Nataka kuanza kusoma masomo ya sekondari kupitia elimu ya watu wazima

Elimu ya ujasiriamali ninayo tayari na ninaifanyia kazi
Ndiyo uachane na shule nikupoteza muda, kitu kimoja utambue muda wa kutafuta pesa ni limited ukifika 50yrs huna pesa za kueleweka sahau kuwa hela tena.
 
Elimu haina mwisho.
Muhammad s.a.w.
Mtume WA waislam anasema "ifate elimu hata china"
Mjingamimi hiyo kauli ya "Itafute elimu hata uchina" si hadithi ya mtume Muhammad rehma na amani ziwe juu yake bali ni miongoni mwa semi za kiarabu za kale. Lakini hadithi sahihi ya mtume Muhammad rehma na amani ziwe juu yake ni "Kutafuta elimu ni wajibu juu ya kila muislamu".
 
Ukishamaliza secondary ulitaka uchukue degree gani???

Sikushauri uende secondary .. mambo ni magumu na yamepitwa na wakati...

Sijui utaratibu ukoje huko lakini kama unaweza anza kusoma cheti then uende diploma kama hata usipofika chuo kikuu tayari una qualifications zinazokufanya uwe na uwezo kujiajiri ama kuajiriwa mamii..

Best of luck!
Huna tofauti na Mwanamke aliejiweka kitanzi cha njiti mkonono kuzui kupata ujauzito lakini anakufata mwanamke mwenzako akitaka ushauri kwako na yeye anataka kujiweka njia ya uzazi wa mpango kama yako na wewe unamwambia ni hatari inasababisha maradhi lukuki ilhali wewe umejiweka ...!!
Acha roho mbaya ...
Mwache Dada akasome ...
 
Huna tofauti na Mwanamke aliejiweka kitanzi cha njiti mkonono kuzui kupata ujauzito lakini anakufata mwanamke mwenzako akitaka ushauri kwako na yeye anataka kujiweka njia ya uzazi wa mpango kama yako na wewe unamwambia ni hatari inasababisha maradhi lukuki ilhali wewe umejiweka ...!!
Acha roho mbaya ...
Mwache Dada akasome ...

Msonyooo!
 
Alhamdulillah .. nashukuru kwa kila aliyenishauri.. leo majibu ya kidato cha nne... nami ni miongoni mwa waliofurahi.

Nimefanikiwa kupata II.20

Naamua kuendelea na safari nitarudi tena kwenye hii post 2023 july.
 
Alhamdulillah .. nashukuru kwa kila aliyenishauri.. leo majibu ya kidato cha nne... nami ni miongoni mwa waliofurahi.

Nimefanikiwa kupata II.20

Naamua kuendelea na safari nitarudi tena kwenye hii post 2023 july.
Hongera sana mkuu
 
NIMERUDI TENA. ALHAMDULILLAH LEO TENA MATOKEO YANGU YA FORM SIX YAMEKUJA MAZURI MNO NAMSHUKURU .

SHUKRANI KWA WOTE MLIONIPA MOYO.
Hongera sana kwa matokeo yako mazuri nakushauri uishi kama uliye elimika na si uliyesoma.
 
Wazima wana Jf.
Kama nilivyoeleza kwenye kichwa cha habari hapo juu.

Nina umri wa miaka 31. Nilimaliza shule ya msingi miaka 18 iliyopita. Sikufanikiwa kuchaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari. Japo nilitaka sana kuendelea lakini hali ya nyumbani ilikuwa ngumu mno hivyo ikashindikakana hata kwenda zile shule za taasisi enzi zile.

Katika purukushani za maisha nilijichanga kipesa mwaka 2006 nikajiunga na elimu ya watu wazima ila majibu hayakuja mazuri bado nikashindwa tena kurudia kutokana na hali ya kifedha. Nikajitahidi tu kwenda English course nashukuru nimejua kingereza na pia nikasoma french course pia kifaransa najua.

Ila bado najiona sijakamilika bila elimu ,nataka kusoma. Mpaka leo hii kiu yangu nisome nifike chuo hasa. Japo naona watu wanaambizana haina haja ya kusoma bora kujiajiri lakini kujiajiri bila elimu sidhani kama unaweza fika mbali unless watu wakuendeshee.

Nina watoto 3 na mume pia.
Ila bado naitaka elimu ya sekondari.. na mara hii nimejipanga vizuri kabisa.
Je niko sahihi ama ndio nakumbuka shuka kushakucha??

Ushauri wenu ni muhimu sana kwa hili
Nannahitaji faraja na munipe moyo niweze kufanikisha hili

Natanguliza shukrani.
Mvp ,mbona Kama wew ni msomi mwandamizi
 
Mwaka 2005mwalimu mchungaji komba aliamua kumuandikisha mke wake fom one ktk shule ya kolila , mkp tunapozungumza sasa HV Yule mam Ni headmaster wa shule moja hapa mpwampwa ddm
 
Alhamdulillah .. nashukuru kwa kila aliyenishauri.. leo majibu ya kidato cha nne... nami ni miongoni mwa waliofurahi.

Nimefanikiwa kupata II.20

Naamua kuendelea na safari nitarudi tena kwenye hii post 2023 july.

Form 4 ulitumia kituo gani kurudia mtihani
 
Sikurudia mtihani kwa maana sikuwahi kuufanya.

Ila nilifanyia kituo cha Yeshua
 
Back
Top Bottom