Natafuta mdada wa kuzaa naye

Typing error. Neno la kiswahili ni Shahada.
Niwashauri vijana wa miaka ya hivi karibuni kwamba,, unaposoma andiko fulani, jikite zaidi kuuelewa ujumbe uliopo kwenye andiko hilo na sio usome huku ukitafuta cha kukosoa kwenye andiko hilo, tabia hii ni ujinga wa hali ya juu sana. Mwenye kutaka maarifa atanielewa namaanisha nini na atajitafakali lakini mpumbavu ataendelea kukosoa makosa ya kimaandishi badala ya kukosoa ujumbe uliomo kwenye andiko kisha kutoa maoni yake.

Nitolee mfano,
Mtu mmoja hapo juu kauliza, " mwezi April ulikuwa na diploma, leo September una bachelor?, Tuambie hicho chuo kinachotoa bachelor ndani ya miezi minne."

Ni hivi , kipindi naandika ujumbe huo nilikuwa ninamiliki cheti cha diploma wakati huohuo nikiwa mwaka wa tatu nikimalizia kusoma Bachelor Degree in........, Na sasa nimemaliza na matokeo yametoka sina supplimentary, unadhani leo nilipoandika andiko hilo ningesema kwa sasa nina diploma ???.
Kwa mtu mwenye akili na mwenye kufikilia kabla ya kutenda angejiuliza maswali kadhaa kabla ya kukutupuka kuja kuhoji swali la kitoto kama hilo.
Binafsi mtu huyo na mwingine wa aina hiyo nimewaza na kuwaona ni wapumbavu, walikwenda shule kujifunza ujinga, walikwenda shule kuchukua cheti na si maarifa, ndio hao wanaoshinda vijiweni wakiilalamikia serikali haiwapi ajira wakati serikali iliwapa mikopo wakasoma akili zao zinawatuma serikali iliowapa mikopo ndo hiyo hiyo wanasubiri iwape na ajira pia na ndio hao hao wanaotaka kazi za raha raha tu hususani za kukaa ofisini wakiwaza kuiibia serikali na kupiga madili, wanaamini msomi yeyote alitoka kimaisha kwa njia za madili tu na sii taaluma na uwezo wake, ni watu pia wanaoamini kazi hupatikana kwa njia ya CONNECTION na si uwezo binafsi, ndio maana wamegeuka kuwa na wasomi "makasuku" wanaokariri bila kufikiri, Fikra zao ni Tasa, hazigawanyiki kuwaza mambo kwa upana zaidi.

Niwatakie jioni njema wale wenye akili na maarifa lakini kwa wale wajinga wanaojiona kuwa wao ni sahihi kwa kila kitu waendelee kubanua madomo yao vijiweni.
Sawa mkuu umesikika, haya wewe una maarifa gani?
 
Kuna mtu anaitwa allency nimemjibu kwa kirefu msome hapo chini maana alikuunga mkono kwa swali lako,
Kwa jinsi ulivyoelezea hapo juu kuhusu diploma na degree yako, ni rahisi mtu kukuelewa pasi na ufafanuzi ulioutoa? Au kwa sababu wengine tulienda shule kusomea ujinga(kwa maoni yako) ndiyo maana tulishindwa kuelewa?
 
mwamba tafuta mwanamke uowe acha kuja na mambo kama haya kwenye social media ..unatufanya wote tuonekane vilaza......

kama unatamani sana watafute huko mitaani ..humu sidhani kama kunamtu yupo tayari kufanya huu upuuzi

Cha ajabu kilaza unaweza kuwa wewe kupita huyu mwamba

Niamini mimi huyu anaweza kuwa na sababu za msingi kukupita wewe
 
Cha ajabu kilaza unaweza kuwa wewe kupita huyu mwamba

Niamini mimi huyu anaweza kuwa na sababu za msingi kukupita wewe
na wewe ni kilaza na mpuuzi mwingine........umeambiwa mjibie..kama unata kumzalia mfate PM...
 
Au mkeo anashida ya uzazi?
Utawapata tu siku hiz wasichana wengi hawataki ndoa wanataka kuzaa tu
 
