Naweza kuongeza somo katika usajili wa CSEE 2016??

Naweza kuongeza somo katika usajili wa CSEE 2016??

UZZIMMA

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2014
Posts
414
Reaction score
483
Kuna ndugu yangu amesajili masomo saba katika CSEE 2016, na hakuweka English. Lengo awe Dokta kwa kuwa miongoni mwa masomo yake anayorisiti ipo Phy, Chem, Math na Biol.

Je naweza kubadili usaji kwa kuongeza English kwa sasa? Japo muda wa marekebisho umeisha?

NB. Naomba nijibiwe kama nilivyouliza tafadhali!
 
ushasema muda umeisha sasa utaongeza vp? kiufup uwez subiri mwakan
 
Kwenda Kuchukua Udoctor Wanaangalia Ufaulu Wa English Form 4 Sasa Kama Alifeli Na Kwenye Kurisiti Hajaweka Bc Mwambie Ajiandae Kurudia Mwaka Mwingne Wa English..
Na Kama Muda Umeisha Bc Hawezi Kusajili Tena
 
ushasema muda umeisha sasa utaongeza vp? kiufup uwez subiri mwakan
Imepita miaka mitatu tangu nitume huu uzi, ila sikuleta marejesho.

Muhusika wa tukio hili ni mimi mwenyewe. Ingawa muda ule mlinikatisha tamaa, ila sikukata tamaa. Nilienda hadi necta nikajieleza nikarekebishiwa. Yaani nikaongezewa somo la english. Na nikafanya mitihani yangu pamoja na english, nikafaulu.
Na sasa nipo chuo naingia mwaka wa tatu.
Wote walionikatisha tamaa katika uzi huu Mungu awabariki.
 
Imepita miaka mitatu tangu nitume huu uzi, ila sikuleta marejesho.

Muhusika wa tukio hili ni mimi mwenyewe. Ingawa muda ule mlinikatisha tamaa, ila sikukata tamaa. Nilienda hadi necta nikajieleza nikarekebishiwa. Yaani nikaongezewa somo la english. Na nikafanya mitihani yangu pamoja na english, nikafaulu.
Na sasa nipo chuo naingia mwaka wa tatu.
Wote walionikatisha tamaa katika uzi huu Mungu awabariki.
Hongera bro[emoji3]
 
Back
Top Bottom