Nauliza: Kwanini Uingereza wanatishia kujitoa EU?

Nauliza: Kwanini Uingereza wanatishia kujitoa EU?

tutafikatu

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2011
Posts
3,399
Reaction score
4,732
Wabobezi wa masuala ya kimataifa, najiuliza kwanini Uingereza anawatishia wenzake (kwa kweli yupo serious sana) kwamba atajitoa EU? Na kwanini members wengine wa EU wanaendelea kuwabembeleza?
Ni vizuri ukioanisha majibu yako na JMT na SMZ, ingawa kuna utofauti wa kimuundo.
 
Uingereza imechoka kuburuzwa na Euro ingawa walijiunga nao na wakakataa kutumia € na wakaendelea na £ UK wanataka wasiingiliwe kuhusu uchumi (fair enough) pili ni single market na tatu suala la uhamiaji muungano unataka wahamiaji wa nchi hizo pindi wanapofika nchi zingine (eurozone) waanzishiwe hela za kujikimu lakini UK wanataka wapatiwe baada ya miaka minne (ambapo naona wameafikiana kwa hilo na lingine ambalo Cameroon anataka ni kuwa na Uhuru wa kufanya biashara na USA na Asia
 
Sina ninalo lijua ila kwa hili la kufananisha EU na JMT ,SMZ sijui kama vitakupa majibu unayo yataka ,Labda mfano ungekua wa Scotland kujiondoa UK kidogo ingeleta maana ya JMT na SMZ
Kujiondoa EU kwa Uingereza ni sawa tu na Tanzania kujitoa EAC
 
Ni haki hata wazanzibar kujitoa, kwa wale wanaojielewa.
Naona ni haki yao na kama kujitoa wangepiga kura labda kama Scotland ingawa walipenda kujitoa lakini kura zikapigwa mwishowe wakapewa wengi.

Labda na Zanzibar wangefanyiwa hivyo
 
Yaah cuf walisajesti hivyo tupige kura lakini wahafaidhina ndo shida.
 
Hilo la kujitoa kwa uingereza sijajua ila kwa SMZ naomba wajitoe tu maana hawana faida yoyote, umeme unatoka bara,chakula kinatoka bara, ajira asilimia kubwa wanaajiliwa huku bara wanabana naasi za wanetu, mishahara inatoka bara, bajeti yao inatoka bara. Wajitoe tu maana tumewachoka
 
Hilo la kujitoa kwa uingereza sijajua ila kwa SMZ naomba wajitoe tu maana hawana faida yoyote, umeme unatoka bara,chakula kinatoka bara, ajira asilimia kubwa wanaajiliwa huku bara wanabana naasi za wanetu, mishahara inatoka bara, bajeti yao inatoka bara. Wajitoe tu maana tumewachoka
Ila kumbuka kuwa kule kuna madem wenye mambo fulani hivi amazing!!
 
Pia waingereza Ni very selfish, wanajionaga nchi yao imejaa "maziwa na asali". Wamezoea nchi yao ilikuwa na identity ya kipekee lkn baadae wakaona inamezwa na Euro ndio maana wanapiga kelele halafu walivyo wajinga wanasema nchi yao Ni kisiwa kidogo sana wanaogopa kisije zama kwa wingi wa watu
 
Wamepima na wakaona faida wanayoipata ni ndogo kuliko hasara.

Wakaona bora watoke.
 
Vurugu imeanza na single currency ya euro
hiyo sarafu inaweza kupoteza thamani hata kwa sababu za uchumi wa nchi kama
Ugiriki au Spain na kadhalika
kwa ufupi nchi yoyote mwanachama anaweza leta vurugu ya kiuchumi
hasa kwa hiyo sarafu

Na waingereza wanajivunia sana sarafu yao ndo maana walikataa kujiunga na euro
baada ya hapo mambo mengi yanajitokeza yanapelekea kuona ni bora wajitoe

Laiti EU ingekuwa zile nchi chache imara kiuchumi Uingereza asingejitoa
lakini ukichanganya na nchi gonjwa kama Ugiriki na zingine shida inaanzia hapo

Sisi tunapaswa mno kujifunza na kukataa kabisa EAC single currency ambayo Kenya
wanataka kuitumia kutuingiza mkenge

Sababu bank kuu ya EAC itakuwa controled na Wakenya na kama niko right head office itakua Nairobi...
hapo ndo tutakapo umizwa

thamani ya fedha yetu kuwa ndogo inatupa advantage kwa baadhi ya bussiness
hata utalii pia...single currency itatuumiza sana
na hatusikiii.......Rala akimshawishi Magufuli we are done
 
thamani ya fedha yetu kuwa ndogo inatupa advantage kwa baadhi ya bussiness
hata utalii pia...

Binafsi naumizwa sana na udogo wa thamani wa hela yetu. Hata kwa position ya nchi kwa sasa hakuna faida kwa hela yetu kuwa na thamani ndogo, ni eneo hilo tu la utalii linaweza kuhesabu faida.
Kama tungekuwa ni nchi inayozalisha bidhaa kwa wingi na ku export hakika tungeona manufaa.
 
Nahisi kama Mwingereza anamhofia Mjerumani hivi ndani ya huo muungano maana Mjerumani yupo vizuri kiviwanda kuliko nchi nyingine za Ulaya,Ulaya naweza kugeuka kuwa soko lake tu.
Wabobezi wa masuala ya kimataifa, najiuliza kwanini Uingereza anawatishia wenzake (kwa kweli yupo serious sana) kwamba atajitoa EU? Na kwanini members wengine wa EU wanaendelea kuwabembeleza?
Ni vizuri ukioanisha majibu yako na JMT na SMZ, ingawa kuna utofauti wa kimuundo.
 
Vurugu imeanza na single currency ya euro
hiyo sarafu inaweza kupoteza thamani hata kwa sababu za uchumi wa nchi kama
Ugiriki au Spain na kadhalika
kwa ufupi nchi yoyote mwanachama anaweza leta vurugu ya kiuchumi
hasa kwa hiyo sarafu

Na waingereza wanajivunia sana sarafu yao ndo maana walikataa kujiunga na euro
baada ya hapo mambo mengi yanajitokeza yanapelekea kuona ni bora wajitoe

Laiti EU ingekuwa zile nchi chache imara kiuchumi Uingereza asingejitoa
lakini ukichanganya na nchi gonjwa kama Ugiriki na zingine shida inaanzia hapo

Sisi tunapaswa mno kujifunza na kukataa kabisa EAC single currency ambayo Kenya
wanataka kuitumia kutuingiza mkenge

Sababu bank kuu ya EAC itakuwa controled na Wakenya na kama niko right head office itakua Nairobi...
hapo ndo tutakapo umizwa

thamani ya fedha yetu kuwa ndogo inatupa advantage kwa baadhi ya bussiness
hata utalii pia...single currency itatuumiza sana
na hatusikiii.......Rala akimshawishi Magufuli we are done
Well said mkuu ,haya alishayaongeleaga jk kipindi kile cha coewl,hata ardhi kwao adimu,hatuwezi kuingia mkenge,wanajua hilo,ndio kama ilivyo UK.
 
Back
Top Bottom