Watu wanajiuliza kwanini tanzania haipo kwenye list pia wanajiuliza kwanini Niger imeingia kwenye list ?. Binafsi naweza kusema hivi Tanzania uchumi wake unakuwa kwa sana lakini ukuaji wake wa uchumi hauendi sambamba na ukuaji wa maendeleo ya nchi, kwa kimombo changu duni naweza kusema ( There is no relationship between Economic Growth and Economic Development in Tanzania).
Infact uchumi unakuwa kwa kasi ya ajabu sana huwezi kuamini mpaka mataifa makubwa tajiri yanashangaa sana kasi ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania, The big problem is how to redistribute this income to individuals, huu uchumi unarubuniwa na kuishia kwenye mikono ya watui wachache wenye roho za ubinafsi wasiokuwa na hata chembe ya huruma kwa wananchi wengine, mfano mdogo tu angalau mapesa ya escrow watu walivyo gawana kirahisi sana mahela kibao.
Lakini kama huu uchumi ungefanya kazi moja kwa moja kuleta maendeleo ya nchi na kwa wananchi kwa ujumla nakwambia hii nchi ingekuwa zaidi ya Africa Kusini. Tatizo kubwa ni rushwa na nchi yetu inashika nafasi za juu sana kwenye mambo ya rushwa