Wakuu habari zenu na wale wakristo heri ya Pasaka.
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Mimi ni mtu ambaye kazi zangu nyingi nazifanyia ndani nikiwa peke yangu na ninaoshiriikiana nao wengi ni foreigners hivyo kazi tunazifanya na kuzifuatilia kupitia Slack, Hubstaff, Jira n.k. Huku tukishiriki sana Zoom na Google Meet video calls.
Hali hii imenifanya marafiki zangu wengi wawe ni watu walioko mbali lakini marafiki ambao ni rahisi kukutana na kujumuika nao moja kwa moja hasa weekends sina.
Pia mimi si mpenzi wa mpira kihivyo, japo ni shabiki wa yanga lakini ni shabiki wa kufuatilia matokeo tena kupitia kwenye threads humu jamiiforums. Zaidi napenda sana kutazama documentaries mfano True Crimes, Crime report za aljazeera na comedy kidogo hasa Dave Shappelle.
Iikitokea nimetoka sipendi kwenda sehemu zenye kelele, napenda kwenda sehemu zenye watu lakini kuwe kumetulia hakuna muziki mkubwa na makelele.
Pia si mlevi au niseme mnywaji, ikitokea nimekunywa pombe haiwezi kuzidi bia 3 tena lite. Spirits, gin siguzi kabisa.
Yani haya mambo yananifanya nikose marafiki na kuna muda nakuwa natamani kuwa na marafiki nijumuike nao. Siwezi kusema mimi ni introvert kwa sababu nazungumza sana na nina utani mwingi nikiwa na watu but cycle ya watu nilionao nje ya ndugu ni wachache sana hata 7 hawafiki.
Wakati nasoma nilikuwa na marafiki wengi ila sasa muda umepita hatukutani na kila mtu asha move on na maisha yake na hata tukikutana hatuna hata story za kuzungumza.
Marafiki nilionao ninaofanya nao kazi ni marafiki wa kweli hata nikiwa na shida kama kufiwa au tatizo lolote huniunga mkono lakini kuna wakati natamani kuwa na marafiki ambao ni rahisi kujumuika nao katika furaha na wakati wa matatizo.
Hivi wakuu ninaweza kuanzia wapi kutimiza hilo?
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Mimi ni mtu ambaye kazi zangu nyingi nazifanyia ndani nikiwa peke yangu na ninaoshiriikiana nao wengi ni foreigners hivyo kazi tunazifanya na kuzifuatilia kupitia Slack, Hubstaff, Jira n.k. Huku tukishiriki sana Zoom na Google Meet video calls.
Hali hii imenifanya marafiki zangu wengi wawe ni watu walioko mbali lakini marafiki ambao ni rahisi kukutana na kujumuika nao moja kwa moja hasa weekends sina.
Pia mimi si mpenzi wa mpira kihivyo, japo ni shabiki wa yanga lakini ni shabiki wa kufuatilia matokeo tena kupitia kwenye threads humu jamiiforums. Zaidi napenda sana kutazama documentaries mfano True Crimes, Crime report za aljazeera na comedy kidogo hasa Dave Shappelle.
Iikitokea nimetoka sipendi kwenda sehemu zenye kelele, napenda kwenda sehemu zenye watu lakini kuwe kumetulia hakuna muziki mkubwa na makelele.
Pia si mlevi au niseme mnywaji, ikitokea nimekunywa pombe haiwezi kuzidi bia 3 tena lite. Spirits, gin siguzi kabisa.
Yani haya mambo yananifanya nikose marafiki na kuna muda nakuwa natamani kuwa na marafiki nijumuike nao. Siwezi kusema mimi ni introvert kwa sababu nazungumza sana na nina utani mwingi nikiwa na watu but cycle ya watu nilionao nje ya ndugu ni wachache sana hata 7 hawafiki.
Wakati nasoma nilikuwa na marafiki wengi ila sasa muda umepita hatukutani na kila mtu asha move on na maisha yake na hata tukikutana hatuna hata story za kuzungumza.
Marafiki nilionao ninaofanya nao kazi ni marafiki wa kweli hata nikiwa na shida kama kufiwa au tatizo lolote huniunga mkono lakini kuna wakati natamani kuwa na marafiki ambao ni rahisi kujumuika nao katika furaha na wakati wa matatizo.
Hivi wakuu ninaweza kuanzia wapi kutimiza hilo?