Kwa jinsi ulivyoelezea hapo juu kuhusu diploma na degree yako, ni rahisi mtu kukuelewa pasi na ufafanuzi ulioutoa? Au kwa sababu wengine tulienda shule kusomea ujinga(kwa maoni yako) ndiyo maana tulishindwa kuelewa?
Mkuu, kwa mtu mwenye kusoma andiko na kutafakari kwa kina kabla ya kukimbilia kuanza kubeza na kuzomea angeweza kufikiria na kuelewa na kama kuna shaka yoyote angeuliza kwa lugha ya staha ili nitor fafanuzi, mimi naamini msingi wa maarifa na uelewa wa mambo huanza na busara kwanza, yaani kuwa mvumilivu katika mashauriano, utambuzi wa hii nadharia, "unaloona wewe kuwa ni sahihi kwa hoja zako za msingi, kuna mwingine analiona ni ujinga wa hali ya juu" katika mijadala huwa tunatafuta "balancing point" yaani wote tufikie mahali tukubaliane kwa kushawishiana kwa hoja.
Jambo la kusikitisha unakuta mtu msomi ana elimu ya kiwango cha shahada lakini akisoma au kusikiliza hoja fulani, anakimbilia kubeza na kumtukana mtoa maada au anajikita kukosoa makosa ya uandishi licha ya ujumbe kueleweka kiufasaha.
Bahati mbaya watu wa aina hii ni wengi mno mpaka wanawameza na wengine wenye hekima.

Ushauri wangu ni kwamba:-

1) Tunaposoma andiko fulani, tujikite katika kuelewa ujumbe uliomo katika andiko hilo

2) kila msomi makini aamini katika nadharia hii, "upumbavu wa mtu ni hekima kwa mwingine" hivyo asiamini kwamba kila aliwazalo yeye ni sahihi kila mala.
Yaani, unaweza kujiona wewe una akili sana na lakini jua kwamba kuna mtu mwingine anakuona ni mpumbavu kuliko kawaida, na huyo anaekuona wewe ni mpumbavu kuna mwingine anamuona yeye si kitu hata kidogo, hivyo mashauriano ni mhimu kufikia lengo na kuzuia migogoro mahali popote.
Kaulimbiu*

" HOJA DHAIFU HAIPIGWI RUNGU BALI HUSHINDWA NA HOJA NYINGINE ILIYO BORA ZAIDI" JK Kikwete.
 
Bachelar enheee?
Yaani andiko lote hujauelewa ujumbe uliomo na badala yake umeenda kushangaa typing error!!,
Eeeh, aisee hii Elimu yetu ya kukaririshana mambo ya grammar, structure, uandishi wa report pindi tunapojiandaa kumaliza vyuo ni ujinga mtupu,, wasomi wa siku hizi ni mabingwa wa uandishi wa report lakini hawana uwezo wa kiakili wa kuchambua ujumbe na maudhui yalioandikwa kwenye report.
Mkuu nikushauri tu, hata kama elimu yetu ndio inatuongoza kuwa wajinga kiasi hiki, ni busara tukiishapata vyeti tujaribu kujielimisha wenyewe, njooni mtaani ndiko kuna vyanzo vya maalifa, tokeni mafichoni mje,, mtaani watu wengi hawana maarifa ya grammar, hawajui kuandika report, hawana mishahara mwisho wa mwezi lakini wanaishi na familia zao zinaenda vuzuri. Ni akili, uwezo wa kuziona fursa na kuaminiana ndiko kunawafanya wawe huru na hawailalamikii serikali juu ya upatikanaji wa ajira kama wasomi wa kileo walio wengi.

Nikuage kwa kukwambia hivi, Hizi elimu zetu tunazozipata chuo zisitufanye kuwa wajinga kiasi hiki, uwezo wako wa kukosoa neno "Bachelor" lenye kosa la kiuandishi yaani "Bachelar" halikufanyi uonekane msomi bali linakufanya uonekane mtu uliekariri mbele ya watu wenye uelewa wa mambo, Andiko lenye maneno 600 kukitokea kosa moja la kiuandishi hakuwezi kuufanya ujumbe wote uliomo kuwa batili, ni mjinga pekee tu ndo atajikita kukosoa makosa ya "kiuandishi" na badala ya kukosoa makosa ya "kimaana" yaani ujumbe.

Lu^2.
 
mwamba tafuta mwanamke uowe acha kuja na mambo kama haya kwenye social media ..unatufanya wote tuonekane vilaza......

kama unatamani sana watafute huko mitaani ..humu sidhani kama kunamtu yupo tayari kufanya huu upuuzi
Aisee! Nimechunguza kwa makini sana wanaonijibu kwa matusi na kejeli ni wanaume na si wanawake, nimewaza sana nikadhani kuwa huwenda ni "Mashoga" ila nafsi inakataa kuamini hilo, nmehitimisha kwa kuamini watu hawa wanaocomment kwa kutukana ni wajinga tu hawajui maana ya mijadala, unakuta mtu anacomment hapa kwa matusi na dharau wakati ukimprofile unagundua kuwa yeye mwenyewe amebebesha mimba wadada wa watu kisha akakimbia majukumu, wadada wamezaa halafu tumizi hatoi, wadada wanajilelea watoto wao bila msaada wowote ule, wakati huo huo janaume zima linajinadi kuwa lina watoto huku halipeleki tumizi lolote kwa hao liliowapa ujauzito, nadhani anajijiua aache unafiki.

