Nchi 14 za Kiafrika zinalipa Kodi Ufaransa

Nchi 14 za Kiafrika zinalipa Kodi Ufaransa

Kama hatuja jitambua unategemea nini? Halafu kama nshu ni barabara waliwatawala Rwanda pia mbona hawamo?

Unyarwanda haikuwahi kutawaliwa na Ufaransa bali kama sisi ilitawaliwa na Ujerumani halafu baadaye Ubelgiji, lugha ya kifaransa ni kwa sababu ya Ubelgiji!
 
Daah nimesoma hayo mamikataba hadi Machozi yamenilengalenga!

nikiyaona ya kwetu hapa Tanganyika naweza kuzimia kabisa!

Kumbe ndio maana vita na Mapinduzi hayaishi Afrika Magharibi!
 
Tuwafukuze waingereza tuitawale tanganyika yetu-Asante baba nyerere 2 Asante kabisaaa,kumbe ndo maana,nyerer alitekeleza
 
Daah nimesoma hayo mamikataba hadi Machozi yamenilengalenga!

nikiyaona ya kwetu hapa Tanganyika naweza kuzimia kabisa!

Kumbe ndio maana vita na Mapinduzi hayaishi Afrika Magharibi!

wewe lia tu ila jua habari yenyewe feki
 
Equatorial Guinea na Guinea Bisao zote ni wanachama wa Francophone au nchi zilizochini ya mwamvuli wa Ufaransa kama vile tulivyo sisi kwenye kwenye Commonwealth ya Uingereza na pia wanatumia West African Franc ambayo inacontroliwa moja kwa moja na Benki Kuu ya Ufaransa Paris!

huwa najiuliza sana,hv inakuwaje mtu amekutawala alafu bado eti mnajiita nchi za commonwealth.U.S.A si imetawaliwa na uengeleza mbona haipo ktk umoja huo
 
huwa najiuliza sana,hv inakuwaje mtu amekutawala alafu bado eti mnajiita nchi za commonwealth.U.S.A si imetawaliwa na uengeleza mbona haipo ktk umoja huo

Sasa unashangaa hilo jiulize ni kwa nini wakati Ubalozi walivyoamua kupeleka shughuli za Visa kenya kwa sababu ya kubana matumizi nchi nzima ilihamia Uingereza kwenda kuwaomba warudishe shuguli TZ mpaka Bunge zima lilijadili hili swala wakati hili ni swala la binafsi kabisa la nchi ya Uingereza na wanaamua ni wapi wawe na Ubalozi na wapi wasiwe nao!
Lakini Mwafrika anafikiri ni haki yake na anaandamana kwa hilo na tena siyo mwafrika wa kawaida bali msomi na Kiongozi kuanzia Raisi Kikwete, Waziri Mkuu Pinda mpaka awaziri wa mambo ya ndani na Bunge walikaa kujadili na kuomba Uingereza warusdishe viza section Dar!,
 
Itakuwa nyerere nae aliuza mechi, burebure tu sio rahisi, maana no pain,no gain
 
Ka uchache hili la kulipa fedha Ufaransa nalikubali. Niliishi nchi iliyotawaliwa na Mfaransa na wote, isipokuwa Guinea Conakry) wanatumia CFA ambayo central bank yake iko Ufaransa. Kwa ujumla nakubaliana na mengi katika orodha hiyo. Kwa ushahidI Sekou Toure wa Guinea alimkatalia De Gaule uhuru wa masharti. Matokeo yake Wafaransa wakang'oa kila kitu na kupakia hata visu vya hospitali vya kufanyia opresheni! Wakoloni wote wabaya ila Mfaransa kiboko yao. Na sisi hivi sasa twajipendekeza kwao kuwaomba.
Wadhani Sankara aliuawa kwa nini?
 
Kwa kuongezea tu: wakati baba yake alipokufa (Omar Bongo kibaraka mkuu wa Ufaransa), Ali Bongo rais wa sasa, aliwahi kutamka kuwa ' Ufaransa inabidi ibadilike na isitegemee kunyonya' hata akaanza kufanya mipango ya kujitoa na Umoja wa Sarafu........lakini yakaishia hapo. Nadhani aliambiwa ukithubutu utaona kaburi kabla ya siku zako!
 
Back
Top Bottom