Nawashangaa sana wanaofurahia ya EU

Nawashangaa sana wanaofurahia ya EU

JF Member

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2014
Posts
8,204
Reaction score
11,364
Kwanza niwaambie tu kama raia lazima ulinde uhuru wa nchi yako. Kuruhusu hawa wazungu waingilie mambo ya ndani ya hawana cha kupoteza kwa lolote. Pale Libya kwa mfano walipofanikiwa kuwaingia raia baada ya kushidwa kulinda uhuru wao hadi sasa mnajua yaliyopo la sivyo tunataka kuugawa uhuru wetu.

Hii kitu inayoendelea haiwezi fanywa na wazungu iwapo kila mtanzania ataamua kulinda uhuru wa nchi.

Kuna wanasiasa ukiwaangalia kabisa hawafai hata kuingia mlango wa ikulu ama wa bungeni maana wanainajisi nchi yetu na wanashindwa kulinda uhuru wa nchi yetu kwa sasabu za njaa zao.

Baada ya kupata uhuru mwaka 1961 sasa ni zamu ya kujenga nchi. Kila mmoja anajua jinsi sasa hivi nchi yetu inajitahidi kujenga miundo mbinu ya uchumi hapa hakuna wa kupinga maana kazi inapigwa kweli kweli. Cha mshingi tujenge nchi.

Pili baada ya uchaguzi wa 2015 ifahamike kwamba ccm iligawanyika sana - Timu Lowasa na Timu Membe zilimtesa sana JK na baada ya JPM kuingia madalakani kila mmoja alijua hataiweza ccm. Ni kweli kwamba JPM amejitahi sana kwa kiasi cha kukimudu kiti cha uenyekiti ambapo JK alikuwa anapotezea bila kuchukua hatua. Sasa hivi ccm bado inapitia kwenye kipindi cha 2015 - Timu Membe na Timu Lowasa bado zinatamani zipate urais eiza kupitia wenyewe moja kwa moja ama zitumie mwamvuli wa majina ya hao wawili.

Pamoja na mapungufu ya aliyo nayo JPM lakini anatimiza yale aliyotuahidi wapiga kura wake mwaka 2015 -- Mlioshindwa subirini 2020 mje muuze sera zenu tumuache Rais atufanyie kazi. Pigeni kelele bungeni.

Naamini JPM atamilizana na Wazungu na ataendeleea naujenzi wa nchi bila kuyumbishwa.

Mungu ibariki TZ.
 
Umezungumzia watu badala ya matatizo yanayodaiwa na EU pamoja US !! eg Team Membe, Team Lowassa, Maghufuli nk, badala kujadili hoja zilizoletwa mezani na hao jamaa !!!!

1. Je u dictator upo au haupo. Na unauelewa ?!
2. Je sheria kandamizi za mitandao, takwimu , vyama, nk zipo ?!
3. Ni kweli watu wanatekwa na kupotezwa ?!
4. Je Makonda aliwatishia amani mashoga na wasagaji ?!
5. Je viongozi wa upinzani wanabambikiwa kesi ?!. eg kuuawa kwa Akwilina.
6. Je vyama tofauti na CCM vinakandamizwa kufanya siasa ?!

Unapiwalaani wanaounga mkono hao mnaowaita ma beberu. Tafakari kama serikali nayo iko fair kwa watu wa kada zote. Kama wana mipango inayokandamiza wengine kwa maslahi yao ya kisiasa then hauko sawa. Tuwe na utaratibu ulio sawa kwa wote .
 
Hata sisi tunakushangaa wewe usiyejua hatari tuliyonayo. Chief Whip wa upinzani kupigwa risasi nje ya nyumba za bunge, miili ya watu kuokotwa Coco Beach, watu kupotea, kubanwa uhuru wa kujieleza, kiongozi mkuu wa upinzani kuwekwa ndani.
 
Kwanza niwaambie tu kama raia lazima ulinde uhuru wa nchi yako. Kuruhusu hawa wazungu waingilie mambo ya ndani ya hawana cha kupoteza kwa lolote. Pale Libya kwa mfano walipofanikiwa kuwaingia raia baada ya kushidwa kulinda uhuru wao hadi sasa mnajua yaliyopo la sivyo tunataka kuugawa uhuru wetu.

Hii kitu inayoendelea haiwezi fanywa na wazungu iwapo kila mtanzania ataamua kulinda uhuru wa nchi.