Mwingine nimemfuatilia nikabaini yeye mwenyewe mama yake alijipeleka kwa mwanaume ili azalishwe tu atalea mwenyewe kwa sababu aliona umri wake umekwenda sana akawa na hofu ya kuzeeka bila mtoto, mtu huyu leo ni kinara wa matusi na kukosoa maandiko ya wengine, jamani tuulizage chimbuko letu kabla ya kutukana badala ya kukosoa.
Unajifahau pia, kamuulize mama yako pia ndo uje tuzungumze.

Nashhkuru ujumbe umeeleweka na tayari kuna baadhi ya wadada wamekuja inbox nimeshawasiliana nao baaddhi pia wakanipa mawasiliano yao nitawaona kwa nyakati tofauti, tutakaefikia muafaka basi tutasonga mbele. Lakini kilichonikera zaidi ni kuona wanaume ndo wamekuwa mstari wa mbele kucomment kwenye andiko linalowahusu wadada tena lililobeba ujumbe wa mambo ya huba, jamani wanaume makini mjihadhali msijekujikuta mnaitwa mashoga kutokana na kuwa viherehere kucomment kwenye maada zisizowahusu.
 
Unajidhalilisha utu wako mitandaoni humu.
Toa ushauri sasa, kimbuka hata wewe kuna kuna jambo unafanya lakini kuna mtu anakuona kwamba unajidhalilisha.
Nashukuru ujumbe umefika na tayari ninaendelea na mazungumzo na baadhi ya wahusika niliowalenga.

Mkuu jitafakali sana aisee,, Yaani upo kwenye forum ya "LOVE CONNECT' Halafu unakosoa watu walioleta andiko linalohusu "love connect" kwenye forum hiyo ??? Kimekuleta nini huku??.

Elimu, Elimu, Elimu.
 
na wewe ni kilaza na mpuuzi mwingine........umeambiwa mjibie..kama unata kumzalia mfate PM...
Wewe nimekwambia uje kujihisi kuwa wewe ni kilaza kutokana na andiko langu??
Hii forum ya "Love connect" ipo kwa ajili ya mambo kama hayo nilioandika, walioandika codes kuunda hii forum walikuwa na akili na maana kubwa kuliko wewe ujue, Kilaza ni yule mtu anayetumia forum ya "love connect" kutukana watu waliokuja kutekeleza maana halisi ya forum hiyo ya love connect.
Wewe ni mwanaume,, ni kiherehere gani kimekufanya uje kudandia uzi unaowahusu wadada, au wewe ni shoga? Au mimi nimekutaka uje unizalie wewe ? Si nimeweka andiko mdada mwenye nia aje? Nini kimekuwashawasha mpaka ukurupuke huko kuja kucomment kwa kejeli andiko linalowahusu wadada?

JITAFAKALI, CHUKUA HATUA
 
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 31,
Naishi Dar es salaam- ubungo
Elimu : Bachelar
Ajira: mwajiriwa serikalini

Mdada nimtakae,

Awe na mpole na mwenye nia njema
Mzuri kiasi tu.
Umri: awe na umri usiozidi miaka 29
Mkazi wa Dar es salaam,
Elimu: Darasa la saba na kuendelea..

Ajira: asiwe na ajira au awe na ajira yoyote ni sawa tu,
Mimi nimejipanga kumhudumia mwenyewe, kikubwa akubali kubeba mimba tu, kujifungua na kushiriki kikamilifu katika kumlea mtoto wetu.

Dada aliyetayari kwa hilo aje inbox tuzungumze!.
Stress unazojaribu kuzikwepa sasa utazikuta mbeleni
 
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 31,
Naishi Dar es salaam- ubungo
Elimu : Bachelar
Ajira: mwajiriwa serikalini

Mdada nimtakae,

Awe na mpole na mwenye nia njema
Mzuri kiasi tu.
Umri: awe na umri usiozidi miaka 29
Mkazi wa Dar es salaam,
Elimu: Darasa la saba na kuendelea..

Ajira: asiwe na ajira au awe na ajira yoyote ni sawa tu,
Mimi nimejipanga kumhudumia mwenyewe, kikubwa akubali kubeba mimba tu, kujifungua na kushiriki kikamilifu katika kumlea mtoto wetu.

Dada aliyetayari kwa hilo aje inbox tuzungumze!.
Mkuu ina maana mtaani unapoishi hawapo? Chuoni uliposoma? Among your classmates? Kanisani au msikitini? Hata kule kijijini kwenu ulipozaliwa? Au unaogopa kurusha ndoano
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom