natafuta kiko

Crucifix

JF-Expert Member
Feb 20, 2011
1,651
588
Jamani natafuta kiko (mtemba wa kuvutia tumbaku). Babu yangu anasema atanipa laana nisipomletea. Nimejitahidi kumweleza madhara ya tumbaku lakini kasema ameanza kuvuta tangia zama hizo. Kiko chake kimevunjika na hakifai tena anasema alikinunua wakati wa azimio la Arusha. Nimepita madukani hakuna nimeona bure nije hapa, hata kama babu yako alikuachia urithi we niuzie nikamfurahishe babu yangu.
 
Arusha vipo mkuu jaribu kucheki na watu wa Arusha wakusaidie
 
Jamani natafuta kiko (mtemba wa kuvutia tumbaku). Babu yangu anasema atanipa laana nisipomletea. Nimejitahidi kumweleza madhara ya tumbaku lakini kasema ameanza kuvuta tangia zama hizo. Kiko chake kimevunjika na hakifai tena anasema alikinunua wakati wa azimio la Arusha. Nimepita madukani hakuna nimeona bure nije hapa, hata kama babu yako alikuachia urithi we niuzie nikamfurahishe babu yangu.
Duh Mkuu hiyo kitu imenikumbusha mbali sana, Kulikuwa na Mzee jirani yetu, Miaka hiyo ya nyuma, alikuwa akifanya kazi rwele (TRC), alikuwa na Sharubu za haja na kutwa yupo na Kiko yake mdomoni, alikuwa akijiita Mdachi (Mjerumani) .....................
 
nenda kwa mafundi wa kuchoma vyuma, hiyo kazi ni rahisi kwao.
 
Una idea Arusha sehemu gani? Maana kwa kweli nikikipata babu yangu atacheza kiduku siku siku hiyo


Kama ni mwenyeji Arusha nenda kwenye maduka yaliyopo kwenye majengo ya TFA upande wa EXIM bank nakumbuka kuona kiko kikiuzwa hapo. Ni karibu pia na Shoprite
 
Pia unaweza kujaribu pale Mwenge kwa wachonga vinyago kuna siku niliona hiyo kitu.
 
kwa hyo uko serious utalaaniwa kisa kiko au unatuletea mazilizala unataka kutumia mwenyewewe
 
313530_445842918781882_225886312_n.jpg
 
Ngoja nikuulizie kwa rafiki yangu mmoja anaitwa Mzee Bantu. Huyu mzee alia ni mkufunzi pale NIT Dar es salaam (amestaafu) na hata tumbaku havuti tena. Sasa sema unazo shilingi ngapi nichome mafuta sasa hivi? Najua atakuwa navyo kadhaa kwenye makumbusho yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom