X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,817
Ndege Unayetafutwa
1. Ewe ulobahatika, ndege uliye hewani
Unopita ukiruka, na kuranda mitaani
Mwenzio ahangaika, aparamia mitini
Fanya urudi haraka, zikuone zake mboni
2. Fani yako memponza, memuathiri moyoni
Dunia kaimaliza, kwa wengine hulingani
Na sasa wamuumiza,'akutaka,hakuoni
Jaribu utavyoweza, ungie mwake tunduni
3. Fuadi kitanda chako, yeye kakutandikiya
Kifua ndicho tandiko, chake kakuzawadiya
Mwengine kwake hayuko, wewe mekusabiliya
Wafanya nini uliko?, hwendi ukamridhiya
4. Lau moja mevunjika, ya pili mbawa rukiya
Ano'itwa huitika, labeka huitikiya
Huwa hafanyi dhihaka, huenenda kisikiya
Nawe jihimu shituka, ushike wangu wasiya
5. Bahati mekugongeya, iko pako mlangoni
Sioni cha kungojeya, na kuchelewa njiani
Naona waichezeya, shilingi yako ******
Ikangia mepoteya, ndio basi huioni
Maher Fundi
1. Ewe ulobahatika, ndege uliye hewani
Unopita ukiruka, na kuranda mitaani
Mwenzio ahangaika, aparamia mitini
Fanya urudi haraka, zikuone zake mboni
2. Fani yako memponza, memuathiri moyoni
Dunia kaimaliza, kwa wengine hulingani
Na sasa wamuumiza,'akutaka,hakuoni
Jaribu utavyoweza, ungie mwake tunduni
3. Fuadi kitanda chako, yeye kakutandikiya
Kifua ndicho tandiko, chake kakuzawadiya
Mwengine kwake hayuko, wewe mekusabiliya
Wafanya nini uliko?, hwendi ukamridhiya
4. Lau moja mevunjika, ya pili mbawa rukiya
Ano'itwa huitika, labeka huitikiya
Huwa hafanyi dhihaka, huenenda kisikiya
Nawe jihimu shituka, ushike wangu wasiya
5. Bahati mekugongeya, iko pako mlangoni
Sioni cha kungojeya, na kuchelewa njiani
Naona waichezeya, shilingi yako ******
Ikangia mepoteya, ndio basi huioni
Maher Fundi