Nataka kumrusha mtoto darasa

Mkuu ushauri uliopewa ni mzuri ila kwa kuongeza tu kabla hujamrusha kaa na,walimu wake wa masomo yote wakupe maoni yao juu ya uwezo wa mwanao ukiachana na wewe mwenyewe kuuona uwezo wa mwanao,pia na kama mkikubaliana arushwe form one basi kwanza mrushe la saba uone maendeleo yake ukiona yupo vzur basi kabla hajamaliza unaweza kumrusha form one.ushauri wangu
 
Wee jamaa mbona unaharaka sana ya mwanao kumaliza shule? unataka ule mahari ya fasta fasta nini!

Na usawa huu wa Magufuli kulivyo hamna hela unaweza ozesha mtoto wa kike wa miaka 10 ili ule hela ya mahara
 
cheti cha darasa la 7 ni muhimu kwa nacho, huwezi jua mkuu huenda siku za usoni kukahitajika sana.
 
Atakua kilaza huko sekondari. Walioweka hizo step hawakua vilaza. Na shule zinazojielewa hawawezi mpokea. Subiri afike darasa ya sita labda ndo anaweza kwenda sekondari. Haraka ya nini? Unataka umuozeshe akiwa na miaka 18 au???
 
hakikisha anasoma la Saba ....mrushe la nne had la sita
Kwani la saba lina umuhimu gani? Mi naonaga ni marudio tu! Kuna msichana tulikua nae form one, aliishia la sita na alituburuza vizuri tu na kutoka na division one.
Kuna shule moja pia naijua wanafunzi wanaofanya vizuri wa la sita wanapelekwa kufanya interview za kuingia form one. Atakaefaulu anaendelea na sekondari yake.
 
mimi sikusoma darasa la saba tu lakini form four nilisoma, na nilikuwa na uwezo wa kufanya mtihani wa darasa la saba hasa hesabu nikiwa darasa la nne
Watu mna vichwa!
 
Kumbe kuna vyeti vya lasaba? Mi sikupataga.
 
Aiseee ww jamaa ni kichwa sana
 
Hivi kuna ambaye alishawahi kufeli chekechea?
 
Kumrukisha madarasa mengi sio busara, mrukishe moja then baada ya 2yrs waweza mrukisha jingine
Ukimrukisha madara mengi, mtoto hatakua socially ila atakuwa mentally na maybe physically but atakuwa analack baadhi ya vitu socially na itamsababishia matatizo mbeleni
 
Nilishuhudia schoolmates wangu wakiishia darasa la tano to pre form one na kuna classmates wangu kama watatu waliishia std six nikawakuta secondary wakiwa wanafanya vyema tu kama kawaida na hawakuwa vipanga primary sababu hawakuwahi hata kunizidi kwenye mitihani.

USHAURI:Washirikishe walimu wake hasa wa maths na Science lakini to me nashauri asome la tano then aende kikubwa awe fluent kwenye ngeli.

Binafsi mother alikataa pamoja na kushauriwa na mwalimu wangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…