Ndege yashindwa kufika eneo la moto mlima Kilimanjaro

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,833
21,466

Ndege ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) iliyokuwa imebeba kamati ya usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro imeshindwa kufika na kufanya tathimini ya athari ya moto katika eneo la Karanga Camp, mlima Kilimanjaro kutokana na hali ya hewa na moshi mzito.
Moshi.


Ndege ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) iliyokuwa imebeba kamati ya usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro imeshindwa kufika na kufanya tathimini ya athari ya moto katika eneo la Karanga Camp, mlima Kilimanjaro kutokana na hali ya hewa na moshi mzito.

Akizungumza leo Jumamosi Oktoba 22, 2022 baada ya kutoka katika eneo hilo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amesema walipofika eneo la mlima Kilimanjaro ndege ilizunguka zaidi ya mara mbili ili kujaribu kufika eneo lenye moto lakini ilishindwa kutokana na hali ya hewa na moshi mkubwa.

"Tumezunguka karibu mara mbili, mara tatu lakini hatukufika kabisa lile eneo la moto kwa sababu mawingu ni makubwa na moshi ni mkubwa, tukaamua turudi kwanza na hali itakapokuwa shwari ndipo tutarudi kuangalia.

Chanzo: Mwananchi
 
moto unawaka, kinachotakiwa ni hatua za haraka za kitaalamu kuuzima na kuuzuia usisambae na sio blah blah..

RC ndio mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama na mkoa, inamaana JWTZ hapo Moshi hawana ndege na plan ya haraka haraka kudeploy ndege nakwenda kuanza kuzima, Zimamoto mkoa hawana utayari wa kuzima moto mlimani?

Hiyo taasisi ya usimamizi wa Mlima kilimanjaro miaka yote hawana option ya kuzima moto ikitokea dharura...

Zipo zile ndege zakumwagilia mashamba dawa, hapo Arusha na Moshi zipo nyingi tu.

Zimamoto mnaweza kuwa na ile powder ya kuzima moto hapo ni quick design ya 200ltrs drums zilizotobolewa chini zibebwe chap na hivyo videge na kwenda kumwaga....
 
moto unawaka, kinachotakiwa ni hatua za haraka za kitaalamu kuuzima na kuuzuia usisambae na sio blah blah..

RC ndio mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama na mkoa, inamaana JWTZ hapo Moshi hawana ndege na plan ya haraka haraka kudeploy ndege nakwenda kuanza kuzima, Zimamoto mkoa hawana utayari wa kuzima moto mlimani? hiyo taasisi ya usimamizi wa Mlima kilimanjaro miaka yote hawana option ya kuzima moto ikitokea dharura...

Zipo zile ndege zakumwagilia mashamba dawa, hapo Arusha na Moshi zipo nyingi tu.
Zimamoto mnaweza kuwa na ile powder ya kuzima moto hapo ni quick design ya 200ltrs drums zilizotobolewa chini zibebwe chap na hivyo videge na kwenda kumwaga....
Ndege za kumwagilia dawa ndo zizime Moto?
 
Hili tatizo haliwezi tatuliwa na Kamati ya ulinzi ngazi ya Mkoa wakuu bali ni KU Taifa janga linazidi kuwa kubwa
 
moto unawaka, kinachotakiwa ni hatua za haraka za kitaalamu kuuzima na kuuzuia usisambae na sio blah blah..

RC ndio mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama na mkoa, inamaana JWTZ hapo Moshi hawana ndege na plan ya haraka haraka kudeploy ndege nakwenda kuanza kuzima, Zimamoto mkoa hawana utayari wa kuzima moto mlimani? hiyo taasisi ya usimamizi wa Mlima kilimanjaro miaka yote hawana option ya kuzima moto ikitokea dharura...

Zipo zile ndege zakumwagilia mashamba dawa, hapo Arusha na Moshi zipo nyingi tu.
Zimamoto mnaweza kuwa na ile powder ya kuzima moto hapo ni quick design ya 200ltrs drums zilizotobolewa chini zibebwe chap na hivyo videge na kwenda kumwaga....
. Pale unapokuwa mjuaji wakati hujui lolote kuhusu lolote, Marekani yenye we na Australia Kuna wakati moto umewaka na sio mliman na hawakuweza ku control for weeks or even months.
 
Tanzania tusione aibu kuomba msaada nje ya nchi, huu Moto sio wa kuzima na NDOO ZA MAJI kama kawaida yetu Bali panahitajika vifaa vya kisasa na wataalamu
 

Ndege ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) iliyokuwa imebeba kamati ya usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro imeshindwa kufika na kufanya tathimini ya athari ya moto katika eneo la Karanga Camp, mlima Kilimanjaro kutokana na hali ya hewa na moshi mzito.
Moshi.


Ndege ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) iliyokuwa imebeba kamati ya usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro imeshindwa kufika na kufanya tathimini ya athari ya moto katika eneo la Karanga Camp, mlima Kilimanjaro kutokana na hali ya hewa na moshi mzito.

Akizungumza leo Jumamosi Oktoba 22, 2022 baada ya kutoka katika eneo hilo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amesema walipofika eneo la mlima Kilimanjaro ndege ilizunguka zaidi ya mara mbili ili kujaribu kufika eneo lenye moto lakini ilishindwa kutokana na hali ya hewa na moshi mkubwa.

"Tumezunguka karibu mara mbili, mara tatu lakini hatukufika kabisa lile eneo la moto kwa sababu mawingu ni makubwa na moshi ni mkubwa, tukaamua turudi kwanza na hali itakapokuwa shwari ndipo tutarudi kuangalia.

Chanzo: Mwananchi
Hizo ni siasa, moto unawaka wanasiasa wanatumia na ndege kwenda kuangalia!
 
Hiyo kamati ilitaka kwenda kuangalia nini huko?hiyo ndege ilitakiwa iwekewe kile kifaa cha kuchotea maji na kuipeleka kuzima moto, helicopters zipo wapi?maana hizi nyingi ni fixed wings zina uwezo wa kuzima moto ,ni kuifungia lile puto, inakwenda bwawani au kwenye mito, chota maji na kwenda kusaidia kuzima moto, sio kila kitu ni politics tu
 
. Pale unapokuwa mjuaji wakati hujui lolote kuhusu lolote, Marekani yenye we na Australia Kuna wakati moto umewaka na sio mliman na hawakuweza ku control for weeks or even months.
Huu ni udhaifu Marekani ndiyo nini
Wakishindwa wao basi na sisi hatuwezi
 
Hapo sasa zamani ukiungua tulikuwa tunakusanywa kama mbuzi kwenda kuzima kwa matawi ya miti
Serikali yangu ya Ccm ni wakati wa kuonyesha TUNAWEZA sio kila kitu mpaka tuombee misaada zimeni huu moto una athari kubwa kibinaadamu
Mungu Ibariki Tanzania Mungu ibariki Africa
 
Back
Top Bottom