Natafuta mke wa kuoa 2016 mwezi wa nne

Natafuta mke wa kuoa 2016 mwezi wa nne

mmp

Member
Joined
Sep 10, 2014
Posts
33
Reaction score
2
Habari Wakuu,

Najitokeza kutafuta mke wakuoa, mimi ni mwanaume rijali naishi Dar. Sifa zangu situmii kilevi chochote. Ni maji ya kunde, mwenye umri wa miaka 32, sina mtoto.

Nimtafutae awe na miaka 24-34, awe mweupe, awe anajishughulisha na kazi yeyote mjasiriamal au mwajiriwa, asiwe na mtoto, elimu kuanzia Degree na kuendelea.

Kama upo serious na unahitaji la kuolewa karibu

Ni Pm weka namba yako
 
We unajishughulisha na nini na umetaka awe na degree we are unayo na je huko Kazini kwako au mtaani kwako hujamuona kabisa anayefaa je mara YA mwisho kuwa na girlfriend ni lini na kwanini mliachana jibu swali Kwani cv yako haijitosherezi
 
Nenda kambi ya fisi au magomeni kwa macheni bar kama uko dar na kama uko Arusha nenda mrina bar au shivazi au matejoo mkuu.

swissme
 
Mbona umesema we ni maji ya kunde sasa kwanini utake mweupe?
 
We unajishughulisha na nini na umetaka awe na degree we are unayo na je huko Kazini kwako au mtaani kwako hujamuona kabisa anayefaa je mara YA mwisho kuwa na girlfriend ni lini na kwanini mliachana jibu swali Kwani cv yako haijitosherezi

Na kweli haijajitoleza kabsa
 
Unamtaka utakaye muoa mwezi wa 4 mwakani??, ina maana ukimpata leo baada ya miezi michache tu uanze michakato ya ndoa?? kaka usiikomoe nafsi yako, inawezekana umetafuta kwa muda mrefu hujapata, ndio umeamua kuja kwa gia hii!! acha, huo muda ni mfupi sana kukaa na mtu usiyemjua na gafla kumuoa. Nakushauri hata ukimpata panga uoe walau mwishoni mwa 2016, lengo ni kupata walau mwaka 1 tu wa kuwa makini na kumsoma vitu vingi. Kila lakheri.
 
Hujakamilisha cv yako mkuu,elimu yako je? unafanya shughuli gani hapa mjini.... tujuze I might be your future wife
 
Unahitaji mke alie ajiliwa au mjasilia mali na awe na degree:what: je wewe level yako ya elimu ni ipi? Na unajishughulsha na nin? Girls angalien sana hawa watu..
 
Ivi kweli jamani maeneo unayoishi,unayopita,au maeneo uanyofanya kazi umekosa mwanamke ambae anakidhi vigezo vyako??
Sijui ni umekata tamaa au laa ila nikutie moyo mkuu fanya sana ibada mke si kitu cha kusema unatafuta kwa style hii...Tunaweza kukusaidia apa alafu akawa sio chaguo lako,keshokutwa ukaja apa ooohh mke kafanya hiki kafanya kile...
ibada muhimu,Mungu anajua hitaji lako
 
Mkuu hata ukimpata humu kwenye jukwaa lazima umchunguze kwanza,usikurupuke tu kutangaza ndoa(mjue vizuri,ijue family yao n.k).........cha msingi sali/swali sana kwa Mungu maana maandiko yanasema "mtu hupata mali kutoka kwa wazazi wake ila mke mwema hupewa na Mungu tu"
Kila la heri.
 
Huu ni utani labda...kutafuta mke hapa kisha utangaze siku ya ndoa.Bora nikupe number upate "call girls"
 
Sifa zako ulizotoa hazijitoshelezi. Na, katika umri wa miaka 32 uliyoishi hujawahi kukutana na mdada ambaye unaweza kumpa nafasi ya kuwa mkeo mpaka umtafute mtandaoni, tena wa kuoa fasta? Inawezekana una matatizo. Anyway, all the best.




s
 
Inaonekana wewe ni mchaguzi sana,jipange upya suala la ndoa ni pana sana sababu linahusisha hisia na upendo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom