Natangaza rasmi kujiunga CCM

Natangaza rasmi kujiunga CCM

ego

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2013
Posts
1,620
Reaction score
1,408
Baada ya kufuatilia mchakato wa kampeni na kutafakari tulikotoka na kuangalia tunakokwenda nimeamua kutangaza kujiunga na CCM.

Sababu ni nyingi lakini kwa uchache sababu zangu ni hizi

1. Ubora wa vyama
Kimsingi CCM ni chama cha watanzania kwa maana chama hiki hakihodhiwi na familia fulani au waasisi hawana mizizi tena ndani ya chama hiki. lakini vyama hivi vingine nimeviangalia nikaona bado vinamirikiwa na watu fulani.

Vyama hivi vinakaribisha wanachama kwa kuwa ndio tiketi ya kuungwa mkono na wapiga kura lakini katika baadhi ya vyama bado nafasi muhimu zinahodhiwa moja kwa moja au kupitia wawakilishi wao. si kila mtanzania anaweza kuingia katika vyama hivi akazigusa nyadhifa hizo hata kama zimevikwa mwavuli wa nyadhifa hizo kupigiwa kura kidemokrasia.

Kama taifa ni lazima tujihakikishie kuwa chombo hiki ni maliyetu kabla ya kufanya maamuzi ya kukikabidhi chombo hicho madaraka makubwa zaidi ya nchi yetu vinginevyo tunaweza kuchuuza uhuru wetu na mali zetu kwa gharama nafuu nafuu.

Kwa chama cha watanzania tunakuwa na uhakika kuwa hata kama chama kitapata kiongozi akatuongoza vibaya lakini kwa kuwa kiongozi huyu chama si chake basi kiongozi huyu anaweza kutoka na akaingia kiongozi mwingine na akatupeleka tunakotaka.

2. Ubora wa wagombea urais waliosimamishwa na vyama.

Leo hii watanzania wote wanalalamika maendeleo yetu hayalingani na uwezo wetu. kabla ya kufanya maamuzi yoyote ni lazima tutafakari tatizo liko wapi na tuchague njia ya kupita.

Jambo hili linachangiwa kwa kiasi kikubwa na viongozi tuliokuwa tumewapa dhamana lakini hiyo pekee haitoshi bali kuchunguza kwa vipi? tatizo kubwa ambalo limefanya viongozi wetu washindwe kutupatia maendeleo tuliyotegemea ni mfumo wa kupatikana viongozi hawa. tulitengeneza utaratibu wa watu kuunda makundi na kuanza kutafuta uongozi na pale wanapoupata hugawana nyadhifa zote lakini muungano wao kama kundi hudhoofisha madaraka na uwezo wa uongozi.

Mtu anapewa kuongoza wizara au shirika si kwa sababu ameonekana kuwa na uwezo wa kuliongoza vizuri bali kwa sababu ni mwana mtandao au kundi. mtu anafanya kosa anashindwa kuwajibishwa si kwa sababu hakuna sheria bali ni mwenzao.

Mambo haya yalifanya watu waliopewa dhamana wakafanya kazi kwa uaminifu kwa kuwatumikia wananchi kuchukiwa na watu hawa waliounda mitandao wakiwa wengi wao hawana sifa kwa maana utendaji wa hawa ama uliwazibia riziki kwa kuziba nafasi walizokuwa wakizitumia kutuibia watanzania au waliumbuliwa kwa uzembe wao au kuonyeshwa wazi kuwa walikuwa mbumbumbu.

Enzi hizo watendaji bora kama Augustino Mrema walikimbia chama hiki cha watanzania, kwa uelewa wangu ni kuwa chama ni mali ya wanachama hivyo katika kufanya maamuzi wote wabaya kwa wananchi na wazuri wanashiriki katika kufanya maamuzi.

Wazuri watajitahidi kuleta maamuzi ya kuwatetea wananchi na wabaya watajitahidi kufanya maamuzi ya kulinda maslahi yao. hivyo inategemea ni kundi gani limeshika mpini na kundi gani limeshika makali.

Baada ya 1995 tumepita hatua tofauti mpaka hapa tulipo leo.

kwa mtizamo wangu binafsi chama hiki cha watanzania yaani CCM kwa sasa bado kinayo makundi yote ndani lakini kundi linalotaka kuwatetea wananchi limeshika mpini. Kwanza walitambua kuwa chama hiki kimetekwa na watu wanaosimama kwenye majukwaa kuwaambia wananchi mambo mazuri lakini walipopewa nyadhifa wamewageka wananchi na katibu mkuu akazunguka nchi nzima akitangaza nia yao ya kurejesha madaraka kwa wanachama.

Msemo huu wasiouelewa wanaweza kudhani ni maswala ya mashina ya vyama huko ngazi ya chini lakini tafsiri pana ni kurejesha chama katika kutumikia wanachama au wananchi na sio chama kutumika kama njia ya watu kuingia kutafutia dili tena nyingi zikiwa ni za kukinzana na sheria.

Bado nikirejea mwaka 2010 wakati wa msimu wa pili wa raisi wetu anayemaliza mda wake, alikuwa ameamua kuachana na wapambe wa kampeni. hili lina maana gani? kwangu mimi ninaona kabisa kuwa raisi baada ya kukaa miaka mitano aliona jinsi mizigo ya makundi ya kampeni ilivyokuwa ikimkwaza katika kutimiza matakwa ya wananchi. nadhani alitamani asitumie watu kufanya kampeni ambao wangemgarimu k
 
Yote 9, 10 LOWASSA tar 25 tunamkabidhi nchi hatuhitaji longolongo tena naona unakumbuka shuka asubuhi kumekucha @@@
 
Oya op! You's a sane guy. Few of em in here, so expect matusi, wengine wala hawatasoma watakujibu, ndio ujue kujua kulog in na kuregister hakumfanyi mtu kuwa sane.
Oya peace......
#HapaKaziTu
 
Uzi mrefu sana... kwasababu ni unahusu kula matapishi nakusikitikia tu.... kama upeo wako ndo huo basi pole.... KURA ni kwa LOWASSA hakuna mtu awezaye mshinda....
 
siku nikibadili mawazo kuhusu CDM, asilani sitaenda CCM,TLP wala ACT, afadhali niende kwa mzeee Rungwe au msela Dovutwa, hata kwa yule Chief nani sijui powa tu. LAKINI SIO CCM
 
CCM Hapa Zika Tu. Ni Mabadiliko.Rais ni Lowassa.
 
hoja yangu sijui kama unajua unachokifanya? na hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa la watanzania kwa kusema tunakosa elimu lakini sio elimu ya kuongeza madarasa bali nadhani tunatatizo la contents za elimu.

hivi unaweza kumsikia mtanzania yeyote anasema msemo wako kwa waajiri, kuwa mimi siwezi kuajiriwa na kampuni fulani, nikihama kampuni hii labda niende kampuni fulani na fulani.

siasa ni sawa na waajiri maana unapofanya maamuzi yanachangia asilimia kama 75% ya maisha yako. lakini watanzania siasa tumezigeuza ushabiki wa timu ya mpira ambao kwako wewe ukishabikia unaleta manufaa kwa timu na sio kwako binafsi hasa kiuchumi.

unahitaji kuangalia tutapigaje hatua za maendeleo na hapa usibaki kusikiliza wanayosema kwenye majukwaa tu bali fuatilia kila kitu ili wewe binafsi uwe na dira na wanasiasa wanapokuja uwapime kwa wao kuonekana wanakidhi matakwa yako.

usipokuwa makini hakuna wa kukuhurumia kuwa eti unahuzuni wa kufiwa na ndugu yako bali wanaweza kukutapeli na fedha ya sanda. wewe mwenyewe ndiye unachunga mzigo wako na uhakikishe unamkabidhi mtu sahihi.

siku nikibadili mawazo kuhusu CDM, asilani sitaenda CCM,TLP wala ACT, afadhali niende kwa mzeee Rungwe au msela Dovutwa, hata kwa yule Chief nani sijui powa tu. LAKINI SIO CCM
 
SERIKALI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaelekea imekanyaga mdudu mchafuzi. Mdudu huyo Zanzibar anaitwa sheshere, Wabena humwita hilufi, Wasangu wanamwita shilufya. MWENENDO wa uongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unasikitisha mno. Masikitiko yenyewe ni yale yanayotokana na utamaduni mbaya wa kuujua ukweli, halafu kwa makusudi, viongozi wakaamua kuudharau.

Mtu akikanyaga sheshere, hawezi kufika anakokwenda; atazunguka sana, atapitiliza hata eneo analokwenda hadi ashikwe au asimamishwe na mtu anayemfahamu.


Hivyo ndivyo ilivyo kwa Serikali ya CCM. Imekanyaga sheshere. Inasema ovyo, inayumba njia nzima tangu ilipoanza safari mwaka 2005. Haieleweki. Mara inasema maisha bora yanawezekana, mara wabunge wake wanalia Ilani ya CCM haitekelezeki.Mara JPM ana ahidi yale yale waliyo ahidi 2005 lakini hayajatekelezeka.


Wapo makada wa chama hiki kikongwe ambao tambo zao ni kwamba kitadumu madarakani kwa karne nyingi zijazo, lakini wamekosa ujasiri wa kuona kuwa kila hatua inayopigwa katika kujipanga upya inakuwa afadhali ya ilivyokuwa hapo kabla, mwendo ni kukimbilia kwenye kuangamia, hawasikii na wala hawaoni.


Kwa sababu hiyo,wapo Makada waliopata kuonya iwapo chama hicho hakitarudi kwenye asili yake hiyo, itakapofika Oktoba 25,2015, siku ya uchaguzi mkuu mwingine, "kinaweza kupata majuto yasiyo na kifani." Tatizo la serikali ya CCM ni kuvimbiwa madaraka kiasi cha kushindwa kujua hata maana ya kaulimbiu ya Peoples Power. Hata watoto wadogo wanajua kwamba kaulimbiu hiyo haina maana ya fujo, tafsiri ya fujo inatolewa na dola na CCM kwa kusisitiza amani na wakati huo huo wakionekana waziwazi wakijiandaa kukandamiza haki.


CCM inaongoza wanachama wa CCM na wahuni,wapumbavu,mbumbumbu na malofa " kwamba kama hauko CCM basi wewe ni mhuni,mpumbavu,lofa na mbumbumbu.


CCM inakandamiiza haki za msingi za raia kwa vitisho ama kwa kutumia kodi za wavuja jasho kama kujiunga na chama chochote cha Siasa,kukusanyika,kutoa maoni n.k.


Kutokana na ukweli huu, CCM haiwezi kuwaletea watu maendeleo bali inanufaika na Umaskini wao.Haiwezi kuwaletea maendeleo kwa sababu maendeleo yatafanya wananchi wasikitegemee chama hicho tawala kwa fulana, kofia na skafu za kuvaa wakati wa sikukuu, kusali makanisani na misikitini na hata sokoni.


Kwa hiyo, si kila anayehudhuria mikutano ya CCM na anayevaa kofia na fulana ya CCM ni mpenzi, shabiki au mwanachama wa chama tawala bali wengine na ambao kwa kweli ndio wengi hufanya hivyo kwa kukosa mavazi mazuri ya kutokea pamoja na kushuhudia burudani za muziki za wasanii Chege,Temba,Diamond na wengineo.


Ushahidi mwingine wa jinsi CCM inavyonufaika na umaskini wa Watanzania ni biashara ya shahada nyakati za uchaguzi. Biashara ya shahada ambapo mabalozi na wenyeviti wa CCM wa mitaa na kata huranda huku na kule kununua shahada hushamiri sana katika maeneo maskini.

Ndiyo maana CCM ambacho ni mtuhumiwa mkuu wa ununuzi wa shahada za kupigia kura mara zote hushinda uchaguzi katika maeneo ambayo wakazi wake ni maskini wa kutupwa kama vile mitaa ya Dar es Salaam iliyojaa wabwia unga.

Pia kuna madai kwamba chama tawala ni maarufu kwa kugawa fedha shilingi elfu mbili mbili, tatu tatu au elfu nne nne ili kipigiwe kura iwe kwenye uchaguzi mkuu au uchaguzi mdogo. Madai haya yanapata nguvu kutokana na ukweli kwamba wapo wana-ccm wamekamatwa wakiuza au kununua shahada za kura.


Kwa ufupi, CCM inanufaika sana na umaskini wa kutupwa. Bila umaskini wa kutupwa fulana za njano, kofia za kijani na skafu zisingeonekana makanisani na miskitini. Watu wanahudhuria mikutano ya hadhara ya CCM ili kuambulia ‘kiwalo' tu na si mapenzi na chama.


Pia watu wanahudhuria kwa wingi mikutano ya hadhara ya CCM ili waweze kuambulia shilingi elfu tatu za kununulia unga wa muhogo wakasogeza siku mbele na si kwa kukipenda chama hicho kikongwe cha siasa nchini. Umaskini ni kete kubwa kwa CCM.


Huenda basi, nchi hii haitapata maendeleo kamwe au daima dumu kwa sababu chama kilichopo madarakani hakitaki maendeleo kwani kuleta maendeleo ni sawa na kujipalia makaa. Watu walioendelea na wasiokabiliwa na umaskini watachagua kutokana na utashi wao na si ili wapate fulana au kofia ya kijani.


Ile ndiyo ilikuwa kete ya mwisho ya Mwalimu kuiokoa CCM mwaka 1995 kwa vile alishaona inazolewa na wimbi la mageuzi.


Jiulizeni, mbona Zambia haikuyumba UNIP ya Kenneth Kaunda ilipoondolewa? Mbona Kenya haikuyumba KANU ya Jomo Kenyatta na baadaye Daniel arap Moi ilipoondolewa? Mbona UPC ya Milton Obote ilipoondolewa na baadaye serikali ya CCM kuwasaidia kina Yoweri Musevuni Uganda kuna utulivu mkubwa? Kwanini nongwa iwe kwa Tanzania? Tanzania ni yetu sote. Kama ni jehanamu iwe yetu sote na kama ni pepo iwe yetu sote na Tanzania bila CCM inawezekana.


Hata Mungu alipowaambia wana wa Israel waondoke Misri, ni Mungu huyo huyo aliyewapa Mafarao wa Misri moyo mgumu. Siku ya mwisho ilipofika Mafarao walipata pigo, jeshi lao liliangamia baharini huku Waisrael wakienda zao.

Ndivyo itakuwa kwa CCM tena katika kipindi ambacho inashikilia kikombe cha mateso. Lowassa amekabidhiwa fimbo ya kugawa maji ya kuangamiza CCM?..

Chagua LOWASSA,Chagua madiwani na wabunge wa UKAWA!!
AMUA LEO,KURA YAKO CHADEMA/NCCR/NLD/CUF/UKAWA....ONDOA CCM kwa amani na Utulivu kupitia sanduku la kura!!
 
Nenda kwa magamba wenzako hapa tupo na Lowassa speed 120 ruka dirishan
 
Upo sahihi mkuu Vilaza ndio bado wanafuata mkumbo hawatambui lolote, na hawa ndio wale wanaojua UKAWA itakuwapo kwenye karatasi ya kupigia kura
 
Back
Top Bottom