Nawaombeni ushauri kuhusu huyu mtoto

Nawaombeni ushauri kuhusu huyu mtoto

kamanyora

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2013
Posts
209
Reaction score
134
Baada ya kumaliza shule nilimpa girlfriend wangu mimba,baadae tulitengana nikamuacha akiwa na mimba ya miezi 7 mm nikaenda masomoni nchini kenya na yeye baadae alitoka kuja dsm kwa dadake,toka hapo tulipotezana,akiwa kwa dadake dar alijifungua mtoto wa kike baada ya kujifungua alikaa kwa mda wa miaka 3 akatokea jamaa mmoja akamuoa na yule mtoto,mwaka jana kwa mara ya kwanza alinipigia cm (cjui namba alipata wapi) akiniambia unajua kama nilikuwa na mwanao?nikamjibu najua,alimueleza na mtoto ukweli wote na kumpa no yangu toka hapo mtoto ananilalamikia anavyoteswa,mama yake alifanya mpango akamtoa mtoto na kumpakiza kwenye gari toka arusha kuja kwangu dar nae akaja tukaandikishana mahakamani kwamba amenikabidhi mtoto(kumbuka alimtoa bila mwanamme kujua)akamwacha mtoto kwangu yeye akarudi arusha kwa mumewe mimi nikamuingiza mtoto shule(yuko form 2),alivyofika kwa mumewe akaanza kumtisha kwamba atamkata mapanga asiporudisha mtoto,mwanamke akanipigia cm kunibembeleza nimrudishie mtoto ili anusuru ndoa yake,nilivyo mwambia mtoto kurudi alikataa kata kata kwamba amechoka na manyanyaso na hawezi kurudi,nilmdanganya kwamba aende atarudi baada ya mwezi toka alivyoenda ananipigia cm akilia na kulalamika kwamba yeye anataka aje kwa baba yake yani kwangu.je nifanye nini?


mtoto ana miaka 16
 
++
Damu ya ulimi haitemwi Inamezwa.
I mean hatima ya mwanao ipo mikononi mwako.
Chukua mtoto Asiendelee kuwa kinga ya ndoa nyingine.
++
 
++
Damu ya ulimi haitemwi Inamezwa.
I mean hatima ya mwanao ipo mikononi mwako.
Chukua mtoto Asiendelee kuwa kinga ya ndoa nyingine.
++
tatizo yule mwanamke amekuwa muoga kwa vitisho vya mume wake na mwanaume nae hataki mtoto aondoke
 
kwani huko hajazaa na huyo mume wake mpaka jamaa ang'ang'anie huyo mtoto wako? au jamaa ana tabia chafu anafanya kwa mwanao ebu peleleza
 
kwani huko hajazaa na huyo mume wake mpaka jamaa ang'ang'anie huyo mtoto wako? au jamaa ana tabia chafu anafanya kwa mwanao ebu peleleza
mzabzab unachosema ndicho alichoniambia huyo mtoto kwamba kuna siku jamaa alimfungia mlango akitaka kumpiga lakini bahati nzuri majirani walimsaidia,huyo mama amezaa watoto wengine watatu na huyo bwana,amemwambia mkewe kwamba huyo mtoto akitoka ajiandae kupewa talaka na mwanamke anaogopa kuachika,na pia alidai mtoto akija kwangu ataenda polisi kuripoti kaibiwa,na swala la kuelewana angalau nimlipe garama alizotumia kama ndo zinamsumbua pia hataki
 
tatizo yule mwanamke amekuwa muoga kwa vitisho vya mume wake na mwanaume nae hataki mtoto aondoke

++
kamanyora
Kuna mambo mawili hapo ninayoyaona
1.
Mumewe huyo aliyekuwa mwenzi wako anamtumia mwanao kama silaha ya kukaa na mke.Hataki waacheni maana huyo mwanamke anajua siri zake nyingi.Na hata huo ukali ni defencisive mechanism ya kuficha udhaifu wake.
2.
Wewe na huyo mwanamke bado mnapendana.Na mtoto mnamtumia kama kura ya VETO jambo linalomuumiza mtoto na sio nyie.
++
USHAURI
Simama kama mwanaume kamili aidha umchukue mtoto hata kama ndoa yake itavunjika Ama umuache mtoto ili akikua awe na hiari ya kukukana au kukusamehe kwa uzembe wa kumtetea.
++
 
Last edited by a moderator:
Mwanao, mwanao tu! Ulivyomtesa inatosha! Fuata sheria ukachukue mwanao!

ww wataka watu wakulele mwanao, ajabu ya Mussa hii.....
 
Kama mliandikishana mahakaman it means kuwa inajulkana kisheria kuwa ni mwanao, so tumia sheria hyohyo kuwa na mwanao badala ya kuacha mtoto aendlee kuteseka.
 
