Naweza kulipwa hela yangu yote NSSF?

Naweza kulipwa hela yangu yote NSSF?

Ngimwike Paul

Member
Joined
Dec 30, 2024
Posts
9
Reaction score
3
Niliajiriwa kwenye kampuni binafsi kama tally clerk na baadae nikajifunza funza wakani badilisha position nikawa nafanya kama Data entry Clerk na jumla kazi nilifanya kwa miaka 5

Mwaka huu mwezi wa 6 mkataba umeisha na nikaamua kufungua madai nssf na kukamilisha mchakato wote na kutia fingerprint, wkt nasubiria mambo yakae sawa nssf wakapiga simu kwa mwajiri kumuuliza elimu yangu, muajiri akajibu nimeishia level ya cheti na ni kweli nimeishia cheti japo kazini niliingia kama form 4 na kule kwenye document za nssf nilijaza elimu yangu ni form 4

So kwa hapo wadau mnaonaje ninaweza kulipwa hela zangu zote kama unskilled au watanilipa kama professional yaani ile 33.3% natakiwa nifanye nn wadau naombeni mawazo na maoni yenu

Screenshot_20251017-141751.png
 
Unafikiri kwa nn walimuuliza hr wako? Wanajua huwa mnadanganya elimu mnapo-process mafao. Kama hr ameconfirm ni you were skilled labour jiandae kuchukua 33.3 then subiri miezi 18 kama hujaajiriwa ndio upate mpunga wako wote.

yani hela ni yangu na nalazimishwa kutunziwa. Siku nikihitaji napewa 33.3% tena bila riba
 
Unatakiwa kupewa pesa yako yote .... harafu hao NSSSF kwa nini hawakudili na nyaraka za ufunguzi wa madai mpaka warudi kwa mwajiri.?
 
Subiri kabla mwezi huu haujaisha utapata message ya benki. Hilo halitazuia kulipwa hela yako yote
 
Unafikiri kwa nn walimuuliza hr wako? Wanajua huwa mnadanganya elimu mnapo-process mafao. Kama hr ameconfirm ni you were skilled labour jiandae kuchukua 33.3 then subiri miezi 18 kama hujaajiriwa ndio upate mpunga wako wote.
Certicate holder nakuaje skilled kiongozi??
 
Certicate holder nakuaje skilled kiongozi??
Unaelewaje kuhusu skilled? (Ujuzi wa kazi). A certificate holder can be skilled in specialized field eg masonry, welding, driving etc. Usikariri mpaka uwe na masters or phd ndio uwe skilled laborer. Kiufupi ujuzi wa kazi ni uzoefu kwa kitu ulichosomea na kugraduate katika level yoyote.
 
Unafikiri kwa nn walimuuliza hr wako? Wanajua huwa mnadanganya elimu mnapo-process mafao. Kama hr ameconfirm ni you were skilled labour jiandae kuchukua 33.3 then subiri miezi 18 kama hujaajiriwa ndio upate mpunga wako wote.
33.3% ni lump sum money au watakulipa asilimia hizo 33.3 kwa mishahara yako mitatu ya mwisho?
 
Andaa siku nzima na document zote mkabishane pale hadi wakubali.
Unnashindwa wapi tununu? Usiniletee balaa baba yako
 
Back
Top Bottom