co fm
JF-Expert Member
- Jul 20, 2016
- 1,569
- 2,584
Habari za jioni humu, japo sio mwandishi mzuri ila naamini lengo langu litaeleweka. Leo katika kutoka kwenye harakati zangu jioni mjini posta Dar es salaam nimekutana na kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 21(according to him), alikuwa kidogo mchafu kiasi akawa ananiomba hela ya kuvuka panton akidai kuwa hana hela ya kuvukia panton.
Katika kumhoji maswali hapa na pale akaniambia ana week moja toka afike katika jiji la Dar es salaam akitokea Mwanza maeneo ya Kisesa, huko Kisesa alikuwa anafanya shughuli za kuuza chakula kwa watu na akipata hela na kusaidia familia yake yaani yeye na mama yake..
Baada ya maongezi ya muda kama nusu saa hivi likaja wazo kwamba hivi siwezi kumsaidia kwa mtaji mdogo hata wa elfu hamsini akafanya biashara hata ya kuuza viungo kama nyanya n.k.
Maana kama ninaweza kuspendi hiyo hela kwa siku moja nikienda club au nikihonga demu. Je wanajamii ushauri wenu au maoni au changamoto zipi ninaweza kukumbana nayo katika hili.Mimi age yangu ni miaka 25, pia sometimes huwa nasaidiwa na watu nisiotegemea
Katika kumhoji maswali hapa na pale akaniambia ana week moja toka afike katika jiji la Dar es salaam akitokea Mwanza maeneo ya Kisesa, huko Kisesa alikuwa anafanya shughuli za kuuza chakula kwa watu na akipata hela na kusaidia familia yake yaani yeye na mama yake..
Baada ya maongezi ya muda kama nusu saa hivi likaja wazo kwamba hivi siwezi kumsaidia kwa mtaji mdogo hata wa elfu hamsini akafanya biashara hata ya kuuza viungo kama nyanya n.k.
Maana kama ninaweza kuspendi hiyo hela kwa siku moja nikienda club au nikihonga demu. Je wanajamii ushauri wenu au maoni au changamoto zipi ninaweza kukumbana nayo katika hili.Mimi age yangu ni miaka 25, pia sometimes huwa nasaidiwa na watu nisiotegemea