Natafuta rafiki wa kike (girlfriend) wa kubadilishana naye fikra na uzoefu wa mambo mbalimbali.
Wasifu Wangu
* Mfupi kiasi, 5'5 ft, Maji ya kunde
* Umri,miaka 28
* Ni mkristo
* Nina kazi
* Napendelea kucheza mpira wa miguu, kucheza pool table, kuogelea, kuendesha baiskeli, kufanya kazi kwa bidii, kusafiri, kusikiliza na/au kuandaa/kutengeneza muziki. Napenda pia mara chache chache kwenda baharini kupunga upepo.
* Ni mcheshi
* Napenda kujifunza mambo mapya
* Nashaurika katika mambo yenye mantiki.
* Makazi: Dar es Salaam
Ningependelea kupata rafiki mwenye sifa hizi
* Awe na umri usiozidi miaka 30
* Mrefu wa wastani
* Awe mweupe kiasi, (sio weupe wa mkorogo)
* Mnene wa wastani ama mwembamba
* Elimu, angalau kidato cha sita
* Awe mcheshi na mwepesi kujifunza
* Sibagui rangi ya mtu (kwa maana ya Uhindi, Uarabu, Uzungu, Uafrika ama Uchotara)
Mwenye sifa mwafaka anitumie PM kwa kujiamini kabisa, nitajibu bila kusita.
Nashukuru!
Mkuu Idimi
PM yangu bado Kimyaaaaaaaaaa!
Kwamba hawapo wenye sifa hizo ama?
Kwi kwi kwi!Tee tee teh,, hatimae mambo yameiva, Idimi huenda akawa amepata rafiki!! hongera Idimi.
Ram, poa sana umempa ndugu yetu ka hope kidogo ..let's hope it will end up well!
Halafu useme huna bahati Idimi,umeonyesha ubaguzi wa wazi kwani marafiki zako wote wapo less than 30 plus na vigezo vyako vyote ulivyotoa!! kwi kwi i doubt if you real need a friend or.....
Hujapata tu mkuu? nasubiri nione kama utapata na mimi niombe.Binafsi nataka wa kike kigoli asiwe ex wa Lyumba
Kwi kwi kwi!
We binadamu (mtu), acha utani mshikaji!
Akikusikia huyo mwombaji wa urafiki kwangu kwamba unamhisi alipita kwa Liyumba mtashikana makoti!
Bado naendelea na 'negotiations' na huenda mambo yakawa freshi muda sio mrefu. Ila sorry, sitaanika jina lake hapa wala detailz zake zingine, nitasema tu kuwa kapatikana!
Ningependekeza uendelee na maombi ya huyo umtakaye, hapa JF hakuna kitu kinaharibika