February
Member
- Nov 15, 2011
- 90
- 21
Mbunge wa kigoma kusini na katibu mwenezi wa nccr mageuzi david kafulila amesema chama chao hakihitaji kukutana na Rais JK kwakuwa CCM, Serikali na hata Rais mwenyewe haina dhamira ya kweli ya kuleta katiba mpya.
Kafulila aliliambia tzdaima kuwa wameshangazwa na kauli ya ccm ya kutaka mazungumzo hayo yahusishe vyama vingine. Uamuzi wa kamati kuu ya ccm kuwa vyama vyote vikutane na JK. Sioni mantiki yake badala yake naona akutane na wanaotaka kukutana nae alisema Kafulila na kuongeza
"Binafsi sitegemei lolote kutoka katika kikao kwa namna hiyo. Wabunge wa nccr hawakutoka bungeni ili badae wakutane na rais. Tunaamini yeye rais, chama chake ccm na hata serikali yake hawana dhamira yakweli katika agenda ya katiba mpya tangu awali na hawatakuwa nayo" akitetea kauli yake, kafulila alisema CCM haiko tayari kukubali mabadiliko kwani ni msumari kwake yeye, ccm na serikali yake.
Akifafanua hoja hiyo kafulila alitoa mifano mitano kuthibitisha hilo. Kwanza ccm walikataa kuingiza agenda ya katiba kwenye ilani yao ingawa ilikuwa mahitaji ya umma, pili hata bada ya uchaguzi mwanasheria mkuu na waziri wa sheria na katiba waliweka wazi kuwa katiba mpya sio muhimu kwasasa kauli ambayo haijafutwa. Tatu ni kwa msingi huo mwezi april serikali kupitia baraza la mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni rais walileta muswada mbovu kabisa ulioibua hasira hata kutakiwa urejeshwe serikalini. Nne bada ya kurudisha kikao kilichopita wamerudisha muswada mpya ambao ilitakiwa usomwe kwa mara ya kwanza ili umma upate nafasi kujadili lakini serikali na ccm wamekataa.
Na kuhitimishwa na kikao cha rais na wazee wa ccm mkoa wa dar kupuuza sauti ya umma ndani na nje ya bunge. Huu ni ushadi tosha kuwa hakuna dhamira ya kweli kutoka kwa rais na chama chake na hivyo nccr hatuoni sababu ya kushiriki alihitimisha Kafulila.
Kafulila aliliambia tzdaima kuwa wameshangazwa na kauli ya ccm ya kutaka mazungumzo hayo yahusishe vyama vingine. Uamuzi wa kamati kuu ya ccm kuwa vyama vyote vikutane na JK. Sioni mantiki yake badala yake naona akutane na wanaotaka kukutana nae alisema Kafulila na kuongeza
"Binafsi sitegemei lolote kutoka katika kikao kwa namna hiyo. Wabunge wa nccr hawakutoka bungeni ili badae wakutane na rais. Tunaamini yeye rais, chama chake ccm na hata serikali yake hawana dhamira yakweli katika agenda ya katiba mpya tangu awali na hawatakuwa nayo" akitetea kauli yake, kafulila alisema CCM haiko tayari kukubali mabadiliko kwani ni msumari kwake yeye, ccm na serikali yake.
Akifafanua hoja hiyo kafulila alitoa mifano mitano kuthibitisha hilo. Kwanza ccm walikataa kuingiza agenda ya katiba kwenye ilani yao ingawa ilikuwa mahitaji ya umma, pili hata bada ya uchaguzi mwanasheria mkuu na waziri wa sheria na katiba waliweka wazi kuwa katiba mpya sio muhimu kwasasa kauli ambayo haijafutwa. Tatu ni kwa msingi huo mwezi april serikali kupitia baraza la mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni rais walileta muswada mbovu kabisa ulioibua hasira hata kutakiwa urejeshwe serikalini. Nne bada ya kurudisha kikao kilichopita wamerudisha muswada mpya ambao ilitakiwa usomwe kwa mara ya kwanza ili umma upate nafasi kujadili lakini serikali na ccm wamekataa.
Na kuhitimishwa na kikao cha rais na wazee wa ccm mkoa wa dar kupuuza sauti ya umma ndani na nje ya bunge. Huu ni ushadi tosha kuwa hakuna dhamira ya kweli kutoka kwa rais na chama chake na hivyo nccr hatuoni sababu ya kushiriki alihitimisha Kafulila.