Natafuta pikipiki ya mkataba ya kuendesha

Natafuta pikipiki ya mkataba ya kuendesha

Wiwachu

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2018
Posts
809
Reaction score
926
Wakuu kama ilivo ada nawasalimu wote baada ya salam husika na kichwa cha habari kama kinavyojieleza mimi ni baba wa mke mmoja na watoto 2 wote wanasoma, naishi Dar maeneo ya Tabata nina mali zisizo hamishika kama kiwanja chenye pagara ambalo bado kuezeka tu cha vymba vi3 maeneo ya Kifuru.

Nina hitaji pikipiki ya mtakaba ambayo baada kumaliza mkataba itakuwa yangu iwe mpya au iwe imetumika kiasi tutaiangalia na tutakubaliana muda wa mkataba na kiasi cha kuwa nampa boss kila wiki nk pikipiki iwe Tvs yoyote 150, au 125 au Boxer 125 au 150 aina nyingine pia naweza kuchukua inategemeana ila hizo tajwa hapo juu ndo ambazo zinahit sana kwa kazi ya bodaboda na ndo wateja wanazipenda sana si mnajua tena abiria wa jiji la makonda yaani dar wanachagua hata daladala ya kupanda DCM hawapandi wataka Coastal mayai nk, yaani kitu pamba kama wanataka ya kununua vile

Hata kama upo mbali kiasi gani tuna weza kuingia makubaliano ama mkataba na mambo yakaenda poa sana kuhusu malipo ya hesabu hata kwa njia ya M-pesa, Tigo pesa au airtel money niko tayar kutuma kwa njia hizo kwa yeyote alie nayo au anaetaka au kutafuta muendesha pikipiki nipo tayar kufanya kazi nae. Kwann unipe mimi pikipiki yako mimi ni mwaminifu sana cjui kudhurum cha mtu naamini kweny kupambana maana hamna aliezaliwa na mali vyote tunavyoviona hapa dukani tumevikuta kwa iyo ni bidii yako tu ya kuchakarika na Mungu akihuska pia ..

Asanteni sana niko tayari hata leo ni wewe tu unasubiri nini pikipiki,,zinalipa ikinunua mfano mpya million 2.2 au 2.3ml unapata 3.5ml au kukuu yaani ikiyotumika ambayo bado iko kweny hali nzuri kwa 1.1ml au 1.3 ww unapata 3ml jmn hiyo faida inakuja tu ww umekaa hujui gharama za uendeshaji wala nini ww ni kuletewa hesabu tu kila wiki ukiwa nazo kama pikipiki 5 huoni mambo uqnajiseti yenyewe kabisaa hapo. Kwa mawasiloano zaidi njoo Pm tupeane namba za cm tuyajenge..

SOMA MREJESHO WA HUU UZI HUTAJUTA. ... Dah nmeukumbuka uzi wangu aisee.. Naleta hapa merejesho wa uzi.. Baada ya uzi huu siku ziliennda sikufanikiwa kupata pikipiki kwa wakati ila Mungu alinijaalia nikapata hera nikanunua pikipiki yangu maana kuna walio nishauri niuze pagare wengine nikope pesa kweny taasisi za kifedha kupitia pagare lakin haikuwa hivo hera niliipata kupitia kitu kingine changu nilichouza nikapata pikipiki ya ml1.25 ambayo mpaka sasa naandika comment hii ndo natumia ninayo ni miaka miwili sasa na hera yangu isharudi sasa nakula faida tu na niliinunua ikiwa tayar imetumika kwa mwaka mmoja

Sasa nina uzoefu wa kutosha kweny kazi hii ya usafirishaji wa abiria kutumia bodaboda maana naenda mwaka wa 3 sasa kwaiyo nmekuja hapa kama mlivoomba nilete merejesho kuwahasisha wengine.. Kiukweli kazi ni ngumu ila ukikomaa ukaacha anasa zote na starehe zote unatoboa aisee huwezi amini lile PAGARE LANGU MLILOKUWA MNANISHAURI NILIUZE NA WENGINE NILIKOPEE HERA BANK SASA NILIPAUA NA SASA NMEHAMIA KABISAA NAISHI SASA NAISHI KWANGU SILIPI KODI TENA NA MIMI NAITWA BABA MWENYE NYUMBA