Kuna wanasiasa ukiwaangalia kabisa hawafai hata kuingia mlango wa ikulu ama wa bungeni maana wanainajisi nchi yetu na wanashindwa kulinda uhuru wa nchi yetu kwa sasabu za njaa zao.

Baada ya kupata uhuru mwaka 1961 sasa ni zamu ya kujenga nchi. Kila mmoja anajua jinsi sasa hivi nchi yetu inajitahidi kujenga miundo mbinu ya uchumi hapa hakuna wa kupinga maana kazi inapigwa kweli kweli. Cha mshingi tujenge nchi.

Pili baada ya uchaguzi wa 2015 ifahamike kwamba ccm iligawanyika sana - Timu Lowasa na Timu Membe zilimtesa sana JK na baada ya JPM kuingia madalakani kila mmoja alijua hataiweza ccm. Ni kweli kwamba JPM amejitahi sana kwa kiasi cha kukimudu kiti cha uenyekiti ambapo JK alikuwa anapotezea bila kuchukua hatua. Sasa hivi ccm bado inapitia kwenye kipindi cha 2015 - Timu Membe na Timu Lowasa bado zinatamani zipate urais eiza kupitia wenyewe moja kwa moja ama zitumie mwamvuli wa majina ya hao wawili.

Pamoja na mapungufu ya aliyo nayo JPM lakini anatimiza yale aliyotuahidi wapiga kura wake mwaka 2015 -- Mlioshindwa subirini 2020 mje muuze sera zenu tumuache Rais atufanyie kazi. Pigeni kelele bungeni.

Naamini JPM atamilizana na Wazungu na ataendeleea naujenzi wa nchi bila kuyumbishwa.

Mungu ibariki TZ.

Uzalendo ni muhimu kwa kila mtanzania lakini uzalendo hauji kama mvua yakupewa na Mungu
 
Umezungumzia watu badala ya matatizo yanayodaiwa na EU pamoja US !! eg Team Membe, Team Lowassa, Maghufuli nk, badala kujadili hoja zilizoletwa mezani na hao jamaa !!!!

1. Je u dictator upo au haupo. Na unauelewa ?!
2. Je sheria kandamizi za mitandao, takwimu , vyama, nk zipo ?!
3. Ni kweli watu wanatekwa na kupotezwa ?!
4. Je Makonda aliwatishia amani mashoga na wasagaji ?!
5. Je viongozi wa upinzani wanabambikiwa kesi ?!. eg kuuawa kwa Akwilina.
6. Je vyama tofauti na CCM vinakandamizwa kufanya siasa ?!

Unapiwalaani wanaounga mkono hao mnaowaita ma beberu. Tafakari kama serikali nayo iko fair kwa watu wa kada zote. Kama wana mipango inayokandamiza wengine kwa maslahi yao ya kisiasa then hauko sawa. Tuwe na utaratibu ulio sawa kwa wote .
Kuna sababu nyingine wala huhitaji nguvu kusema.

Swala la msingi ni je ? Hayo madai yako unahitaji yakamilike yote? Unahisi ni nchi gani ziko huru kama unavyo unavyo zani? Kuna mtu kasingiziwa kesi bila kuambiwa alichokosea? Hakuna sehemu iliyo kamili kama unavyotaka ndugu. Cha msingi tujenge nchi yetu wenyewe . JPM atapita nawe utapewa madaraka uongoze kama unayataka.
 
Hata sisi tunakushangaa wewe usiyejua hatari tuliyonayo. Chief Whip wa upinzani kupigwa risasi nje ya nyumba za bunge, miili ya watu kuokotwa Coco Beach, watu kupotea, kubanwa uhuru wa kujieleza, kiongozi mkuu wa upinzani kuwekwa ndani.
Kwa kutaka kuiangamiza TZ kwa wazungu nawapigwe tu hizo risasi.. Watu badala ya kutetea misingi ya nchi wanatetea misingi ya wawekezaji wa kibeberu.
 
Kuna sababu nyingine wala huhitaji nguvu kusema.

