Nataka kuachana na ualimu

Rjohn usithubutu kuacha ualimu kuwa mbunifu utafanikiwa hakuna kazi utakayokuwa huru kama ualimu ni kazi gani ambayo ni ya kuajiriwa halafu unapata muda wa kufanya shughuli zako bila tabu unajipa likizo kiulaini jishughulishe usisubiri serikali ikutambue jitambue mwenyewe kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe

Siyo kweli!!!!

Hakuna kazi inayohitaji muda mwingi kama ualimu. Mwalimu anapaswa ajiandae kufundisha, atoe kazi na asahishe kazi ya kila mwanafunzi ili kupima/kutathmini kama kila mwanafunzi ameweza kufikia malengo ya somo. Mwalimu pia hufanya kazi zingine nje ya darasa hasa malezi katika nyanja mbalimbali mfano michezo, tabia/maadili nk. mwalimu husimamia usafi na shughuli nyingine kwa lengo la kumjenga mwanafunzi kiakili, kitabia/mwenendo na kiroho.

Watu wengi huishia kusema walimu wana muda mwingi wa kufanya mambo binafsi kwa sababu wanawaona walimu wanakaa bila kazi. Kimsingi walimu na watumishi wengi wa serikali hawatekelezi majukumu yao inavyotakiwa. Madhara ya walimu kutotekeleza majukumu yao kama inavyotakiwa tunayashuhudia... mfano wanafunzi kumaliza darasa la saba hawajui kusoma. kuandika na kuhesabu. Hali ya elimu sekondari pia inadidimia siku hadi siku.
 
ualimu ni janga, ila nakushauri nenda kafanye kazi ya kufundisha ili upate mtaji wa kujisomesha maana ukifika kule unaweza kupata mkopo wa kuweza kujisomesha ila usitegemee kufanya kazi hii,

Kama ualimu ni janga nani atafundisha watoto wetu kwa manufaa ya taifa letu?
 
Siyo kweli!!!!

Hakuna kazi inayohitaji muda mwingi kama ualimu. Mwalimu anapaswa ajiandae kufundisha, atoe kazi na asahishe kazi ya kila mwanafunzi ili kupima/kutathmini kama kila mwanafunzi ameweza kufikia malengo ya somo. Mwalimu pia hufanya kazi zingine nje ya darasa hasa malezi katika nyanja mbalimbali mfano michezo, tabia/maadili nk. mwalimu husimamia usafi na shughuli nyingine kwa lengo la kumjenga mwanafunzi kiakili, kitabia/mwenendo na kiroho.

Watu wengi huishia kusema walimu wana muda mwingi wa kufanya mambo binafsi kwa sababu wanawaona walimu wanakaa bila kazi. Kimsingi walimu na watumishi wengi wa serikali hawatekelezi majukumu yao inavyotakiwa. Madhara ya walimu kutotekeleza majukumu yao kama inavyotakiwa tunayashuhudia... mfano wanafunzi kumaliza darasa la saba hawajui kusoma. kuandika na kuhesabu. Hali ya elimu sekondari pia inadidimia siku hadi siku.

kama serikali na jamii haitambui umuhimu wa walimu kwa nini usihangaikie maisha yako
 
km ww ni comitted teacher kwa sasa utakufa masikini ukiwa serikalini, ila kama mzugaji ualimu bado utakulipa (free time)
 
Unataka ukasome nini au unapendelea nini? au huna mwelekeo kokote kule poa tu.Ni ngumu kutafuta kazi ukiwa huna kazi.Inaonekana una msongo wa mawazo na unataka kutoka kiuchumi mapema.try your lucky unapoona utatoka.kuomb ushauri jamii forums lazima uwe una sehemu ya kuanzia maan ushauri w humu ndani sometimes unahitaji akili,kama mimi nakushauri ukagombee udiwani au ubunge kwa sababu ndo unaolipa
 
mimi ni mwalimu nakushauri acha ualimu.
unaweza kuacha ualimu kwa busara ya kujiendeleza kwenye fani nyingine lakini uwe na uhakika unarefa ukimaliza masomo yako maana kwa tanzania kazi inayopatikana kwa kutopigiwa sound na marefa ni ualimu pekee, ndio maana wengi tuliosomea na tunaofundisha ni watoto wa watanzania wakawaida/walalahoi.
kwa ujumla tunavumilia kuwa walimu na wala hatujivunii kuwa walimu hapa tanzania.
 
Mwl. JK Nyerere na Al Haji AH Mwinyi wote hawa ni walimu, fuatilia walivyojigaragaza kama jongoo kichaa na kuibukia ikulu na kuishi 'chiza' maisha yao yote. Ukiisha fuatilia, fuata nyayo zao.
 
Back
Top Bottom