Masikini_Jeuri
JF-Expert Member
- Jan 19, 2010
- 6,829
- 1,296
Home boy Kipipili!
Nikiwa mwana Iringa kijana nakupongeza kijana mwenzangu kwa uamuzi wako!
Nakushukuru pia kwa kuamua kujitolea! Iringa kwa ujumla imekuwa na uwakilishi ; pengine naweza sema wa kiimla kwa muda mrefu sasa na matokeo yake mimi na wewe tunayafahamu.
Ushauri wangu ni kuzingatia vipaumbele vifuatavyo
Jimbo la Kalenga linayo rasilimali kubwa sana kiuchumi UTALII na ukiacha juhudi za binafsi za wadau wa sekta hiyo ni kiasi kidogo sana kimetokana na msukumo wa viongozi waliokuwepo na waliopo! Hii nafasi pekee inaweza kuwaajiri vijana wengi sana wa eneo hilo.
Kalenga pia kwa kuwa jirani na Mji wa Iringa inayo nafasi ya kuuuhudumia mji huo kwa nyanja zote; Kama mawasiliano ya barabara yataimarishwa; Basi huduma nyingi amabzo si lazima zibanane mjini Iringa zinaweza kuhamishiwa huko; esp kwa maeneo kama Tosamaganga; Kiwere, Nduli na Kalenga yenyewe hii itaharakisha maendeleo ya maeneo husika na kukuza kipato cha wakazi wako; Hivi sasa naona linafanyika upande wa elimu na huduma za hospitali tu lakini lingewezekana hata katika makazi ya wanafunzi na mahoteli na masoko ya bidhaa za kilimo ama minada ya bidhaa hizo mfano zao la tumbaku.
Nakutakia kila kheri!
Nikiwa mwana Iringa kijana nakupongeza kijana mwenzangu kwa uamuzi wako!
Nakushukuru pia kwa kuamua kujitolea! Iringa kwa ujumla imekuwa na uwakilishi ; pengine naweza sema wa kiimla kwa muda mrefu sasa na matokeo yake mimi na wewe tunayafahamu.
Ushauri wangu ni kuzingatia vipaumbele vifuatavyo
Jimbo la Kalenga linayo rasilimali kubwa sana kiuchumi UTALII na ukiacha juhudi za binafsi za wadau wa sekta hiyo ni kiasi kidogo sana kimetokana na msukumo wa viongozi waliokuwepo na waliopo! Hii nafasi pekee inaweza kuwaajiri vijana wengi sana wa eneo hilo.
Kalenga pia kwa kuwa jirani na Mji wa Iringa inayo nafasi ya kuuuhudumia mji huo kwa nyanja zote; Kama mawasiliano ya barabara yataimarishwa; Basi huduma nyingi amabzo si lazima zibanane mjini Iringa zinaweza kuhamishiwa huko; esp kwa maeneo kama Tosamaganga; Kiwere, Nduli na Kalenga yenyewe hii itaharakisha maendeleo ya maeneo husika na kukuza kipato cha wakazi wako; Hivi sasa naona linafanyika upande wa elimu na huduma za hospitali tu lakini lingewezekana hata katika makazi ya wanafunzi na mahoteli na masoko ya bidhaa za kilimo ama minada ya bidhaa hizo mfano zao la tumbaku.
Nakutakia kila kheri!