Ndaisaba mwenyekiti mpya CHADEMA Kata ya Nyakato

Ndaisaba mwenyekiti mpya CHADEMA Kata ya Nyakato

Joined
Dec 11, 2010
Posts
3,321
Reaction score
6,331
Wakuu

Kama mnavyojua kuwa uchaguzi ndani ya chama unaendelea kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini kuanzia ngazi ya msingi, matawi na kata. Leo umefanyika uchaguzi wa kata ya Nyakato wilaya ya Ilemela mkoa wa Mwanza.

Uchaguzi huo ulikuwa na wagombea watatu, Wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti walikuwa ni Ndaisaba Burushi, John Membe na Didas Seyuu.

Wagombea hao na kura zao

1. Ndaisaba Aroni Burushi - kura 45.

2. John Membe kura - 33

Na

3. Didas Seyuu kura - 22.

Jumla ya wapiga kura ni 100. Hakuna kura iliyoharibika.

Kata hiyo sasa inaungana na kata nyingine zilizo maliza chaguzi kujiandaa kwa uchaguzi wa wilaya, mkoa na baadae Taifa.

Pichani ni matukio wakati wa uchaguzi huo.
 

Attachments

  • 1404726659301.jpg
    1404726659301.jpg
    76.3 KB · Views: 278
  • 1404726699230.jpg
    1404726699230.jpg
    58.7 KB · Views: 232
  • 1404726737540.jpg
    1404726737540.jpg
    45.5 KB · Views: 217
hizi ndizo habari tunazotaka kusikia na si kupiga porojo humu jf na wachumia tumbo
 
Hongereni kwa kazi nzuri mliyoifanya & thanks for the info. Mwisho wa mamluki unakaribia kwisha Cdm.
 
Eti CCM na vibaraka wao wa ACT wanataka kuua Chadema.Hizo ni Ndoto za Abunuasi
 
Eti CCM na vibaraka wao wa ACT wanataka kuua Chadema.Hizo ni Ndoto za Abunuasi
Wakati Chadema kinajiimarisha kwenye msingi ili kupata wajumbe wa baraza kuu na mkutano mkuu wa taifa wasaliti wamekaa wakisubiri kiti cha Mbowe kidondoke.
 
Wakuu

Kama mnavyojua kuwa uchaguzi ndani ya chama unaendelea kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini kuanzia ngazi ya msingi, matawi na kata. Leo umefanyika uchaguzi wa kata ya Nyakato wilaya ya Ilemela mkoa wa Mwanza.

Uchaguzi huo ulikiwa na wagombea watatu, Wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti walikuwa ni Ndaisaba Burushi, John Membe na Didas Seyuu.

Wagombea hao na kura zao

1. Ndaisaba Aroni Burushi - kura 45.

2. John Membe kura - 33.

3. Didas Seyuu kura - 22.

Jumla ya wapiga kura ni 100. Hakuna kura iliyoharibika.

Kata hiyo sasa inaungana na kata nyingine zilizo maliza chaguzo kujiandaa kwa uchaguzi wa wilaya, mkoa na baadae Taifa.

Pichani ni matukio wakati uchaguzi huo.

Hongera zake sana ajitahidi kujenga chama maeneo ya meco nundu hapo sokon neshinal gedeli na mitaa ya temeke kwan kuna wapiga kura wengi sana. Nasubiri kata ya mahina na butimba.
 
Mapunguani ya ccm na tawi lao ACT wao wanawaza uchaguzi wa mwenyekiti mbowe tu.

Na wao kwao hizi zinazoendelea sasa hawazioni kuwa ni chaguzi za muhimu. CHADEMA ni chama pekee pinzani kimefanya/kinafanya chaguzi kuanzia ngazi ya msingi na matawi nchi nzima kuelekea kwenye uchaguzi wa kata, wilaya na kisha mkoa kabla ya ule mkubwa wa taifa.

Tunasonga mbele kwa dhana na spirit ile ile " ...hakuna kulala mpaka kieleweke..."
 
Eti CCM na vibaraka wao wa ACT wanataka kuua Chadema.Hizo ni Ndoto za Abunuasi

Kaka sikufichi wanavyopambana kuiua cdm kumbe ndio wanavyoijenga. Juzi nilibahatika kua mkoa wa kagera maeneo ya ngara kama rulenge kabanga kanazi benako na rusumo hakika wananchi wanaijenga cdm kwa nguvu zote wanahamasishana sana juu ya uchaguzi wa serikali wa serikali za mtaa kuelekea uchaguzi mkuu. Wamechoshwa kuitwa wakimbizi mbunge wao kawatenga sana hafiki jimboni. Baada yakutoka ngara nilifika wilayani kakonko mkoa wa kigoma hakika wananchi wana hali mbaya sana kuanzia miundo mbinu maji afya shule ni shida tupu. Wanalalamika mbunge wao ambaye ni waziri amewatelekeza yeye bunge likiisha anaenda kwake moshi. Kakonjo ni kama hawana mbunge.
 
Wakati Chadema kinajiimarisha kwenye msingi ili kupata wajumbe wa baraza kuu na mkutano mkuu wa taifa wasaliti wamekaa wakisubiri kiti cha Mbowe kidondoke.

Watasubiri sana.
 
Hongera zake sana ajitahidi kujenga chama maeneo ya meco nundu hapo sokon neshinal gedeli na mitaa ya temeke kwan kuna wapiga kura wengi sana. Nasubiri kata ya mahina na butimba.
Mkuu,
Kata za Butimba na MAhina uchagizi wao ulifanyika mwezi wa sita.
 
Mkuu,
Kata za Butimba na Mahina chaguzi zake
zimeshafanyika toka mwezi wa sita.

Natambua mkuu. Tunakwenda na style hii kuchuja makapi ya mkakati wa mabadiliko 2013 kupitia ule mpango wao wa kuwa na MK1 mpaka MK10 na ile MMK1 mpaka MMK30.

Tunawabana kotekote.
 
Hiyo ndiyo cdm,mamluki wote watajifuta wenyewe!
 
Mkuu,
Kata za Butimba na Mahina chaguzi zake
zimeshafanyika toka mwezi wa sita.

Mkuu leteni na matokeo ya hizo kata za Butimba na Mahina hâta kama chaguzi zilifanyika mwezi wa 6 ili yaunganishwe hapa maintarahamwe yazidi kutahayari.
 
Mods heading ya kwanza ilikuwa sahihi, hapa ni thread ya matokeo ya chaguzi mbali mbali za chama kuanzia ngazi za misingi,
 
Back
Top Bottom