Naweza kumuoa huyu?

Naweza kumuoa huyu?

bujaganoni

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
561
Reaction score
453
Habari wana MMU

Kwanza naomba mnivumilie kwa maelezo marefu.

Anaitwa Romana ndio ninayemuongelea nimekaa naye kwenye mahusiano tangu akiwa form one mim nikiwa form six by then...2009. Tulikuwa tunapendana sana tena sana... japokuwa alipofika 2011 akawa kama amebadilika kipindi hicho mim nilikuwa Chuo DSM yeye yupo Form three MWANZA huko.

Taarifa hizo nilikuwa napewa na rafiki yake kwamba siku hizi anatembea na wanaume wengine japo anasema bado ananipenda. mim nikawa nimechukulia ujana unamsumbua nikamvumilia. sasa huyo rafk yake akawa kila muda anatoa hizo taarifa baadae nikamwambia huyo Romana akakana tena nilivomwambia nineambiwa na rafk yake alitaka hadi kujiua kwa kusingiziwa nakumbuka alikaa wik 2 bila kwenda shule had nikawa naogopa. Bas tuliyaongea yakaisha.

Bahati nzur au mbaya alivomaliza form four alikuja huku DSM kwa mjomba wake kwa hiyo akawa anakuja geto nakumbuka kimbindi hicho nilikuwa nakaa Riverside yeye Majumba Sita (kwa mjomba wake) hiyo ilikuwa 2013. kipindi hicho mim nilikuwa mwaka wa nne chuo. Basi saa zingine alikuwa anakuja tunakaa nae getto kwa siku hata mbili au tatu mfululizo yaan anakuwa amedanganya kwa mjomba ake kwamba anaenda kwa shangaz yake mbez.

Baadae matokeo yao yalitoka akawa kapata IV kwa hiyo hakufanikiwa kuendelea akawa kataftiwa chuo akawa anasoma certificate... katika kusoma huko akawa kapata bwana bhana... mim nikawa nashangaa mawasiliano yamepungua nikijua labda mwenzangu kawa busy na masomo.kwa hiyo sikujal sana... bas nilikuwa nafanya final project ikabid nijikip busy as well.

Baada ya kumaliza chuo nikamuita akaja nikamuulza kwa nn amepunguza nawasiliano akadai mim ndio chanzo kwa kuwa simtafti bas tukayaongea yakaisha... mim nikawa nimemuaga kwamba narud Mwanza kwanza then nitakuja DSM kutafta kazi.

Ilikuwa mwez wa 9, 2013 nilirud DSM kabla sijarud namba yake ikawa haipatikani nikawa naitafta bila mafanikio... nilivofka DSM nikaenda kwa mjomba wake, lkn sikumkuta nikamkuta rafk yake ambaye alinieleza kuwa Romana keshaolewa... yaan niliishiwa hadi nguvu... basi nikawa natafta namba yake bila mafanikio ili nijue sababu za kuniacha... baade nikasikia yupo Mwanza kwao na ana ujauzito.. hiyo ilikuwa 2014 sikutaka kuamini ila huo ndio Ukwel. bas nikawa nimekata tamaa na Romana.

Siku moja nikakutana naye mnaz mmoja hospital akiwa anakaribia kujifungua, nilimuulza ilikuwaje akasema shetani, nikamuulza kwa iyo ushaolewa akadai anakaa naye tu lkn hajajitambulisha kwao basi nikamtakia maisha mema. huku roho ikiwa inaniuma kwa kuwa nampenda.

Bas ikawa hivo sasa cha kushangaza alikuja siku moja akanipigia simu ya kukir kwamba alifanya makosa na akawa anasema mimsamehe, nikamwambia nishasamehe, akadai eti anaishi na mwanaume ambaye hampendi na hawez kuishi na wakati upendo wake uko kwangu eti nimsamehetu turudiane anajuta kwa nin alifanya hivyo.. nahiyo ilikuwa baada ya kusikia kuwa nimeajiriwa... mim nikamwambia kwa kwel aendelee tu na mumewe, bas akawa ananisumbua hivo hivo mim baadae nikahamishwa kikaz nikaenda Dodoma, akaendelea kunisumbua bas nikamwambia sawa, mwez uliopita nimerudishwa hapa DSM tena sasa ndio imekuwa taabu zaidi.

