Nateseka sana na complicated U.T.I. Naelekea kukata tamaa, nisaidieni niondokane na mateso haya

Mu7

JF-Expert Member
Jun 15, 2013
1,560
1,821
Habari za leo wapendwa?

Mwenzenu niko njia panda hata future yangu siioni! Kwa ujumla naelekea kukata tamaa kabisa. Mimi ni mgonjwa, nahitaji ufumbuzi wa tatizo langu lakini pamoja na juhudi zote mpaka sasa sijapata mwanga nalimalizaje mie! Ni mwaka sasa tangu nimeanza kuteseka na tatizo hili. Mimi ni mwanaume, umri wangu miaka 50. Nina tatizo katika njia ya mkojo ambalo daktari wangu amelitambua kuwa ni COMPLICATED U.T.I.

DALILI ZAKE:

1. Mkojo kuuma sana wakati wa kukojoa mpaka muda mfupi baada ya kukojoa.
2. Muwasho na maumivu eneo zima la kinena, mapajani kwa ndani na njia ya haja kubwa.
3. Ninapokaa nahisi kama nimekalia kitu katikati ya makalio (eneo kati ya uume na njia ya haja kubwa).
4. Maumivu makali wakati wa ejaculation (kutoa mbegu za uzazi).

N.B: Pamoja na mkojo kuuma, mkojo unatoka kawaida na unaisha kwenye kibofu.

JUHUDI ZA KUSAKA TIBA:
Nilianza kupata huduma katika hospitali ya wilaya huku kwetu mkoani ikionekana nasumbuliwa na U.T.I. lakini sikuwahi kupata nafuu yoyote. Hatimaye nilipewa rufaa kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako nilipata vipimo mbalimbali (ikiwa ni pamoja na ULTRASOUND SCAN, VIPIMO VYA DAMU NA MKOJO).

Baada ya vipimo, Daktari Bingwa wa njia ya mkojo (Urologist) aliniambia kuwa tatizo langu linaitwa COMPLICATED U.T.I. Ni U.T.I. ambayo imesababisha maambukizi kwenye Tezi Dume. Tezi dume haijangezeka (not enlarged) lakini imevimba (inflamed) ndio sababu ya hisia ya kukalia kitu katikati ya makalio. Alinambia kuwa tiba yake haihitaji upasuaji kwa kuwa tezi haijaongezeka. Nitapewa dawa za kuondoa maambukizi (infection) na hali yangu itaimarika.

Nilipewa dozi ya LEVOFLOXACIN 500mg mara moja kwa siku kwa muda wa siku 30 lakini hata baada ya kutumia dawa hiyo kwa ukamilifu sikupata nafuu yoyote. Kwa sasa nipo nyumbani huku mkoani. Changamoto niliyonayo ni kukosa fedha ya kurudi Muhimbili kufuatilia tiba zaidi ukizingatia sina bima ya afya.

SABABU YA KULILETA HAPA JAMVINI:
Natambua kuwa JamiiForums imejaa wabobezi wa fani na taaluma mbalimbali. Nimelileta hapa nikiomba msaada wa ushauri kwa madaktari mliomo humu juu ya tiba zaidi ninayoweza kutumia bila kulazimika kurudi Muhimbili baada ya LEVOFLOXACIN kufeli ukizingatia tatizo tayari linafahamika.

Mniwie radhi kwa post ndefu. Nimejaribu kuandika hivi ili maelezo yatosheleze bila kuacha maswali mengi na hivyo kurahisisha upatikanaji wa msaada kutoka kwenu.

Natanguliza shukrani nikisubiri msaada wenu!
 
Pole Mkuu. Ni vyema ningejua upo mkoa gani ili nikusaidie na Dawa za kisunna. Kama utakua na uhitaji nazo
 
Tatizo, kuna vitu watu mnafanya halafu mnapokuja kuomba ushauri huwa mnaongea kama haya maradhi yamewakuta tu......

Naomba nikuulize, huwa hauli nyuma yaani kula mwanamke hata mwanaume kinyume na maumbile haujawahi fanya hiyo kitu?!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HOME / ... / PROSTATITIS
Prostatitis
(Prostatodynia)
By Gerald L. Andriole, MD, Barnes-Jewish Hospital, Washington University School of Medicine
Last full review/revision Nov 2020| Content last modified Nov 2020
CLICK HERE FOR THE PROFESSIONAL VERSION
GET THE QUICK FACTS
Prostatitis is pain and swelling, inflammation, or both of the prostate gland.
The cause is sometimes a bacterial infection.
Pain can occur in the area between the scrotum and anus or in the lower back, penis, or testes.
Men feel a frequent, urgent need to urinate, and urination, erection, ejaculation, and defecation may be painful.
Urine and sometimes fluids expressed from the prostate gland are cultured.
Bacterial infection is treated with antibiotics.
Symptoms of prostatitis, regardless of the cause, may be treated with warm sitz baths, relaxation techniques, and drugs.
The prostate is a gland in men that lies just under the bladder and surrounds the urethra. The gland, along with the nearby seminal vesicles, produces much of the fluid that makes up a man's ejaculate (semen). The prostate is walnut-sized in young men but enlarges with age.

Male Reproductive Organs

Prostatitis usually develops for unknown reasons. Prostatitis can result from a bacterial infection that spreads to the prostate from the urinary tract or from bacteria in the bloodstream. Bacterial infections may develop slowly and tend to recur (chronic bacterial prostatitis) or develop rapidly (acute bacterial prostatitis). Some people develop chronic prostatitis in the absence of bacterial infection. This type may or may not involve inflammation. Occasionally, prostatitis without bacterial infection causes inflammation but no symptoms.
 
 
Tatizo, kuna vitu watu mnafanya halafu mnapokuja kuomba ushauri huwa mnaongea kama haya maradhi yamewakuta tu......

Naomba nikuulize, huwa hauli nyuma yaani kula mwanamke hata mwanaume kinyume na maumbile haujawahi fanya hiyo kitu?!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kutoka moyoni kabisa SIJAWAHI KUFANYA HIVYO iwe kwa mwanamke au kwa mwanaume. Ninahitaji sana msaada wa utatuzi,, ningekuwa nimeshawahi hata mara moja ningesema wazi maana nahitaji kupata ufumbuzi.
 
Jitahidi ukipatiw tiba upatiwe pamoja na wapenzi wako wote kama unao ila kama uko CHAPUTA hapo utapata tiba peke yako maana mikono haina UTI
 
Back
Top Bottom