The email
JF-Expert Member
- Nov 16, 2022
- 666
- 1,244
Natumai hamjambo wana JF wenzagu,
Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu. Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakiuchukulia mzozo/vita ya Ukrein kwa mitazamo tofauti tofauti na hata baadhi yao kumtupia lawama Putin kwa kuanzisha balaa hilo,ila ukweli ni kuwa si Putin wala Urusi kuwa ndio mwanzilishi katika mgogoro huo na vita kwa ujumla katika Ukrein.
Mataifa haya yamekuwa na historia ndefu kidogo katika mahusiano yao kiuchumi ,kijamii na kidiplomasia
Kiukweli mvutano wa mataifa haya umekuwa ukichangiwa sana na sera chochezi kutoka mataifa ya magharibi hasa Marekani na washirika wake.
Malengo ya mataifa haya ya magharibi ni kutaka kuiweka dunia kwapani na ndo kitu pekee nchi kama Urusi ni mhasimu mkuu wa umoja wa NATO
Kwa nini Urusi ilichukua maamuzi magumu ya kuingia kijeshi nchini Ukrein? Je kama isingeingia kijeshi amani ingekuwepo baina ya Urusi ,Ukrein na bwana zake NATO,
Hiyo ni hapana,vita hivi hata kama visingetokea katika miaka hii vingetokea tu siku zijazo. Kwa nini ilimlazimu Putin kupeleka vikosi Ukrein,we jiulize una ugomvi na mtu harafu jirani yako wa karibu kabisa na wewe anamuarika adui yako kwake.
Na huyo adui yako anaweka kambi kwa jirani yako, wanapika ,wanakula na kunywa,na wanaweka makubaliano kuwa na umoja wao wa kusaidizana kwa lolote baya ama jema. Ina maana tayari adui yako yupo mpakani mwako kupitia jirani yako. Na jirani yako una mwambia aachane na huyo rafike yake mana hana lengo zuri na nyumba wala familia yako.
Jirani yako anakujibu kuwa usimpangia kwani yupo huru kufanya urafiki na mtu yoyote hata kama ni mtu hatarishi kwako,na wala usimpangie cha kufanya .
Wewe ungefanyaje hapo, kama adui yako alikuwa mbali na mlikuwa hamuelewani tangu awali sasa leo yupo karibu na kwako, kuna usalama hapo? Na huyo adui unamjua wazi tabia zake za kuponda mawe juu ya paa za nyumba za watu wengine kwa masirahi yake binafsi,yani kwa choko choko hajambo, na ni mbabe hasa na kuna wengine alisha watandika ngumi za uso pindi tu walipo pishana nae kauli kidogo
Kusema umemtukania kiungo chake cha ndani ya mwili kisha kuja kukuponda hapo hapo kwako ni kawaida kabisa,uwe umetukana au hujatukana utajua mwenyewe,yeye akisema fulani kanitusi basi inatosha
Na wala huwa hahitaji ushauri kutoka kwa mtu yoyote katika kutimiza adhima yake. Maana ana kikundi chake kilicho tayari ki shali popote pale akitaka msaada anapata ,naye ndo mwenye sauti hapo.
Sasa leo yupo karibu na wewe. Kama wewe ungefanyaje, na mwelekeo wa lengo la adui yako unajua kuwa sio wa kheri. Ndicho alicho fanya Mrusi kwa Ukrein.
Nchi za magharibi kama una tumia akiri vizuri sio za kuzipigia promo hata kidogo,ni watu walio jaa ubinafsi wa kutosha,huwa wanaona wengine kama wapo kwa bahati mbaya duniani.
Wapo tayari kufanya lolote kwako pindi tu ukienda kinyume na matakwa yao.Wamejawa na tamaa na ni wachoyo kupita kiasi, chochote atakacho kupa jua tu utakilipia hata kama sio leo. Mambo yao siku zote ni meme ila ya wenzao ni mabaya kila kuchwao.
NATO eti ni kikundi cha kujihami, wanajihami na yupi wakati wao ndo waanzisha shari kila kuchwao.
Tuombe Mungu sana vita hii mrusi ashinde,kinyume na hapo dunia itakuwa imeangukia kwenye shimo ambalo kamwe haitakuja kuokolewa na yeyote tena.
Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu. Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakiuchukulia mzozo/vita ya Ukrein kwa mitazamo tofauti tofauti na hata baadhi yao kumtupia lawama Putin kwa kuanzisha balaa hilo,ila ukweli ni kuwa si Putin wala Urusi kuwa ndio mwanzilishi katika mgogoro huo na vita kwa ujumla katika Ukrein.
Mataifa haya yamekuwa na historia ndefu kidogo katika mahusiano yao kiuchumi ,kijamii na kidiplomasia
Kiukweli mvutano wa mataifa haya umekuwa ukichangiwa sana na sera chochezi kutoka mataifa ya magharibi hasa Marekani na washirika wake.
Malengo ya mataifa haya ya magharibi ni kutaka kuiweka dunia kwapani na ndo kitu pekee nchi kama Urusi ni mhasimu mkuu wa umoja wa NATO
Kwa nini Urusi ilichukua maamuzi magumu ya kuingia kijeshi nchini Ukrein? Je kama isingeingia kijeshi amani ingekuwepo baina ya Urusi ,Ukrein na bwana zake NATO,
Hiyo ni hapana,vita hivi hata kama visingetokea katika miaka hii vingetokea tu siku zijazo. Kwa nini ilimlazimu Putin kupeleka vikosi Ukrein,we jiulize una ugomvi na mtu harafu jirani yako wa karibu kabisa na wewe anamuarika adui yako kwake.
Na huyo adui yako anaweka kambi kwa jirani yako, wanapika ,wanakula na kunywa,na wanaweka makubaliano kuwa na umoja wao wa kusaidizana kwa lolote baya ama jema. Ina maana tayari adui yako yupo mpakani mwako kupitia jirani yako. Na jirani yako una mwambia aachane na huyo rafike yake mana hana lengo zuri na nyumba wala familia yako.
Jirani yako anakujibu kuwa usimpangia kwani yupo huru kufanya urafiki na mtu yoyote hata kama ni mtu hatarishi kwako,na wala usimpangie cha kufanya .
Wewe ungefanyaje hapo, kama adui yako alikuwa mbali na mlikuwa hamuelewani tangu awali sasa leo yupo karibu na kwako, kuna usalama hapo? Na huyo adui unamjua wazi tabia zake za kuponda mawe juu ya paa za nyumba za watu wengine kwa masirahi yake binafsi,yani kwa choko choko hajambo, na ni mbabe hasa na kuna wengine alisha watandika ngumi za uso pindi tu walipo pishana nae kauli kidogo
Kusema umemtukania kiungo chake cha ndani ya mwili kisha kuja kukuponda hapo hapo kwako ni kawaida kabisa,uwe umetukana au hujatukana utajua mwenyewe,yeye akisema fulani kanitusi basi inatosha
Na wala huwa hahitaji ushauri kutoka kwa mtu yoyote katika kutimiza adhima yake. Maana ana kikundi chake kilicho tayari ki shali popote pale akitaka msaada anapata ,naye ndo mwenye sauti hapo.
Sasa leo yupo karibu na wewe. Kama wewe ungefanyaje, na mwelekeo wa lengo la adui yako unajua kuwa sio wa kheri. Ndicho alicho fanya Mrusi kwa Ukrein.
Nchi za magharibi kama una tumia akiri vizuri sio za kuzipigia promo hata kidogo,ni watu walio jaa ubinafsi wa kutosha,huwa wanaona wengine kama wapo kwa bahati mbaya duniani.
Wapo tayari kufanya lolote kwako pindi tu ukienda kinyume na matakwa yao.Wamejawa na tamaa na ni wachoyo kupita kiasi, chochote atakacho kupa jua tu utakilipia hata kama sio leo. Mambo yao siku zote ni meme ila ya wenzao ni mabaya kila kuchwao.
NATO eti ni kikundi cha kujihami, wanajihami na yupi wakati wao ndo waanzisha shari kila kuchwao.
Tuombe Mungu sana vita hii mrusi ashinde,kinyume na hapo dunia itakuwa imeangukia kwenye shimo ambalo kamwe haitakuja kuokolewa na yeyote tena.