Natamani kuwa na mpenzi

Chasaka

Member
Joined
Jun 23, 2011
Posts
67
Reaction score
14
Imesalia miaka kadhaa hivi niwe na miaka thelathini, lakini sijui ni ushamba au ni matatizo yaliyokithiri kiasi cha kushindwa kuwa na historia ya kuwa mpenzi hadi sasa.

Lakini kwa sasa nina hamu kubwa ya kuwa na mpenzi. Kimsingi nimekulia mtaani kama chokoraa lakini nikawa na mtazamo tofauti na watoto wengine wanao kulia mtaani fikra zangu zote ni kwamba niwe msomi hivyo nguvu na akili yangu yote ilikuwa nikutafuta namna ya kupata elimu rasmi.

Nimefanikiwa kuhusu hilo nimemaliza form six mwaka huu na nimefaulu natafuta mtu jinsia ke' wakuni sifia ninapofanya vizuri na kunitia moyo pale changamoto zinapokuwa nyingi 'SINA NDUGU RASMI' ukihisi tunaweza kusonga na haya maisha niujuze kwa namba hii.
 
yahaya huyo tena jide alikuulizia mda si mrefu...usijali utaolewa tu
 
I can never be more proud of you! You challenged the odds!
 
Nimependa jinsi ulivyomkweli na muwazi. Subiri PM toka kwa aliye tayari.

My take: Ondoa mawazo ya kuwa huna bahati kwa hivyo ulivyo, pigana kusoma na kutafuta maisha, ishi na watu vizuri, usikubali kutolewa nje ya goals zako ambazo umejiwekea ambazo unatakiwa uzifikie.
 
Usjali mkuu utawapata tu: ila uwe makin kuna matapeli weng
 

Hongera kwa jitahida za kupata elimu, kila la kheri kwa hayo unayoyafikiria kwa sasa!
 

Nimekuelewa mkuu nitapigana kama ushauri wako unavyo elekeza
 
Soma sana, tafuta pesa utampata unaemtaka ukiwa na pesa
 
hongera kwa mafankio uliyofkia. Kwenye swala la mapenz hasa wewe ambae unayakuta ukubwani hivi sidhan (japo sipingi moja kwa moja) kama utampata anaekufaa kwa staili hii ya kutoa namba hapa. Matapeli ni wengi. Kuwa makini.
 
Hakuna kitu feki kama mapenzi siku hizi. Muombe mungu,utampata wa ukweli.
 


Unatafuta mtu wa kukusifia??? au unatafuta mpenzi wa kungonoka naye?? tiririka kijana. JF ni kila kitu utapata kile unachohitaji.
 
DU matangazo ya namna hii yamekuwa mengi mno humu ndani , nakushauri uyapeleke makanisani au misikitini ikibidi hata vituo vya mabasi.
heee hee heeeeeeeeeeee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…