Niliwaambia mimi ni mwaminifu na kwa haya unaeza kuona uaminifu wangu changamoto za kazi hii ni starehe, wanawake yaani mademu na michepuko nk... Nakumbuka mimi nilianza kipindi kigumu sana kile cha corona imechachamaa kweli kweli mwezi wa 4 mwka 2020 nadhani wote mnakumbuka ilikiwaje hali tete na watu hata kazini hawaendi wanashinda wamejifungia makwao lakini hali baadae ilikaa ssawa na watu wakaanza kutoka kwenda makazini na shule zikafunguliwa pia sasa nmeanza kupata connection za wateja ama abaria, japo mafuta nayo yanapamda kila mwezi sasa lita ya petrol ni 3148 na point kadhaa ila tunapambana kiume na hali yetu.

nikuombe kama uko mitaa ya tabata yote ila hasa segerea, kinyerez ama kifuru nifanye niwe bodaboda wako mimi ni mtu mzima kiasi sio sana na ninajua kutunza siri za abiria pia ni mwaminifu sana hutajuta nikiwa bodaboda wako aisee lakini pia hata ukiwa mbali kidogo ila unasafar ya mbali naweza kuja ila kama ni safar ya karibu ya 1000 au 2000 ninaweza kuja kama nikiwa jirani nawe pia kama unauza bidhaa online na unataka kuwa pelekea wateja wako mahali popote ndani ya dar au pwani nafanya kazi hizo pia au uko home na hutaki au husikii kutoka kwenda dukani kufata mahitaji yako nk naweza kukununulia na nikakuletea ulipo na ukanilipa kwa mawasiliano zaidi 0756695846, 0712776823 Asanteni sana wote kwa ushirikiano wenu tupo pamoja.
 
Asante sana mkuu kwa ushauri ila nashindwa kufanya ivo kwa sababu unaweza kuuza harafu ikala kwako kupata tena pagare kama hilo na sehemu kama iyo harafu viwanja vinapanda sana kila mwaka mkuu.
Wazo zuri,ila kwa ushauri wangu,uza Hilo pagale milioni 10,nunua pikipiki 4 upige kazi,
 
Asante sana mkuu kwa ushauri ila nashindwa kufanya ivo kwa sababu unaweza kuuza harafu ikala kwako kupata tena pagare kama hilo na sehemu kama iyo harafu viwanja vinapanda sana kila mwaka mkuu
huo Sasa Ni uoga,Kama una hakika biashara inalipa uza utanunua kiwanja kingine,pengine hata ukaja kununua nyumba kabisa
 
Asante mkuu lakin mambo ya ardhi si unayajua mara nyingi ukitumia hera uliouza nyumba au kiwanja kwa mambo mengine huwa haifiki mbali sasa unajikuta umepoteza ila nashukur kwa mawazo yako mkuu
huo Sasa Ni uoga,Kama una hakika biashara inalipa uza utanunua kiwanja kingine,pengine hata ukaja kununua nyumba kabisa
 
Tatizo namba moja la uwekezaji kwenye jambo lolote Tanzania ni uaminifu. Ukitoka hapo ndio mambo mengine yanaweza kufuatia sasa. Watu hawaaminiani, na ukiwaamini hawaaminiki na ni vigumu kujua yupi ni yupi kwa sababu 98℅ hivi ni pasua kichwa.

Wewe unaweza kuwa mtu mzuri sana tu, lakini kasheshe sasa ni kujiridhisha na hilo.

Zaidi ya hapo nakutakia kila la heri. Wewe na atakayekupa pikipiki, ni vyema baada ya mwaka mkaleta mrejesho jinsi mlivyofanya kazi pamoja, changamoto na fursa ili kuwavutia wengine
 
Asante sana mkuu kwa maoni na ushaur wako hakika kila jambo msingi wake ni uaminifu kama ulivosema natamani nipate mtu wa kuniamini ili awe shuhuda kwa wengine humu maana inaonekana imani kati yetu imepungua sana

aidha niko tayar kumuinesha wapi nakaa na kumpeleka kweny hilo pagare langu na kumuonesha hati zake na vitambulisho vyangu ili aone kama kweli ni mali yangu lakini pia hata kuonesha kwa majirani zangu huko kweny saiti yangu pia siku ya kwenda yy ndo anatangulia na kuwauliza kama kweli mimi ndiye mmiliki wa hilo pagare mimi stakuwa mzungumzaji sana..

Jf naianimi sana imewasaidia wengi na kuwakomboa na changamoto mbali naamini hata mimi nitapa wa kunishika mkono maisha yamenikalia kinyume kwa wakati huu nahitaji msaada wenu aisee na nitashukur sana.
Tatizo namba moja la uwekezaji kwenye jambo lolote Tanzania ni uaminifu. Ukitoka hapo ndio mambo mengine yanaweza kufuatia sasa. Watu hawaaminiani, na ukiwaamini hawaaminiki na ni vigumu kujua yupi ni yupi kwa sababu 98℅ hivi ni pasua kichwa.

Wewe unaweza kuwa mtu mzuri sana tu, lakini kasheshe sasa ni kujiridhisha na hilo.

Zaidi ya hapo nakutakia kila la heri. Wewe na atakayekupa pikipiki, ni vyema baada ya mwaka mkaleta mrejesho jinsi mlivyofanya kazi pamoja, changamoto na fursa ili kuwavutia wengine
 
Nina piki piki ni mpya aina ya mahindra ....vipi hiyo tunaweza kufanya biashara kwa siku sh ngapi utanipa !! Ukitimiza mkataba bila quick nakupa inakuwa yako

sent from toyota Allex
 
Mkuu ina cc ngap na je naweza pata picha yake hapa niione harafu mambo mengine yaendelee
Nina piki piki ni mpya aina ya mahindra ....vipi hiyo tunaweza kufanya biashara kwa siku sh ngapi utanipa !! Ukitimiza mkataba bila quick nakupa inakuwa yako

sent from toyota Allex
 
Wakuu bado sjapata pikipiki kwa iyo nawakaribisha sana
 
Uza pagare nunua bajaji watoto waende shule na maisha yasonge mbele, pikipiki unaweza ibiwa huku dhamana ni pagare ukashangaa pagare zima limeenda kwa milioni 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu siwezi kuweka dhamana pagare labda tu kukupeleka upaone ili kujiridhisha awe na imani nami ila sio kuweka kama dhamana
Uza pagare nunua bajaji watoto waende shule na maisha yasonge mbele, pikipiki unaweza ibiwa huku dhamana ni pagare ukashangaa pagare zima limeenda kwa milioni 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jmn bado sjapata pikipiki kwa anaetaka dereva wa bodaboda aje tufanye kazi nipo tayari.
 
Mkuu siwezi kuweka dhamana pagare labda tu kukupeleka upaone ili kujiridhisha awe na imani nami ila sio kuweka kama dhamana
Unaposema huwezi kuweka pagale kama dhamana huoni unawafanya watu watilie shaka nia yako na uaminifu wako pia? Maana kama una uhakika na hiyo biashara na wewe ni muaminifu kwanini unaogopa kuweka pagale lako kama dhamana ili mtu akupatie hiyo pikipiki?
 
Inatakiwa pesa hii
1578894853503.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni namba gani c au b naje inaenda kwa sh ngap
 
Mkuu uweke dhamana pagare kwani unanikopesha!?? Yaani pikipiki mfano kukuu hata 1 5M haifiki unataka niweke pagare langu la 15M dhamana haiwezekani mkuu wewe ukijua pagare lilipo na ninapoishi inatosha kwani wote wanaoendesha hizo bodaboda wana mapagare wanayo weka kama dhamana!?? Kama ni hivo si bora nikakope bank mimi kama mimi sasa
Unaposema huwezi kuweka pagale kama dhamana huoni unawafanya watu watilie shaka nia yako na uaminifu wako pia? Maana kama una uhakika na hiyo biashara na wewe ni muaminifu kwanini unaogopa kuweka pagale lako kama dhamana ili mtu akupatie hiyo pikipiki?
 
Uza pagare nunua bajaji watoto waende shule na maisha yasonge mbele, pikipiki unaweza ibiwa huku dhamana ni pagare ukashangaa pagare zima limeenda kwa milioni 2.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwann hili wazo asilifanyie kazi, Inavyoonekana hata yeye hana uhakika wa aina ya biashara anayotaka kufanya kwa maana kama malipo yapo why asiuze au akachukulia mkopo bank kwa hilo pagale lets say akapata 10m ambayo anunue bajaj na bodaboda moja ambavyo ndan ya miaka miwili amerudsha mkopo wote bank?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom