Natafuta meneja wa kunidhamini mimi ni msaani chipukizi

Natafuta meneja wa kunidhamini mimi ni msaani chipukizi

OME123

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2010
Posts
1,497
Reaction score
606
Wana jf mimi ni kijana miaka 23 ndo nachipuka ki muziki,nahitaji meneja wakuniwezesha ili nitoke na nitambulike.nikk vizuri sana nimeshafa maojiano na vituo mbalimbali za redio na tv na mpaka sasa nimetoka single mbili na hata kwenye you tube unaweza kuzicheki kazi yangu.aksanteni
 
Weka wimbo hapa tusikilize acha ushamba eti tutakuibia nana aibe, au unategemea kuuza hizo single uwe tajiri ebu jiongeze kiki mjini ndiyo kuuza kwenyewe.
 
Dogo weka ngoma apa watu wasikilize kama unafaa au weka jina unatumia jina gani la kisanii
 
Unajitahidi lakini kwa upande wa kuimba jitahidi uwe na Melody, Sauti na pia ujue kuandika, Kila la kheri
 
Umeingia kwenye muziki kwa ukosefu wa ajira au ni kipaji? OK, sasa hivi jaribuni kuangalia tunasema Social Problems/matatizo ya kijamii ndy myafanyie kazi. Nyimbo za inspiration ni nzuri kwa kipindi hiki kwa sababu utapata promo sehemu mbalimbali katika mashirika makubwa na hata serikalini. Siyo lazima muimbe mapenzi tuuuuuuuuuuuuuuu mpaka sasa tumechoka na mapenzi, mfn. Kuna mabadiliko ya tabia nchi, kuna njaa, mimba za utotoni, vijana kuacha shule, madawa ya kulevya, etc. Kuwa Mwalimu kupitia muziki wako na siyo kuwa mwanamuziki bila wanafunzi.
 
Aksanteni sana kwa ushauri ntazifanyia kazi wazee.
 
Nimeisikiliza nyimbo yako
Bado Sana
Ila never give up[emoji123][emoji123]
 
Nimecheki wimbo wako,

Unajua. Unajua. Unajua.

I can see something inside you, put it up Braza.

Sijajua upo mkoa gani ila kama upo Dar jitahid Kwenda THT kwa ruge ili upate msasa zaidi wa muziki halafu ulale mbele au ukutane na maprodyuza wengi ili upate platform ya kujuana na wadau.
 
Nimecheki wimbo wako,

Unajua. Unajua. Unajua.

I can see something inside you, put it up Braza.

Sijajua upo mkoa gani ila kama upo Dar jitahid Kwenda THT kwa ruge ili upate msasa zaidi wa muziki halafu ulale mbele au ukutane na maprodyuza wengi ili upate platform ya kujuana na wadau.
brother niko mwanza
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom