- Thread starter
- #21
Changamoto ni watanzania hatujui kuchambua mambo na kuyahusisha na maisha yetu.
mifumo yetu ya elimu haituwezeshi kuoanisha practical life na theorical knowledge.
anayekabiliwa na changamoto sio chama cha mapinduzi bali ni watanzania.
chama cha mapinduzi hakina mwenyewe bali ni mali ya watanzania.
ni sawa na watanzania tulivyounda mashirika kama tanesco kushughulikia mambo ya umeme. sasa kama tumeunda shirika la tanesco tukakusanya kodi tukaweka na wakatokea baadhi ya watanzania wakagundua kuwa watanzania tumelala wakatumia kodi zetu tunazoingiza tanesco kwa matumizi yao na sisi tukabaki tukisema tatizo la tanesco ni kutokuboresha umeme hivyo bora yaje makampuni ya kigeni yatupatie umeme unadhani nani mjinga hapo je ni wale wachache waliotuibia? au ni sisi wenyewe tulioibiwa tuna matatizo?
mfumo wetu wa siasa tumeweka uongozi wa nchi lazima upitie kwenye vyama vya siasa. asilimia kubwa ya watanzania tumelala lakini wakawepo wahuni wachache wakatutambua tulivyolala wanaingia wanasimama kwenye majukwaa wanatulaghai kwa maneno kwa staili ya matapeli tunawakabidhi madaraka kumbe wengi si viongozi.
tukitambua hili hatutakaa kuangalia jina la chama na kudhani jina ndio tatizo, kama unavyoona mkisema kampuni haitalipa kodi miaka mitano na wajanja wakaanza kubadili majina na kujifanya ni kampuni mpya na kuendelea kutokulipa kodi ndivyo wajanja hawa watakavyobadili majina ya vyama lakini matendo ni yaleyale na watu ni walewale.
tunahitaji kutambua matatizo yetu ni yapi na tutatue hayo na sio kukalili majina ya makundi kumbe wajanja wanahama huku na kule.
mifumo yetu ya elimu haituwezeshi kuoanisha practical life na theorical knowledge.
anayekabiliwa na changamoto sio chama cha mapinduzi bali ni watanzania.
chama cha mapinduzi hakina mwenyewe bali ni mali ya watanzania.
ni sawa na watanzania tulivyounda mashirika kama tanesco kushughulikia mambo ya umeme. sasa kama tumeunda shirika la tanesco tukakusanya kodi tukaweka na wakatokea baadhi ya watanzania wakagundua kuwa watanzania tumelala wakatumia kodi zetu tunazoingiza tanesco kwa matumizi yao na sisi tukabaki tukisema tatizo la tanesco ni kutokuboresha umeme hivyo bora yaje makampuni ya kigeni yatupatie umeme unadhani nani mjinga hapo je ni wale wachache waliotuibia? au ni sisi wenyewe tulioibiwa tuna matatizo?
mfumo wetu wa siasa tumeweka uongozi wa nchi lazima upitie kwenye vyama vya siasa. asilimia kubwa ya watanzania tumelala lakini wakawepo wahuni wachache wakatutambua tulivyolala wanaingia wanasimama kwenye majukwaa wanatulaghai kwa maneno kwa staili ya matapeli tunawakabidhi madaraka kumbe wengi si viongozi.
tukitambua hili hatutakaa kuangalia jina la chama na kudhani jina ndio tatizo, kama unavyoona mkisema kampuni haitalipa kodi miaka mitano na wajanja wakaanza kubadili majina na kujifanya ni kampuni mpya na kuendelea kutokulipa kodi ndivyo wajanja hawa watakavyobadili majina ya vyama lakini matendo ni yaleyale na watu ni walewale.
tunahitaji kutambua matatizo yetu ni yapi na tutatue hayo na sio kukalili majina ya makundi kumbe wajanja wanahama huku na kule.
SERIKALI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaelekea imekanyaga mdudu mchafuzi. Mdudu huyo Zanzibar anaitwa sheshere, Wabena humwita hilufi, Wasangu wanamwita shilufya. MWENENDO wa uongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unasikitisha mno. Masikitiko yenyewe ni yale yanayotokana na utamaduni mbaya wa kuujua ukweli, halafu kwa makusudi, viongozi wakaamua kuudharau.
Mtu akikanyaga sheshere, hawezi kufika anakokwenda; atazunguka sana, atapitiliza hata eneo analokwenda hadi ashikwe au asimamishwe na mtu anayemfahamu.
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Serikali ya CCM. Imekanyaga sheshere. Inasema ovyo, inayumba njia nzima tangu ilipoanza safari mwaka 2005. Haieleweki. Mara inasema maisha bora yanawezekana, mara wabunge wake wanalia Ilani ya CCM haitekelezeki.Mara JPM ana ahidi yale yale waliyo ahidi 2005 lakini hayajatekelezeka.
Wapo makada wa chama hiki kikongwe ambao tambo zao ni kwamba kitadumu madarakani kwa karne nyingi zijazo, lakini wamekosa ujasiri wa kuona kuwa kila hatua inayopigwa katika kujipanga upya inakuwa afadhali ya ilivyokuwa hapo kabla, mwendo ni kukimbilia kwenye kuangamia, hawasikii na wala hawaoni.
Kwa sababu hiyo,wapo Makada waliopata kuonya iwapo chama hicho hakitarudi kwenye asili yake hiyo, itakapofika Oktoba 25,2015, siku ya uchaguzi mkuu mwingine, "kinaweza kupata majuto yasiyo na kifani." Tatizo la serikali ya CCM ni kuvimbiwa madaraka kiasi cha kushindwa kujua hata maana ya kaulimbiu ya Peoples Power. Hata watoto wadogo wanajua kwamba kaulimbiu hiyo haina maana ya fujo, tafsiri ya fujo inatolewa na dola na CCM kwa kusisitiza amani na wakati huo huo wakionekana waziwazi wakijiandaa kukandamiza haki.
CCM inaongoza wanachama wa CCM na wahuni,wapumbavu,mbumbumbu na malofa " kwamba kama hauko CCM basi wewe ni mhuni,mpumbavu,lofa na mbumbumbu.
CCM inakandamiiza haki za msingi za raia kwa vitisho ama kwa kutumia kodi za wavuja jasho kama kujiunga na chama chochote cha Siasa,kukusanyika,kutoa maoni n.k.
Kutokana na ukweli huu, CCM haiwezi kuwaletea watu maendeleo bali inanufaika na Umaskini wao.Haiwezi kuwaletea maendeleo kwa sababu maendeleo yatafanya wananchi wasikitegemee chama hicho tawala kwa fulana, kofia na skafu za kuvaa wakati wa sikukuu, kusali makanisani na misikitini na hata sokoni.
Kwa hiyo, si kila anayehudhuria mikutano ya CCM na anayevaa kofia na fulana ya CCM ni mpenzi, shabiki au mwanachama wa chama tawala bali wengine na ambao kwa kweli ndio wengi hufanya hivyo kwa kukosa mavazi mazuri ya kutokea pamoja na kushuhudia burudani za muziki za wasanii Chege,Temba,Diamond na wengineo.
Ushahidi mwingine wa jinsi CCM inavyonufaika na umaskini wa Watanzania ni biashara ya shahada nyakati za uchaguzi. Biashara ya shahada ambapo mabalozi na wenyeviti wa CCM wa mitaa na kata huranda huku na kule kununua shahada hushamiri sana katika maeneo maskini.
Ndiyo maana CCM ambacho ni mtuhumiwa mkuu wa ununuzi wa shahada za kupigia kura mara zote hushinda uchaguzi katika maeneo ambayo wakazi wake ni maskini wa kutupwa kama vile mitaa ya Dar es Salaam iliyojaa wabwia unga.
Pia kuna madai kwamba chama tawala ni maarufu kwa kugawa fedha shilingi elfu mbili mbili, tatu tatu au elfu nne nne ili kipigiwe kura iwe kwenye uchaguzi mkuu au uchaguzi mdogo. Madai haya yanapata nguvu kutokana na ukweli kwamba wapo wana-ccm wamekamatwa wakiuza au kununua shahada za kura.
Kwa ufupi, CCM inanufaika sana na umaskini wa kutupwa. Bila umaskini wa kutupwa fulana za njano, kofia za kijani na skafu zisingeonekana makanisani na miskitini. Watu wanahudhuria mikutano ya hadhara ya CCM ili kuambulia ‘kiwalo' tu na si mapenzi na chama.
Pia watu wanahudhuria kwa wingi mikutano ya hadhara ya CCM ili waweze kuambulia shilingi elfu tatu za kununulia unga wa muhogo wakasogeza siku mbele na si kwa kukipenda chama hicho kikongwe cha siasa nchini. Umaskini ni kete kubwa kwa CCM.
Huenda basi, nchi hii haitapata maendeleo kamwe au daima dumu kwa sababu chama kilichopo madarakani hakitaki maendeleo kwani kuleta maendeleo ni sawa na kujipalia makaa. Watu walioendelea na wasiokabiliwa na umaskini watachagua kutokana na utashi wao na si ili wapate fulana au kofia ya kijani.
Ile ndiyo ilikuwa kete ya mwisho ya Mwalimu kuiokoa CCM mwaka 1995 kwa vile alishaona inazolewa na wimbi la mageuzi.
Jiulizeni, mbona Zambia haikuyumba UNIP ya Kenneth Kaunda ilipoondolewa? Mbona Kenya haikuyumba KANU ya Jomo Kenyatta na baadaye Daniel arap Moi ilipoondolewa? Mbona UPC ya Milton Obote ilipoondolewa na baadaye serikali ya CCM kuwasaidia kina Yoweri Musevuni Uganda kuna utulivu mkubwa? Kwanini nongwa iwe kwa Tanzania? Tanzania ni yetu sote. Kama ni jehanamu iwe yetu sote na kama ni pepo iwe yetu sote na Tanzania bila CCM inawezekana.
Hata Mungu alipowaambia wana wa Israel waondoke Misri, ni Mungu huyo huyo aliyewapa Mafarao wa Misri moyo mgumu. Siku ya mwisho ilipofika Mafarao walipata pigo, jeshi lao liliangamia baharini huku Waisrael wakienda zao.
Ndivyo itakuwa kwa CCM tena katika kipindi ambacho inashikilia kikombe cha mateso. Lowassa amekabidhiwa fimbo ya kugawa maji ya kuangamiza CCM?..Chagua LOWASSA,Chagua madiwani na wabunge wa UKAWA!! AMUA LEO,KURA YAKO CHADEMA/NCCR/NLD/CUF/UKAWA....ONDOA CCM kwa amani na Utulivu kupitia sanduku la kura!!