Baada ya kumaliza shule nilimpa girlfriend wangu mimba,baadae tulitengana nikamuacha akiwa na mimba ya miezi 7 mm nikaenda masomoni nchini kenya na yeye baadae alitoka kuja dsm kwa dadake,toka hapo tulipotezana,akiwa kwa dadake dar alijifungua mtoto wa kike baada ya kujifungua alikaa kwa mda wa miaka 3 akatokea jamaa mmoja akamuoa na yule mtoto,mwaka jana kwa mara ya kwanza alinipigia cm (cjui namba alipata wapi) akiniambia unajua kama nilikuwa na mwanao?nikamjibu najua,alimueleza na mtoto ukweli wote na kumpa no yangu toka hapo mtoto ananilalamikia anavyoteswa,mama yake alifanya mpango akamtoa mtoto na kumpakiza kwenye gari toka arusha kuja kwangu dar nae akaja tukaandikishana mahakamani kwamba amenikabidhi mtoto(kumbuka alimtoa bila mwanamme kujua)akamwacha mtoto kwangu yeye akarudi arusha kwa mumewe mimi nikamuingiza mtoto shule(yuko form 2),alivyofika kwa mumewe akaanza kumtisha kwamba atamkata mapanga asiporudisha mtoto,mwanamke akanipigia cm kunibembeleza nimrudishie mtoto ili anusuru ndoa yake,nilivyo mwambia mtoto kurudi alikataa kata kata kwamba amechoka na manyanyaso na hawezi kurudi,nilmdanganya kwamba aende atarudi baada ya mwezi toka alivyoenda ananipigia cm akilia na kulalamika kwamba yeye anataka aje kwa baba yake yani kwangu.je nifanye nini?


mtoto ana miaka 16
MTUMIE NAULI ATOROKE AJE KWAKO... mIAKA 16 ANA UWEZO WA KUKUFUATA POPOTE
 
Kwanini huyo mume mwenzio ang,ng,ane na mwanao? Je anataka umlipe gharama alitumia juu ya mwanao? Kama sio gharama basi kuna kitu nyuma ya pazia.
 
mzabzab unachosema ndicho alichoniambia huyo mtoto kwamba kuna siku jamaa alimfungia mlango akitaka kumpiga lakini bahati nzuri majirani walimsaidia,huyo mama amezaa watoto wengine watatu na huyo bwana,amemwambia mkewe kwamba huyo mtoto akitoka ajiandae kupewa talaka na mwanamke anaogopa kuachika,na pia alidai mtoto akija kwangu ataenda polisi kuripoti kaibiwa,na swala la kuelewana angalau nimlipe garama alizotumia kama ndo zinamsumbua pia hataki

hivi huyo ni mwanao kweli?

Mbona kama hauna uchungu?

Kwanini unaruhusu mwanao awe kinga kwenye ndoa ambayo haina furaha wala amani?

Au unamuonea mzazi mwenzio huruma ya kudundwa wakati mwanao pia anasulubiwa ipasavyo?

Nahisi wewe ni wale wanaume wapole.....!!!!

Copy to Himidini
 
mi mwenyewe naona hata we mwenyewe haupo sawa sawa, Hivi wewe ni baba gani ambaye huna hatachembe ya uchungu, huruma, kujali na kufikiri??????Mtoto ameshakudokezea kinachoendelea kati ya huyo Baba wa kambo, Unataka usikie amebakwa au ana mimba ndo utachukua hatua, au ulitaka akwambie aje???? uelewe mambo mengine yanachefua saana, mfyuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!!!!!!
 
tatizo yule mwanamke amekuwa muoga kwa vitisho vya mume wake na mwanaume nae hataki mtoto aondoke
Kwani huyo mwanaume anamng'ng'ania kwa kigezo gani? Kwani Alioa mama au mtoto au vyote viwili. Kisheria mtoto anayezidi miaka 7 anachagua akae na Mzazi yupi baada ya wazazi kutengana, unless Mzazi anayependwa kuishi na mtoto Hana uwezo kabisa wa kumtunza. Lakini na wewe Nadhani una matatizo yako, ukamtoe mtoto wako ateseke eti kulinda ndoa ya mwingine?! Una lako jambo wewe
 
Kwani huyo mwanaume anamng'ng'ania kwa kigezo gani? Kwani Alioa mama au mtoto au vyote viwili. Kisheria mtoto anayezidi miaka 7 anachagua akae na Mzazi yupi baada ya wazazi kutengana, unless Mzazi anayependwa kuishi na mtoto Hana uwezo kabisa wa kumtunza. Lakini na wewe Nadhani una matatizo yako, ukamtoe mtoto wako ateseke eti kulinda ndoa ya mwingine?! Una lako jambo wewe
ushauri wenu nimeuelewa nashukuru ila kuna jambo moja ambalo naomba nijuzwe kwa anaejua,je nikimtumia mtoto nauli akatoroka akaja alafu yule mwanaume akaenda labda polisi akatoa taarifa kwamba mtoto amepotea baadae akapatikana kwangu je hii haiwezi kuleta shida? ndio hofu yangu
 
Kwanini huyo mume mwenzio ang,ng,ane na mwanao? Je anataka umlipe gharama alitumia juu ya mwanao? Kama sio gharama basi kuna kitu nyuma ya pazia.
ndio hicho kinachonishangaza hataki kabisa hata habari ya kuambiwa garama kitu ambacho mm nilikuwa tiari kutoa garama
 
Fuata taratibu mchukue mwanao. Kwanini alazimishe kukaa na mtoto wakati anamtesa? Lazima kuna namna hapo!
 
Kama mliandikishana mahakaman it means kuwa inajulkana kisheria kuwa ni mwanao, so tumia sheria hyohyo kuwa na mwanao badala ya kuacha mtoto aendlee kuteseka.
asante
 
Back
Top Bottom