Tangu nirudi amekuwa akitoka kwa bwana yake anakuja kwangu sasa kwa kwel mim nimeshaanza kuogopa... dhumuni lake aivunje ndoa yake ati mim nimuoe, sasa nafikiria kama vile nimejifunga mim mwenyew kumpenda sawa nampenda lkn itakuwaje? Nitaweza kumuoa kwel mtu wa namna hii, na mpaka sasa imefkia hatua anashindwa kukaa kwake eti kisa mumewe hajajitambulisha kwao jaman is it fair? halafu mbona siku hizi nikimuona yaan anachoongea nakubaliana naye kulikoni? nahitaj ushaur kabla sijafanya uamzi wa kijinga.. nampenda sawa lkn ana mtt wa mtu nabado anaishi na huyo mtu japo hajajitambulsha..

Kingine mama yake hataki atoke kwa bwana yake huyo... hajajitakbulisha sawa lakin wazaz wanajua anaishi na bwana kiukwel huwa nataka ninwambie aendelee kuishi naye mume wake nashindwa kwa kuwa nampenda... lkn naona siwez kumuoa sa itakuwaje..? nitatembea na mke wa mtu mpaka lini? nifanyeje nimuache mbona nakuwa sina maamuz juu yake???

naombeni ushaur wenu
 
Huyo mwanamke kakugeuza wewe zombie wake......

Ila jua cha mtu mavi...ngoja mumewe ajue wewe ndio chanzo cha ndoa yake kuvunjika...(ingawa unasema mwanaume hajajitambulisha)

Anyway kama anakupenda sana angehamia kwa mwingine???

Hivi inapokuja swala la mapenzi akili zinawekwa (ga) mfukoni eeeh???
 
Jibu ni kuwa huwezi tena kumuoa kwa kuwa tayari ameshaolewa.

Kama moyo wako unampenda unaweza kuendelea naye, ila at your own risk.

Lakini ni aidha yeye hakupendi au hajui anataka nini au amekosa alichokitarajia kwa hao mabwana wengine. Ila tambua kabisa kuwa wewe kwake ni last option...
 
Huyo mwanamke kakugeuza wewe zombie wake......

Ila jua cha mtu mavi...ngoja mumewe ajue wewe ndio chanzo cha ndoa yake kuvunjika...(ingawa unasema mwanaume hajajitambulisha)

Anyway kama anakupenda sana angehamia kwa mwingine???

Hivi inapokuja swala la mapenzi akili zinawekwa (ga) mfukoni eeeh???

Cheza na papuchi wewe
 
Yaani aliyeumba mbunye haki ya nani alicheza Pele. Mwanaume hata uwe bilionea au msomi na maPh.D kibao mbunye ikikukolea yaani unageuka ---- tu unakosa hata aibu.

Wewe subiri huyo mume mwenzio aje akukamate ndo utakuja kushuhudia vizuri humu. Tena na OFM ya Shigongo iwepo kesho yake ujikute kwenye front page ya Uwazi na kazi ufukuzwe ndo utaelewa. Follow your instincts huku ukilinganisha na utamu wa mbunye yake. Ni lazima ufanye maamuzi magumu ASAP!
 
Yaani wewe ni zombie kwake, umekosea sana kumpa chans ya kuwasiliana na wewe. Ye si alifanya ujinga, mwache ajutie ujinga wake. Na unachokifanya sio fair kwa mwenye mke.

Mtafutie sababu umpige chini, mfano tafuta hata mfanyakaz mwenzio ajifanye mpenzi wako inapendeza awe mzuri kuliko yeye.

Mwisho uache ujinga, na uingineer wako wote unazugwa na papuchi
 
Kumbe kuna watu waji.nga kiasi hiki. Yan mwanamke keshaolewa keshazaa wa nini tena!!! mbona wanawake wako wengi sana mjini humu mkuu.
 
