Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 13,625
- 29,891
Napenda kutoa Rai kwa heshima na Taadhima kwa Watanzania. Tumuunge mkono Kapten Tesha. Natamani haraka sana nije Tanzania. Natamani sana. Nimemsikiliza machozi yamenitoka.
Huyu Kapten anajua vizuri hatari ambayo inamkabili baada ya hili. Anajua vizuri changamoto ambazo atakumbana nazo. Ameamua kumfunga paka kengele. Huyu ni mmoja ya Wazalendo wakubwa wa hii nchi. Tafadhali nawaomba Watanzania bila kujali vyama, dini na rangi au njaa na matumbo yetu. Tumuunge mkono.
SAA YA UKOMBOZI NI SASA. Miaka mingi sisi tumeshiriki kuifisadi hii nchi na kujineemesha wenyewe na familia zetu. Huu ni wakati wetu kutubu na kuona aibu kwa mateso ambayo tumewapa mama, dada, shangazi na wake zetu.
Mateso ambayo wamepata wazee na watoto wetu. Kwa namna yoyote. Mimi nakiri kuwa nimeshiriki kuifisadi nchi kwa kula kwa urefu wa kamba yangu. Bila kufikiria wale ambao wamefungiwa kwenye milingoti hata kamba hazipo. Nimekula kwangu na nikaenda kula kwao. Naombeni msamaha watanzania.
Hotuba ya Kapten Tesha imenifikirisha sana. Nimetokwa na machozi. Amemtaja Shetani kwa jina kabisa bila woga wowote. Tumuunge mkono. Lissu nisamehe pale ambapo nlikusema vibaya. Sasa nakuelewa zaidi. Umeutoa uhai wako sababu yetu. Ungeweza kukaa ughaibuni ukala maisha. Hukufanya hivyo. Ulirudi nchi ile ile iliyokupiga risasi ukapambane na mafisadi. Wewe si mtu wa kawaida. Katika hili Lissu hukuwahi kufikiria Dini. Ulifikiria haki zaidi.
NATOA WITO TUMUUNGE MKONO KAPTENI TESHA.
Huyu Kapten anajua vizuri hatari ambayo inamkabili baada ya hili. Anajua vizuri changamoto ambazo atakumbana nazo. Ameamua kumfunga paka kengele. Huyu ni mmoja ya Wazalendo wakubwa wa hii nchi. Tafadhali nawaomba Watanzania bila kujali vyama, dini na rangi au njaa na matumbo yetu. Tumuunge mkono.
SAA YA UKOMBOZI NI SASA. Miaka mingi sisi tumeshiriki kuifisadi hii nchi na kujineemesha wenyewe na familia zetu. Huu ni wakati wetu kutubu na kuona aibu kwa mateso ambayo tumewapa mama, dada, shangazi na wake zetu.
Mateso ambayo wamepata wazee na watoto wetu. Kwa namna yoyote. Mimi nakiri kuwa nimeshiriki kuifisadi nchi kwa kula kwa urefu wa kamba yangu. Bila kufikiria wale ambao wamefungiwa kwenye milingoti hata kamba hazipo. Nimekula kwangu na nikaenda kula kwao. Naombeni msamaha watanzania.
Hotuba ya Kapten Tesha imenifikirisha sana. Nimetokwa na machozi. Amemtaja Shetani kwa jina kabisa bila woga wowote. Tumuunge mkono. Lissu nisamehe pale ambapo nlikusema vibaya. Sasa nakuelewa zaidi. Umeutoa uhai wako sababu yetu. Ungeweza kukaa ughaibuni ukala maisha. Hukufanya hivyo. Ulirudi nchi ile ile iliyokupiga risasi ukapambane na mafisadi. Wewe si mtu wa kawaida. Katika hili Lissu hukuwahi kufikiria Dini. Ulifikiria haki zaidi.
NATOA WITO TUMUUNGE MKONO KAPTENI TESHA.