NBS - Taasisi inayotudharirisha kimataifa

Tutafika

JF-Expert Member
Nov 4, 2009
1,443
631
NATIONAL BUREAU OF STATISTICS (NBS)


National Bureau of Statistics Tanzania - NBS


Hii taasisi, kusema kweli watanzania wengi hawaijui. Si kwa sababu hakuna ufisadi unaoendelea huko, hasha!, ni kwa sababu ya kushidwa kwake kutekeleza majukumu. Taasisi hii inategemewa kutoa takwimu za kitaifa za mambo yote yanayolihusu taifa la Tanzania. Mambo ya kiuchumi, kijamii, kisiasa, n.k. Hii taasisi inategemewa itoe hali halisi ya nchi yetu na itoe habari zinazoendana na wakati.


Kwanini nasema inatudharirisha?

Kila mtu anajua umuhimu wa takwimu na jinsi takwimu zinavyoweza kutumika vibaya zikaleta adhari kubwa katika maisha ya mtu mmoja mmoja. Takwimu zinazotumika kuielezea Tanzania kimataifa hazitokani na taasisi hii na wala haijawahi kusema lolote kuhusu takwimu hizo. Kimsingi Takwimu hizo zimekosewa ama kwa makusudi au kwa kukosa takwimu mbadala (za ukweli). Takwimu zinazopatikana https://www.cia.gov/library/publications/the-world-factbook/geos/tz.html nyingi hasa za kiuchumi sio za kweli na zinatudharirisha. Nani anawajibika katika hili?, bila shaka ni hii taasisi.

Wanauchumi wanajua jinsi kipimo cha uchumi - GDP, ambavyo kinatumika kufanya watu wajione wanyonge na wajidharau. GDP kwa nchi kama yetu ambayo watu wake wanaishi kwa kutegemea kilimo na ambayo zaidi ya asilimia 75 wanalima na kula wenyewe bila kuuza, haiwezi kuonesha hali halisi ya maisha ya mtanzania. haiwezi kuwa kipimo cha umasikini wetu. Katika hili, NBS ilitakiwa iwe ya kwanza kupima uchumi wetu na kuweka takwimu sahihi zinazojumuisha uzalishaji wa watu wote, lakini cha kushangaza, hata takwimu za uchumi wetu hazipo NBS!!


Je, kuna haja ya kuwa na taasisi hii isiyo na faida?, Viongozi wa Taasisi hii wanafanya nini?,
 
Ndugu ulilosema ni kweli tupu. Mimi nadhani wizara na idara zote za serikali hazina mfumomzuri wa ukusanyaji takwimu na kuzifania update. Inawezekana ni makusudi au kugomba kwa teknohama. Lakin ukweli unabakia pale pale kuwa mfumo kwa sasa ni mbovu na takwimu nyingi zimeparaganyika. Ndo maana hata ndani ya serikali unaweza kuuliza takwimu juu ya jamboo fulani, lakini document unazopewa zinakuwana different figues!
 
TUTAFIKA!!
Unamaanisha kwamba hawa Jamaa wakicalculate GDP independently majibu yatakuwa kwamba tunaishi juu ya Dolla Moja kwa siku au unataka watoe statistics za namna hiyo ili kuficha aibu?
 
Ndugu ulilosema ni kweli tupu. Mimi nadhani wizara na idara zote za serikali hazina mfumomzuri wa ukusanyaji takwimu na kuzifania update. Inawezekana ni makusudi au kugomba kwa teknohama. Lakin ukweli unabakia pale pale kuwa mfumo kwa sasa ni mbovu na takwimu nyingi zimeparaganyika. Ndo maana hata ndani ya serikali unaweza kuuliza takwimu juu ya jamboo fulani, lakini document unazopewa zinakuwana different figues!

Yaani ni balaa, ukienda NBS kuulizia takwimu za uchumi wetu wanakuambia nenda BoT. BoT nako ukienda wanakuambia nenda NBS. Kama vile hawajui majukumu yao
 
TUTAFIKA!!
Unamaanisha kwamba hawa Jamaa wakicalculate GDP independently majibu yatakuwa kwamba tunaishi juu ya Dolla Moja kwa siku au unataka watoe statistics za namna hiyo ili kuficha aibu?

Sio kuficha aibu, ni ukweli kwamba takwimu sio za kweli. Wafanye hiyo kazi wenyewe badala ya kuachia World bank ambao wanabuni tu na kuacha kusema hali halisi. vitu vyote ambavyo haviendi sokoni vikiingizwa kwenye calculation ni dhahiri tunaishi juu ya dola 1. NBS wafanye kazi waache kula mshahara wa bure (wizi)
 
Back
Top Bottom