malisak
Platinum Member
- Mar 16, 2006
- 739
- 852
Naandika Uzi huu huku Nikiwa nimegubikwa na huzuni nyingi na masikitiko makubwa sana. Nchi yetu imekuwaje?
Ile nchi tulioisifu kwa mapambio, tungo na ngonjera za kuvutia kwani kuna laana ilioachwa na waasisi Baba wa taifa Mwl. Nyerere na akina Mkwawa? toka kipindi cha kupata Uhuru na Hatujui? Hatusikilizani tena, hatuelewani tena na hatuheshimiani tena.
Ni masikitiko makubwa Sana kuona mkanganyiko juu ya kishika madaraka, demokrasia umekufa, Uhuru imetoweka, tumedhuriwa na hofu na taharuki kila Wakati. Kwani tumekosea wapi? Kila nikitafakari nakosa majibu.
Kuna Muda nakumbuka maneno ya waziri ya fenda "Hamieni Burundi" kila nikitafakari Ile kauli ni kama ilikuwa na unabii uliojificha ambao muheshimiwa aliuchukulia kama mzaha Lakini kuna kaukweli ndani Yake.
Sitaki kusikia wala sitamani na Sisi siku moja tuwe wakimbizi, natamani Amani yetu,umoja na mshikamano wetu na kama kutawala na hofu basi iwe na hofu ya Mungu Tu. Nikitazama video za wenzetu waliopoteza Uhuru na Amani yao napata hisia mbaya juu ya hatma ya kizazi chetu kama itatokea tukakiacha huko siku zijazo.
Jasho la maumivu na hofu linanimwagika,machozi ya damu yanavuja moyoni mwangu nikitafakari Nyakati. Natamani Muda urudi Nyuma,natamani ule upendo wetu uliotukuka mpaka kubatizwa jina la kisiwa cha Amani. Hebu tushushe silaha chini na tusalimu amri kwa manufaa ya nchi yetu.
Natamani kuona tukicheka na kutabasamu pamoja tena mbele ya majukwaa yenye kumiliki midahalo ya mgongano wa mawazo yenye kujadili mustakabali wa nchi yetu hii Nzuri ya kuvutia.
Mungu bariki na uwezeshe Amani ya nchi hii irejee na kudumu kama zamani. Naamini hakuna kinachoshindikana chini ya jua tukikubali kujishusha. Mungu tusaidie.
Ile nchi tulioisifu kwa mapambio, tungo na ngonjera za kuvutia kwani kuna laana ilioachwa na waasisi Baba wa taifa Mwl. Nyerere na akina Mkwawa? toka kipindi cha kupata Uhuru na Hatujui? Hatusikilizani tena, hatuelewani tena na hatuheshimiani tena.
Ni masikitiko makubwa Sana kuona mkanganyiko juu ya kishika madaraka, demokrasia umekufa, Uhuru imetoweka, tumedhuriwa na hofu na taharuki kila Wakati. Kwani tumekosea wapi? Kila nikitafakari nakosa majibu.
Kuna Muda nakumbuka maneno ya waziri ya fenda "Hamieni Burundi" kila nikitafakari Ile kauli ni kama ilikuwa na unabii uliojificha ambao muheshimiwa aliuchukulia kama mzaha Lakini kuna kaukweli ndani Yake.
Sitaki kusikia wala sitamani na Sisi siku moja tuwe wakimbizi, natamani Amani yetu,umoja na mshikamano wetu na kama kutawala na hofu basi iwe na hofu ya Mungu Tu. Nikitazama video za wenzetu waliopoteza Uhuru na Amani yao napata hisia mbaya juu ya hatma ya kizazi chetu kama itatokea tukakiacha huko siku zijazo.
Jasho la maumivu na hofu linanimwagika,machozi ya damu yanavuja moyoni mwangu nikitafakari Nyakati. Natamani Muda urudi Nyuma,natamani ule upendo wetu uliotukuka mpaka kubatizwa jina la kisiwa cha Amani. Hebu tushushe silaha chini na tusalimu amri kwa manufaa ya nchi yetu.
Natamani kuona tukicheka na kutabasamu pamoja tena mbele ya majukwaa yenye kumiliki midahalo ya mgongano wa mawazo yenye kujadili mustakabali wa nchi yetu hii Nzuri ya kuvutia.
Mungu bariki na uwezeshe Amani ya nchi hii irejee na kudumu kama zamani. Naamini hakuna kinachoshindikana chini ya jua tukikubali kujishusha. Mungu tusaidie.