Credibility ya aliyeleta hii mada ni questionable, huwezi toa accusation kali kama hizi bila vivid evidence bwana, be specif, what happened? Umefikia wapi conclusion hii? Acha ubabaishaji
MSent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
Hata NMB mambo ni hivyo hivyo. Rais dhaifu, Tiss dhaifu, ndo matunda hayo ya CCM.
Kuna mchezo wa kupunguza buku mbili mbili kila akaunti,alafu hela badala ya kufanya kitu cha maana wanaleta tunywe.
Nafikiri hizi ni tuhuma nzito sana kwa benki yote kwa ujumla! haya mambo hutokea na unapaswa kuripoti kwenye benki husika! kuleta mada kama hii mahali kama hapa ni kujaribu ku-damage taswira ya benki husika na najua unafanya hivi kwa urahisi kwasababu ID yako halisi haiko revealed!
Nakushauri uende au uwaandikie barua NBC ninaamini watahandle vizuri suala lako lakini zaidi utawasaidia kujua tatizo na ukubwa wa tatizo! Binafsi niliwahi kukuta pesa yangu imepungua katika akaunti yangu kwenye benki moja jina ninalihifadhi,niliwaandikia barua na nikakutanishwa na Manager anayeshughulikia malalamiko ya wateja ambaye alinisaidia na marekebisho yakafanywa katika akaunti yangu na bado ninaendelea kubenki na benki hiyo!
Nakushauri badala ya kuipaka matope NBC shughulikia suala lako kwa njia zinazostahili tatizo ni kwamba watanzania tumekosa uaminifu sana hilo haliko NBC pekee ndiyo maana nimesema ni vyema ufuatilie suala lako vizuri badala ya kukimbilia kuichafua benki hiyo!
Lawrence Mafuru ...ameondoka,walitaka kumuharibia CV....,amepata kazi Nzuri Zaidi
Mkuu.. Madai yako ni mazito bt yanaweza kuwa yanatoka upande wa pili.. Maana wabongo kwa fitina ciku hizi..!
Ninapenda kuchukua nafasi hii kuutaarifu umma kuwa usalama wa Pesa za watanzania katika benki ya NBC si wa uhakika.
Kuna wizi wa ndani kwa ndani unafanyika katika account za wateja. Nipende kuwaomba wateja wote wa benki hii wafike katika matawi ya NBC ili waangalie Bank statement zao.
Pia niwaombe Usalama wa Taifa, Benki Kuu ya Tanzania, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali, Polisi na Mamlaka zote zinazohusika, watume timu zao kwa ajili ya kuichunguza Benki hii Kongwe nchini.
Mambo yakiachwa yaendelea hivi, mamilioni ya Watanzania yatapotelea kwa mafisadi wachache.