Ndaga, Malafyale Magufuli

Mkuu kama ule mfuoa wa barabara za Tukuyu unatafunwa, huu wa doble way Mbeya utafanyika tu.
Ndo maana nasema its a matter of time.
 
Mkuu viongozi wote si sawa, na ni jana tu hata Magufuli amesema hata yeye ana mapungufu.
Tuchukuliane kwa wema na kupendana.
Pale penye makosa tukosoane ili sote tusonge mbele.

Tukubali kuwa huko Tukuyu Magufuli katekeleza ahadi ambazo aliziweka, kwa hilo tumshukuru.
 
Waliokuwa na nia mbaya wameumbuka, Magufuli amefanya ziara yenye mafanikio na amepokewa na wananchi wengi sana haijapata kuonekana Mbeya.
Mkuu mdogo wangu alivonipigia simu toka Busokelo, furaha yake niliisikia akitaka kulia kwa shukrani. Tumeteseka sana kwa barabara hizi za kwenda milimani, asante Magufuli.
Siye tunashukuru kwa matendo mema, naona roho yako inaomba laana ikutokee.
Unapo ahidi wananchi, ustaarabu ni kutekeleza. Pamoja na kuahidi kila kampeni ya urais kama ilani ya chama, sina kumbukumbu marais wetu ingakao kufika huko makwetu. Magufuli aliahidi, sasa anatekeleza. Ndaga Magufuli.
Mkuu hilo ni kweli kabisa, Mbeya bado ni ngome ya CCM. KUNA wanafiki hata ndani ya CCM wameumbuka walisema Mbeya kuna ukabila, ati wanamchukia Magufuli! Nyomi iliyojitokeza kumpokea Magufuli imewaumbua vibaya.
Duh! Njaa mbaya sana, hizo sifa! Kwa majaliwa ukumbukwe enzini... Kumbe huko Mbeya kuna wao na sisi! Nilidhani mkusanya kodi ni moja tu! Heri mlioambulia barabara, wapo walioambulia risasi za moto na wengine kuishia magerezani kama si kupoteza kabisa maisha!
 
Simple minds mnafikiria njaa.

Tukuyu na Mbeya kwa ujumla hakuna njaa ya aina yoyote.

Tatizo ni maendeleo.

Bila kichocheo cha miundombinu bora, tatizo lililopo toka uhuru, maendeleo yatakuwa ndoto.

Naamini hujafika Mwakaleli, hivyo hujui kinachoongelewa hapa.
 
Mbeya tunajuwa ujenzi wa barabara ni kodi zetu. Ajenge ila siyo kigezo cha kutafuta kura.
 
Mbeya tunajuwa ujenzi wa barabara ni kodi zetu. Ajenge ila siyo kigezo cha kutafuta kura.
Tutampa kura tu kwa kutimiza ahadi.
Kuna walioahidi na kutotekeleza, hata kuja kushukuru tu hawakuja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…