LuciusKaisery
Member
- Feb 19, 2018
- 18
- 31
- Alipigwa risasi Tundu Lissu
Watanzania wengi waliongea wengine wa waka-post mitandaoni twitter, facebook, instagram tukaishia hapo. Hakuna hatua inayochukuliwa.
Watanzania wengi waliongea wengine wa waka-post mitandaoni twitter, facebook, instagram tukaishia hapo. Hakuna hatua inayochukuliwa.
3. Kapotea Azory mwandishi wa habari ya Mwananchi.
Watanzania wengi waliongea wengine wa waka-post mitandaoni twitter, facebook, instagram tukaishia hapo. Hakuna hatua inayochukuliwa.
4. Msimu wa Makonda
Watanzania wengi waliongea wengine wa waka-post mitandaoni twitter, facebook, instagram tukaishia hapo. Vyombo vya kutetea haki za vyombo vya habari vikaalani vikali vikaishia hapo. Hakuna hatua inayochukuliwa.
5. Kifo cha Aquelina Akwilini
Watanzania wengi wanaongea wengine wa wana-post mitandaoni twitter, facebook, instagram tunaishia hapo. Wengine wanataka Mwigulu Nchemba ajiudhuru tutaishia hapo. Hakuna hatua itayochukuliwa.
6. Serikali awamu ya tano na usimikaji wa mfumo wa chama kimoja.
Watanzania tunaongea bila kuchukua hatua yoyote. Vyama pinzani nchini vinakandamizwa, kuwa mpinzani nchini ni jinai au hatia. Tuna kila sababu ya kusema chama tawala kinanunua viongozi wa vyama pinzani na moja kwa moja serikali inahusika. Kwa nini tunasema serikali inahusika? Serikali kama inaridhia kutoa pesa za kurudia chaguzi ndogo ndogo maana inafurahiswa na swala hilo. Bado wakishinda chaguzi ndogo ndogo wanafurahi, chaguzi sio za haki na huru kuna furaha ya kweli hapo? Unapigana na mtu umempatia panga wewe una bunduki nawe unasema ulipambana kweli kweli? Mpe bunduki nae.
Sisi tutakuwa nchi ya aina gani? Kuzungumza ndio suluhisho tosha? Ina maana hatujui mizizi ya matatizo yetu? Hatujui chanzo cha matatizo yetu?
Kwa nini tunashindwa kuungana watanzania? Kupelekea tunakuwa nchi ya waongeaji.
Tunakubali kugawanya na vyama vya siasa vyetu.Vyama vya siasa visitugawe tukashindwa kukemea na kutatua matatizo yetu na tukumbuke hamna tatizo la mtanzania mmoja mmoja bali kuna tatizo la watanzania.
Huenda ungekuwa wewe au mimi tungepigwa risasi au kutekwa utasemaje ni tatizo la mtanzania mmoja mmoja.
Kuwa mfuasi wa CCM ndio isiwe serikali ikikkosea au inapokosea au inapoiminya katiba ndio ushindwe kuungana na wengine au ushindwe kukosoa kisa tu wewe ni mkereketwa wa CCM hivyo hivyo kwa vyama pinzani.
CCM si zaidi ya utaifa wetu au Upinzani si zaidi ya Utanzania wetu au Utanganyika wetu au Unzanzibari wetu. Au tushindwe kuungana tutatue matatizo yetu ya Tanzania yetu kisa vyama vyetu vya siasa. Tanganyika au Zanzibari ilikuwepo kabla ya vyama vya siasa vyote nchini.
Jambo baya ni baya tu haijalisha nani amefanya awe babaako au mamako au ndugu yako litabaki kuwa baya tu.
Kifo cha Aquelina Akwilini tunajua tatizo ni nini, lakini tunatupiana lawama. CHADEMA walikuwa wanatumia haki ya msingi kikatiba ya MAANDANO HURU NA YA AMANI. Ni kosa kutumia haki yako kikatiba? CHADEMA ndio waliopiga risasi? Au Aquelina Akwilini alikuwa miongoni mwa waandamanaji wa CHADEMA?
POLISI ndio waliopiga risasi kwa mgongo wa kuzuia maandamano, Unazuia maandamano kwa kupiga risasi? Waandamanaji walikuwa na silaha? Halafu tunataka kuzui matumizi mabovu ya silaha au kuzuia maandaamano?
Mfano hili jambo lipo wazi tutataka kuleta uhusikaji wa vyama vya siasa, lakini chama tawala kinazungumzia upande mmoja kukishtumu CHADEMA. Lakini chama tawala kinasahau kuwa ndio chanzo cha matatizo yote.
Tume ya taifa ya uchaguzi NEC si taasisi huru ipo chini ya chama tawala, NEC inashirikiana moja kwa moja na chama tawala. NEC nayo inapaswa kuwajibishwa, Lakini wa kuwa-wajibisha nani? Serikali au Bunge au Mahakama? Mihimili yote ni chama tawala, vinatumika na chama tawala na viko chini ya chama tawala.
Serikali inasema haina hela lakini inapata wapi mabilioni ya kurudia chaguzi ndogo ndogo hizi? Kwenye kuongeza mshahara wa mwalimu serikali inasema haina pesa, kwenye mambo ya msingi serikali inasema haina pesa.
Tuache siasa, tuache kuzungumza zungumza na tuache kulopoka lopoka tuchukue hatua ya vitendo stahiki.