Swala la msingi ni je ? Hayo madai yako unahitaji yakamilike yote? Unahisi ni nchi gani ziko huru kama unavyo unavyo zani? Kuna mtu kasingiziwa kesi bila kuambiwa alichokosea? Hakuna sehemu iliyo kamili kama unavyotaka ndugu. Cha msingi tujenge nchi yetu wenyewe . JPM atapita nawe utapewa madaraka uongoze kama unayataka.
hovyooooo
 
Mimi. Nionavyo mambo ya EU. Na kuingilia utawala wetu inatokana. Na serikali yetu kutokua wavumilivu hawa wapinzani kila wanalofanya wanawekwa ndani. Mbona tawala zilizopita walikua wanahangaika sana lakini serikali iliwachukulia poa na mambo yakaenda .lakini kwa sasa wanabinnywa kwa kila namna wakiwa na vikao vyao vya ndani wanakamatwa mbona ccm wanafanya vyao anawakamata nani? Tawala zote ziliwapotezea wapinzani na mambo yalienda vizuri lakini awamu hii INA hofu za kijinga kabisa dhidi ya opposition.
 
Wapo waliopo magerezani zaidi ya miaka kwa kesi za uchochezi
Na hawajafunguliwa mashtaka nini? Hii
Nani uko magereza kwa miaka ndugu? Wote walishitakiwa malishahukumiwa na wangine walishamaliza vifungo vyao.
 
Mimi. Nionavyo mambo ya EU. Na kuingilia utawala wetu inatokana. Na serikali yetu kutokua wavumilivu hawa wapinzani kila wanalofanya wanawekwa ndani. Mbona tawala zilizopita walikua wanahangaika sana lakini serikali iliwachukulia poa na mambo yakaenda .lakini kwa sasa wanabinnywa kwa kila namna wakiwa na vikao vyao vya ndani wanakamatwa mbona ccm wanafanya vyao anawakamata nani? Tawala zote ziliwapotezea wapinzani na mambo yalienda vizuri lakini awamu hii INA hofu za kijinga kabisa dhidi ya opposition.
Hayo yote tuliyaomba sana wakati wa JK tukapata mtu tukamwambia hatutaki achekecheke. Mengine ni ya kujitakia mfano Mbowe kaitwa mahakamani kaanza kulandalanda mara south mara ubeligiji wakati anajua anatakiwa mahakamani.
 
Kwanza niwaambie tu kama raia lazima ulinde uhuru wa nchi yako. Kuruhusu hawa wazungu waingilie mambo ya ndani ya hawana cha kupoteza kwa lolote. Pale Libya kwa mfano walipofanikiwa kuwaingia raia baada ya kushidwa kulinda uhuru wao hadi sasa mnajua yaliyopo la sivyo tunataka kuugawa uhuru wetu.

Hii kitu inayoendelea haiwezi fanywa na wazungu iwapo kila mtanzania ataamua kulinda uhuru wa nchi.

Kuna wanasiasa ukiwaangalia kabisa hawafai hata kuingia mlango wa ikulu ama wa bungeni maana wanainajisi nchi yetu na wanashindwa kulinda uhuru wa nchi yetu kwa sasabu za njaa zao.

Baada ya kupata uhuru mwaka 1961 sasa ni zamu ya kujenga nchi. Kila mmoja anajua jinsi sasa hivi nchi yetu inajitahidi kujenga miundo mbinu ya uchumi hapa hakuna wa kupinga maana kazi inapigwa kweli kweli. Cha mshingi tujenge nchi.

Pili baada ya uchaguzi wa 2015 ifahamike kwamba ccm iligawanyika sana - Timu Lowasa na Timu Membe zilimtesa sana JK na baada ya JPM kuingia madalakani kila mmoja alijua hataiweza ccm. Ni kweli kwamba JPM amejitahi sana kwa kiasi cha kukimudu kiti cha uenyekiti ambapo JK alikuwa anapotezea bila kuchukua hatua. Sasa hivi ccm bado inapitia kwenye kipindi cha 2015 - Timu Membe na Timu Lowasa bado zinatamani zipate urais eiza kupitia wenyewe moja kwa moja ama zitumie mwamvuli wa majina ya hao wawili.

Pamoja na mapungufu ya aliyo nayo JPM lakini anatimiza yale aliyotuahidi wapiga kura wake mwaka 2015 -- Mlioshindwa subirini 2020 mje muuze sera zenu tumuache Rais atufanyie kazi. Pigeni kelele bungeni.

Naamini JPM atamilizana na Wazungu na ataendeleea naujenzi wa nchi bila kuyumbishwa.

Mungu ibariki TZ.
Wewe ni raia mwema na mzuri.
Linda Sana uhuru wako na nchi.
Kama JPM anamapungufu chukua mafuta nenda ikulu kaiwashe moto.
Kati ya watu milioni 50 lazima kutakua na mzuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom