Franky
JF-Expert Member
- Apr 27, 2012
- 2,038
- 2,247
Wanaume tuna kazi kubwa sana, usimshangae mwanaume anaongea mwenyewe barabarani.
Mwanamke atataka care, uwe karibu nae muda wote na hapo hapo atataka pesa, mara umkojoleshe, saivi tena wanataka mshahara.
Bado kuna watoto wanakusubiri ulipe ada na matumizi ya nyumbani, hapo mwenye nyumba anakusubiri, mara sijui kuna kwenda saloon akasuke, bado kuna nguo mpya imetoka amemuona shoga yake amevaa na yeye anataka.
Bado kijijini mama na baba yako wanakutegemea washazeeka, bado kuna ndugu wanahitaji support yako.
Bado kuna starehe zinakusubiri, mara umepita instagram umekutana na aisha nyigu, yaani ni tabu tupu wakuu.
Hizi stress watu wengine mnazitolea wapi aisee?? Fanya kazi pata kipato chako furahia maisha yako, mambo ya nyumbani wazee wamezeeka wanakutegemea Wewe ni kujitwisha kazi za Mungu na serikali Ndio maana wazungu wazee Kama hao wanawapeleka foster homes sio kwamba hawana akili! Muda wa kujijenga unautoa wapi ukibeba mzigo wote huo? Tunza watoto wako huo Ndio wajibu wako!