Natafuta kiwanja Goba

Natafuta kiwanja Goba

Old Member (Retired)

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2012
Posts
3,401
Reaction score
1,618
Natafuta kiwanja Goba chenye ukubwa wa meters kati ya 1500-2000.Kama kipo niambie kipo Goba sehemu gani, kina ukubwa wake halisi na bei yake hapa hapa jukwaani kabla hatujaingia PM.

NB: Ukubwa wa kiwanja na bei yake ni lazima zitajwe hapa wazi, biashara za kujificha ficha huwa sizitaki.

Asante.
 
mfetere umenitumia pm kuwa kiwanja kinauzwa milioni 35, hujaniambia kina ukubwa gani? naomba uweke hapa wazi biashara ya viwanja si ya madawa ya kulevya mpaka tujifiche
 
Last edited by a moderator:
Kuna jirani yangu ndio mmiliki wa hiko kiwanja nimeshakiona bahati mbaya picha zake sina coz nimebadili cm kubwa wa nusu heka.
 
Kuna jirani yangu ndio mmiliki wa hiko kiwanja nimeshakiona bahati mbaya picha zake sina coz nimebadili cm kubwa wa nusu heka.
kwenye PM umesema wewe ni mmliki wa kiwanja hicho hapa unasema kiwanja cha jirani yako, hueleweki mbona ndiomaana sipendi biashara za siri siri
 
kunamatapeli sana kwenye hizi biashara za humu. kunajamaa niliona tangazo lake kwenye mtandao wa ujenzi zone. tukakubaliana kuonana huko goba kulangwa karibu na madale. Tukaonana akanionesha kiwanja na document za serikali ya mtaa. Na siku hiyo alikuwa na kanjanja mmoja aliyejidai kiongozi wa serikali ya mtaa. Siku ya kulipana tukakubaliana tukutane saa nane mchana. Mimi nikaenda hasubuhi nikafika serikali ya mtaa nikawaeleza. Wakaniambia huyo jamaa anayejidai kiongozi wa serikali ya mtaa ni uongozi uliopita ambao walikuwa mafisadi sana na wamesha waliza watu wengi. Tukaingia mtaani kuwatafuta wajumbe ili tufanye utafiti wa nani mmiliki wa eneo husika. tukafuatilia majirani na watu wanaofahamu. tukaja kugundua mmiliki ni Dr. mmoja wa mlimani. Jamaa alivyo kuja nikamwambia nipo serikali za mtaa akaingia mitini. Nikipiga sm hapokei.
 
Huwe makini mimi mwenyewe mpaka leo ninatafuta kiwanja lakini nimeamua kulifanya taratibu.
 
Sawa supu ya mawe kweli matapeli wapo humu jf nimeshawauzia watu viwanja mpk vya mil 50 na kadhalika na sijawahi pata taarifa zozote zile kama nimeshawahi mtapeli mtu yyte.
 
Sawa supu ya mawe kweli matapeli wapo humu jf nimeshawauzia watu viwanja mpk vya mil 50 na kadhalika na sijawahi pata taarifa zozote zile kama nimeshawahi mtapeli mtu yyte.

Tutajie member uliyemuuzia kiwanja.
 
Nauza kiwanja kina title deed sqm 1586, kipo block 4 buyuni chanika, million 17 tu, maelewano yapo.
 
Natafuta kiwanja Goba chenye ukubwa wa meters kati ya 1500-2000.Kama kipo niambie kipo Goba sehemu gani, kina ukubwa wake halisi na bei yake hapa hapa jukwaani kabla hatujaingia PM.

NB: Ukubwa wa kiwanja na bei yake ni lazima zitajwe hapa wazi, biashara za kujificha ficha huwa sizitaki.

Asante.

Nenda Goba mwisho(centre) ulizia kwa mwanambilimbi alikua diwani mstaafu ana viwanja kibao.
Onyo madalali amtakiwi.
 
kunamatapeli sana kwenye hizi biashara za humu. kunajamaa niliona tangazo lake kwenye mtandao wa ujenzi zone. tukakubaliana kuonana huko goba kulangwa karibu na madale. Tukaonana akanionesha kiwanja na document za serikali ya mtaa. Na siku hiyo alikuwa na kanjanja mmoja aliyejidai kiongozi wa serikali ya mtaa. Siku ya kulipana tukakubaliana tukutane saa nane mchana. Mimi nikaenda hasubuhi nikafika serikali ya mtaa nikawaeleza. Wakaniambia huyo jamaa anayejidai kiongozi wa serikali ya mtaa ni uongozi uliopita ambao walikuwa mafisadi sana na wamesha waliza watu wengi. Tukaingia mtaani kuwatafuta wajumbe ili tufanye utafiti wa nani mmiliki wa eneo husika. tukafuatilia majirani na watu wanaofahamu. tukaja kugundua mmiliki ni Dr. mmoja wa mlimani. Jamaa alivyo kuja nikamwambia nipo serikali za mtaa akaingia mitini. Nikipiga sm hapokei.

Me nilitaka kulizwa bunju ,jamaa wameokota hati mtu alidondosha wanajifanya ya kwao wanauza kiwanja, nikawaomba copy nikaenda ardhi kucheck kumbe hati hiyo imesharipotiwa imepotea na mwenyewe kaomba mpya, namuuliza aliyeweka tangazo hapo anawatetea hao watu kwamba kiwanja ni chao nikamwambia kesho njooni ardhi tukahakikishe hajaja huyo mtangazaji aliyeweka tangazo hapa wala mmiliki kwa hiyo jamani kuweni waangalifu kuna utapeli mwingi unaendelea hapa usipokuwa mwangalifu mtu unaweza kulizwa hivi hivi
 
Bado hujapata kiwanja? Ninadhani naweza kukusaidia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom