lakini kila cku unakua haupo ktk hao kumi wa mwanza, last time nilichajiwa go and return 380,000/-, so hawako honest and open na nauli zao ni danganya toto hizo bei za chini, pili ni kweli hawa jamaa wanandege mbili tu, ile jet wanayojivunia ya bombardier na atr 42, so sidhan kama wana mda wa service maana ratiba zake ziko tight kweli better go with precision at least wana ndege nyingi na wakisema mda hua ndio huo! nadhan wanaitaj kuongeza ndege kwa soko lilivyokubwa hapa nchini hawa jamaa hawatasimamisha huduma kufanya service!
 
Panda air tanzania, kitu ni noma! nauli sawa na bure! kwa nn 540 hawakushusha bei zao mpaka air tanzania watangaze bei ndogo? wauni tu hao, sawa na precision, wote wauni! kitu ni air tanzania, tuwe wazalendo tuachane na ndege za kiuni uni! mungu ibariki tanzania, mungu ibariki air tanzania, nauli ni 199000 dar mwanza dar hakuna usumbufu, dk 45 umeshafka, kitu boing ya ukwel 737
 
Hawa nao wanakaribia kufulia,,,kwa ufupi usafiri wa Anga hapa bongo ni Mungu tu anasaidia...
 
Panda air tanzania, kitu ni noma! nauli sawa na bure! kwa nn 540 hawakushusha bei zao mpaka air tanzania watangaze bei ndogo? wauni tu hao, sawa na precision, wote wauni! kitu ni air tanzania, tuwe wazalendo tuachane na ndege za kiuni uni! mungu ibariki tanzania, mungu ibariki air tanzania, nauli ni 199,000 dar mwanza dar hakuna usumbufu, dk 45 umeshafka, kitu boing ya ukwel 737, precision n wezi balaha! nauli kama unaenda ugaibuni! nauli ni 460,000 dar mwanza dar
 
Panda air tanzania, kitu ni noma! nauli sawa na bure! kwa nn 540 hawakushusha bei zao mpaka air tanzania watangaze bei ndogo? wauni tu hao, sawa na precision, wote wauni! kitu ni air tanzania, tuwe wazalendo tuachane na ndege za kiuni uni! mungu ibariki tanzania, mungu ibariki air tanzania, nauli ni 199,000 dar mwanza dar hakuna usumbufu, dk 45 umeshafka, kitu boing ya ukwel 737, precision n wezi balaha! nauli kama unaenda ugaibuni! nauli ni 460,000 dar mwanza dar

Mkuu nauli za precision ukifanya booking online ni zaidi ya hiyo kwenye nyekundu. Kwamfano nimejaribu kufanya booking online ya kuondoka DAR tarehe 12 June kwenda Mwanza na kurudi tarehe 20 June wananiambia nauli ni USD 396.8 sawa na Tshs. 636,070/= lol! nimechoka.
 
Tena kipindi cha peak season ndo usiseme ukiingia kuulizia nauli ukatoka nje hata kupokea simu ukirudi unaambiwa naul ingine ,mara 2 me imenitokea na hawako makini kabisa na mizigo mara mbili walitaka kupeleka mizigo yetu Nairobi tena sitaki kukumbuka all my academy cert was inside the case.Halafu hi staili yao ya first cancellation $25 sijui imekaaje kwa wahusika wanaosimamia usafiri hapo bongo?Ni binadamu gani hawezi kua na emergency?
 
Itakuja kuanguka siku moja hako ka ndege ka ngama. Bongo hovyo sana. Wakati hilo likijiri Precision Air mvua ikinyesha inaingia ndani wakati ndege ikiwa hewani utadhani mabasi ya kwenda Nanjilinji mikoa ya kusini. Hovyooooooooo.
 
Ndio wakati muafaka wa ATCL kujipanga upya na kulichukua soko lao la africa nzima....bado wana nafasi kurudisha imani kwenye biashara hapa africa
 
Niliwahi kukutana na karaha kama hiyo, ila yangu ilichelewa kwa masaa 3 walituambia ni jet, baada ya huo muda wakatupakia kwenye ATR ndogo na tukapitia zanzbar, turbulance tuliokumbana nayo kutoka zanzbar Dar sitasahau. Kwa kweli nilikasirika sana siku hiyo maana waliifanya safari yangu ikose maana kwa kuchelewa interview muhimu.

Nawashauri tuliunge mkono shirika letu la ATC, juzi nilipanda boing Dar Mza. Huduma zao ni the best, nimesafiri na mashirika mengi ya ndege. Huduma yao inakaribiana na ndege za Qatar. Try ATC you will never regret.
 
540 is really not good! Halafu na lunch yao ya kimkate kikavuu na butter! Na juice!
Na ni kweli ndege zao ni mbovu. Nilipanda once, nikakaa facing bawa, nilijuta manake kulikuwa na stranger noise! I hope watu wa usalama watakuwa makini, the last thing we need is a plane crush manake za barabarani zinatutosha!
 
Back
Top Bottom