Huyo mwanamke kakugeuza wewe zombie wake......

Ila jua cha mtu mavi...ngoja mumewe ajue wewe ndio chanzo cha ndoa yake kuvunjika...(ingawa unasema mwanaume hajajitambulisha)

Anyway kama anakupenda sana angehamia kwa mwingine???

Hivi inapokuja swala la mapenzi akili zinawekwa (ga) mfukoni eeeh???


Bro ninakushkru sana yaan leo usiku kucha nalifkria hili suala sijawahi kupost JF kitu chochote ila imenibid... kwanza naomba mnisamehe wana jamvi na Mungu aliye juu nakri.kwamba sifanyi fair kwa jamaa yangu na kiukwel ingawa simjui ipo siku ntamtafuta... nafkri nshapata majibu mazur hata haya matusi ninasitahiki sikuwah kuwa na maamuz negative juu yake sijui kaweka nin... leo alikuwa kaniandalia guest huko but from the deepest bottom of my heart ninacomfess mbele ya wasomaji nimekosea mapenz upofu... nitafanya maamz magumu leo.
 
Hivi kwanini hivi vinyago mnavyovichonga baadae vinakuja kuwatisha wenyewe?
 
Jibu ni kuwa huwezi tena kumuoa kwa kuwa tayari ameshaolewa.

Kama moyo wako unampenda unaweza kuendelea naye, ila at your own risk.

Lakini ni aidha yeye hakupendi au hajui anataka nini au amekosa alichokitarajia kwa hao mabwana wengine. Ila tambua kabisa kuwa wewe kwake ni last option...


Ahsante kaka uko sawa kabisa kwa sababu akija anaanza kukupangia mipango mingi sijui kwa kuwa ni mchaga yaan atakupangia vitu vya kufanya.... dah kwel kanigeuza uyu... lkn yote haya huwa nayawaza ila akija kama vile cjui kaniwekea nin
 
Kijana mwenzangu achana nae huyo dada. Mbona wanawake wako wengi tuu na wazuri!! Huyo mwanamke hajitambui mpaka sasa nini anataka. Tafuta mwanamke mwingine halafu kata mawasiliano nae. Hiyo ndo njia pekee ya kumsahau. Ila sema na moyo wako kwanza. Uamuzi unao wewe. Sisi tuna kushauri tuu.
 
Mmmmhhmm tuko wengi kumbe!!!

Kaka nimeshafanya kuifuta namba yake kwa mufa kama wa wiki lakin alivonitafuta yaan nikawa nimeshasahau kila kitu... inanisikitisha sana kwa nin sina maamuz juu ya hili hata kama nampenda why nikimfikria nasahau ujinga ninaoufanya dah very sad aiseee!
 
Kwa maelezo yako huyo dada anaonekana ni mcharuko. Hajatulia na ukimuoa ujue lazima atakuwa na mwanamme nje kama anavyofanya sasa. Hivyo ujiandae kuchapiwa na wewe. Kata mawasiliano nae na ikiwezekana hata namba yako ya simu badilisha na usimkaribishe tena nyumbani kwako.
 
Kwa maelezo yako huyo dada anaonekana ni mcharuko. Hajatulia na ukimuoa ujue lazima atakuwa na mwanamme nje kama anavyofanya sasa. Hivyo ujiandae kuchapiwa na wewe. Kata mawasiliano nae na ikiwezekana hata namba yako ya simu badilisha na usimkaribishe tena nyumbani kwako.

Ahsante kaka
God bless you!
 
Huyo mwanamke kakugeuza wewe zombie wake......

Ila jua cha mtu mavi...ngoja mumewe ajue wewe ndio chanzo cha ndoa yake kuvunjika...(ingawa unasema mwanaume hajajitambulisha)

Anyway kama anakupenda sana angehamia kwa mwingine???

Hivi inapokuja swala la mapenzi akili zinawekwa (ga) mfukoni eeeh???

Nimekuelewa mno mkuu...
Mda mwingine tunalalamika kuwa na matatizo huku tukiwa tumeyakumbatia
 
Back
Top Bottom